Ni sababu ipi muhimu sisi wazazi tunakuwa na mtoto zaidi ya mmoja?

Ni sababu ipi muhimu sisi wazazi tunakuwa na mtoto zaidi ya mmoja?

Watu wawili muungane halafu mzae mtoto mmoja basi binadamu wataisha.

Kule Tailand kuna kisiwa watu hawataki kuzaa ila tambua hilo kundi lenye imani hiyo lishaanza kutokoweka maana wanakufa bila ya kuzaliana...Dunia haiwezi kuvumilia mitazamo ya kipumbavu la sivyo mtapotea wote.
 
Hivi ukoo wako ili udumu unahitaji mtoto wa kiume au wa kike?
Mali zako ukiondoka duniani zintakiwa kuangaliwa na nani?
Mkuu, ukiondoka; mali unazoziacha sio zako tena... ni za warithi/ uliowaacha hai.

Wao ndio watajua wanaziangaliaje, kama wakizinywea bia au wakiamua tu kuzitom#bea hadi ziishe wewe haikuhusu kabisa! [emoji41][emoji23]
 
Sasa issue kubwa nataka kufahamu nimeona kama nimeridhika

Mkuu sababu pekee ni kuridhika na kutokuridhika...

Wewe umepata mmoja na umeridhika kabisa (umeona ndiyo riziki), wengine watataka wawili, watatu na kuendelea...

Baada ya kuwa na hamu ya watoto kadhaa, wapo wanaotazama uwezo wao kiuchumi, mwanaume au mwanamke sahihi wa kulea naye familia, jinsia ya watoto n.k n.k
 
Habari za muda huu ndugu zangu. Nimekaa, nikafikiria, Mimi ni mzazi wa mtoto mmoja wa kike.

Sasa issue kubwa nataka kufahamu nimeona kama nimeridhika au sina sababu maalumu ya kuongeza mtoto. Najiweza sana kiuchumi, mimi kijana mdogo ila mwanangu yupo anaishi na mama yake Uingereza (Mama mtanzania age 27) nilimpeleka mwenyewe. Anajiweza. Na pia sipo nae kimahusiano kwa sasa ila nina mtunza huyu binti.

(Nia nikutoa point za uchumi na uhusiano). Sasa sina Wazo lolote la kuongeza mtoto, yaani nina mapenzi yaliyopitiliza kwa huyu niliye nae.

Wazee sababu ipi inafanya mtu awe na watoto zaidi ya mmoja au wengine kupitiliza hadi watano. Nini sababu?

Au huwaga ni bahati mbaya tu, mimba hiyo?
So long as uko na nguvu za kiume na unatomba basi Watoto kuja kawaida tu Mkuu, labda kama sijakuelewa
 
Mkuu wewe humu ni kama Senior sikutegemea kama ungemjibu maneno haya Tena mtoto wa kike.Kibaya zaidi una heshima kubwa humu mwenye thread kapotezea wewe ukaamua kununua kesi.Naamini sio Kiranga yule tunayemjua kama atakuwa ni yeye basi account Kuna wahuni wamehack.
Mkuu,

Mimi nina heshima kwa wenye heshima.

Ukileta ukauzu mimi ni kauzu kupita maelezo.

Na hizo heshima mnazonipa kama zinanizuia mimi kuwa huru, kuwa Kiranga original, kuwa Kiranga authentic, basi sizitaki.

Kwangu mimi, kuwa huru nikasema ninachotaka ni muhimu kuliko hizo heshima mnazotaka kunipa.

Ikiwa hizo heshima zitazuia uhuru wangu, basi hizo heshima zitakuwa mzigo tu, zitakuwa mtego wa kunitega nisiwe huru, nisiwe my authentic self, niwe Kiranga feki anayeogopa kusema anavyojisikia kweli eti kwa sababu watu watamuona hivi au vile.

Nakuomba sana nivue hizo heshima ulizonibandika ili nipate wepesi kujieleza.

Naona heshima hizo zinanitia udhia na mzigo tu.

Falsafa zangu ni tofauti sana na zako, usilazimishe zako ziwe zangu wakati mimi sizielewi wala sizikubali.

Ushanifahamu?
 
Mkuu,

Mimi nina heshima kwa wenye heshima.

Ukiketa ukauzu mimi ni kauzu kupita maelezo.

Na hizo heshima mnazonipa kama zinanizuia mimi kuwa huru, kuwa Kiranga original, kuwa Kiranga authentic, basi sizitaki.

Kwangu mimi, kuwa huru nikasema ninachotaka ni muhimu kuliko hizo heshima mnazotaka kunipa.

Ikiwa hizo heshima zitazuia uhuru wangu, basi hizo heshima zitakuwa mzigo tu, zitakuwa mtego wa kunitega nisiwe huru, nisiwe my authentic self, niwe Kiranga feki anayeogopa kusema anavyojisikia kweli eti kwa sababu watu watamuona hivi au vile.

Nakuomba sana nivue hizo heshima ulizonibandika ili nipate wepesi kujieleza.

Naona heshima hizo zinanitia udhia na mzigo tu.

Falsafa zangu ni tofauti sana na zako, usilazimishe zako ziwe zangu wakati mimi sizielewi wala sizikubali.

Ushanifahamu?
Hahaha huyo ndo Kiranga. Anapiga spana na kufundisha.
 

Kwanza kabisa narudia tena kuzaa vyovyote au kutozaa kabisa ni haki ya kikatiba na kiutu, hakuna jinsi ya kuiingilia haki hii bila kuvunja haki za kikatiba na za kiutu.

Kwa hivyo, hapa naandika majadiliano ya kifalsafa na kidhahania, simshawishi mtu azae au asizae, simlaumu mtu kwa kuzaa au kutozaa.

Having said that:-

Watoto wote watakufa, sasa unaposema ni risk sana kuwa na mtoto mmoja una maana gani?

Ukiwa na watoto wengi hawafi?

Mtu mwingine anaweza kukuambia kuwa ni maadili mabaya kumzaa mtoto katika dunia ambayo unajua ina risk kubwa na matatizo mengi.

Yani hiyo high risk ya mtu kuweza kufa Bongo ni sababu ya kutozaa watoto wengi, si sababu ya kuzaa watoto wengi.

Kwa sababu ukizaa watoto wengi katika nchi yenye risk kubwa ya watoto kufa, maana yake umewafanya watoto kuwa expendable, maisha yao hayana thamani, unawazaa kwa mchezo wa kamali ya pata potea.
 
Aah, wewe unaweza kuona ukweli kumbe unatuletea shombo tu.

Mtu kauliza swali, hajakuuliza wewe.

Anapata michango ya watu wengine kumjibu.

Wewe kinachokuuma nini?

Kama hupendi hiyo mada kwa nini usiiruke tu uende kwenye mada unazopenda?

Ulitaka kumzalia mtoa mada mtoto wa pili akakukatalia, ndiyo maana unatuletea kisirani chako hapa?

Au uko mwezini unasumbuliwa na hormones?
Weee komaaaa, huyo mgumba anazo mbegu za kuzalisha kwanza, nyie wote wagumba mmejaribu wee imeshindikana ndio mnakuja kujishaua hapa ooh mtoto mmoja inatosha badala muombe tiba ya ugumba wenu mnataka kujifariji washamba wakubwa,

Ikikuuma chomoa
 
Suala la kuzaa watoto wangapi, au kutozaa kabisa, ni la utashi wa mtu binafsi. Ni haki ya mtu binafsi. Hapo hakuna mwanya wa haki hiyo kuingiliwa bila kuvunja haki za kikatiba na za kibinadamu za huyo mtu.

Ila.

Kuzaa kwa hesabu zozote za watoto kuja kukusaidia kwa namna yoyote baadaye ni aina fulani ya biashara, tena biashara ya utumwa.

Watu wanatakiwa wazae bila mategemeo yoyote ya kulipwa fadhila yoyote na watoto, hata ya kutunzwa uzeeni. Wajiwekee mipango yao wenyewe.

Kwa sababu.

Kwanza mtu hawezi kujua kwamba mtoto wake ataishi maisha marefu kumpita yeye. Inawezekana mtoto akafariki awali.

Pili, si maadili mema kuzaa kwa lengo la kibiashara. Kwamba mimi namzaa mtoto namtunza ili naye aje anitunze. Hiyo si familia, hiyo ni biashara ya kutunzana.

Vipi kama mtoto hana interest yoyote ya kutunza wazazi, yeye anataka kuishi kwa uhuru wake akae mbali akiendesha maisha yake? Hiyo ni haki yake. Utataka aache maisha yake amtunze mzazi?

Hiyo ni sababu moja ya kibinafsi kabisa ya kuzaa watoto.

Sisemi kwamba kumtunza mzazi ni kitu kibaya, nasema kwamba, mzazi kuweka mahesabu kwamba nazaa watoto wengi waje kunitunza vizuri baadaye ni kama kuwafanya wale watoto ni watumwa wake, kazaa watumwa wengi waje kumtumikia, kawekeza kibiashara, hajazaa kifamilia.
umemamaliza
 
Back
Top Bottom