Ni shule gani ya sekondari ilijengwa na wakoloni Waarabu halafu Serikali ikaitaifisha baada ya uhuru 1961?

Ni shule gani ya sekondari ilijengwa na wakoloni Waarabu halafu Serikali ikaitaifisha baada ya uhuru 1961?

Habari wadau.

Nasikia baada ya kupata uhuru mwaka 1961 Serikali ilitaifisha shule zilizojengwa na wakoloni

Mfano shule zilizojengwa na wakoloni wazungu kama Minaki, Ilboru, Pugu, Mazengo, forodhani, etc

Je ni shule zipi zilitaifishwa ambazo zilijengwa na wakoloni waarabu?

Maana waarabu walitangulia kuja Tanganyika na Zanzibar kwa kwa miaka zaidi ya 500 kabla wakoloni wazungu hawajaja.

Zanzibar pia waarabu walifika mapema sana maana msikiti wa Kazimkazi ulijengwa mwaka 1006 AD, waarabu walitawala kwa miaka mingi Zanzibar na walifika mapema sana, naomba mnitajie ni shule gani ya sekondari waarabu walijenga Zanzibar, na ilijengwa mwaka gani?
Mkuu, ikiwa lengo la uzi ni kujifunza basi nikujulishe tu kuwa zipo shule kadhaa zilizojengwa na muarabu tena si serikali bali mtu ama watu binafsi.

Tofauti na wazungu muarabu hakuwahi kuwa mtawala wa Tanganyika bali visiwani na baadhi ya sehemu ya bara ambayo ilikuwa kama strip ili afanye biashara zake na aweze kusafiri bila bughuza.

Mwaka 1882 Sewa Haji Paroo aligawa jengo la ghorofa tatu kuwa shule ya kwanza ya watu mchanganyiko Tanganyika. Shule hii ipo hata sasa ninavyoandika kwenye tarafa ya mwambao kata ya Dunda Bagamoyo. I grew up next to the school na I can say nimeona legacy ya mwarabu.

Binafsi ni muhusudu wazungu kweli na nimepita na kusoma kwenye shule za wazungu lakini nikiri sijaona mzungu mwenye roho ya utu kama aliyokuwa nayo Sewa Haji Paroo. Nimepita Ilboru naifahamu historia ya shule tangu ikiwa Lushoto mpaka kuhamia Arusha na kutaifishwa. Unlike Mwambao ambayo iliruhusu mtu wa dini na rangi yeyote kupata elimu you cant Say the same kwa shule nyingi za wazungu.

Kwenye swali lako umeuliza kwanini hakuna shule iliyotaifishwa ni kwasababu waarabu waliamini kwenye sadaka na hawakuhodhi shule yeyote kama mali yao.

Mwisho sijapata kuona uzi ulioanzishwa kwa minajili ya chuki kama huu.
 
Kuna sehemu moja huwa inaitwa "Maskati" sijui kama kuna shule kule ila hao jamaa wamekaa kule kinachonishangaza kule ni bushi kichizi ilikuaje miamba wakakaa huko
Sio huko tu hata sehemu za Tanga, kwa miaka hii bado ni porini, na wao waliishi miaka hiyo hata kabla ya Uhuru. Kwa kweli ni watafutaji sana.
 
Sijasema Wakristu ndio wasomi zaidi Tanzania hapana, dini zote Zina wasomi wabobezi kwenye nyinja mbalimbali. Lakini asilimia kubwa ya wasomi wote Tanzania, wamenufaika au kutumia kwa njia Moja au nyingine miundombinu ya elimu iliyotengenezwa na kanisa. Hivyo hata wakati tunawarushia madongo tukumbuke ukweli huo, tuwatambe na angalau tuwaheshimu kwa hilo.

Wamisionari wa Kikristu walikuwa wanajenga vitu mapacha vitatu. Kanisa, shule na hospitali. Ila waarabu wao walijua na mpaka Sasa hivi wanajenga kitu kimoja tuu
Ungekuwa umeisoma na kuelewa historia ya Tanganyika na ujio wa hawa watawala, kama wewe ndiye ulieandika mada hii utajiona mjinga.

Dini zilikuja kama biashara hasa baada ya utumwa kuanguka, kipindi cha biashara ya utumwa dini zilikua za mababu tu, mtumwa hawezi kwenda kanisani wala msikitini.
Hebu fuatilia kuhusu biashara ya utumwa na mateso yao, na kuabudu hizi dini za kigeni kama kuna endana, utakua umeona kama si video hata picha za mfano juu ya maisha ya mtumwa.

Ilipo anguka biashara ya utumwa, ndipo walipokuja na biashara kupitia dini, sasa kwenye biashara kuna kushindana kuwavutia wateja. mwarabu alipokuja alikua anauza maneno tu, mzungu mmissionali akaja na kujenga makanisa mazuri, shule na hospital, ili kuvutia Watu.

Ukifuatlia kwa makini utaona waliwekeza zaidi maeneo ya pwani kuliko bara, ambako mwarabu hakufika.
 
Mimi sijasema kama tabora boys na girls zimejengwa na mzungu.

Ngoja nikupe mfano wa ushahidi kuhusu shule za wazungu

mfano wa kwanza ILBORU
Ilboru School was opened in 1946 as a lutheran school and was managed by the Lutheran Church until 1969 when it became a government school.

Mfano wa pili PUGU

Pugu high school was then know as St. Francis College Under Roman Catholic Church with the famous slogan "Docebit Vos Omnia" meaning "Teach you things"...
Pugu Secondary School is located in the outskirts of Dar es Salaam. There are about 800 students.
In the early 1950s, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere was the only indigenous teacher.


Mfano wa tatu Minaki

In 1970 Minaki school was taken over by the government from the Anglican Missionaries.


Nataka maelezo kama hayo kuhusu tabora girls na tabora boys kwamba serikali ilizitaifisha kutoka kwa Waarabu gani ama taasisi gani ya ki arabu uitaje jina na mwaka gani ?
Mkuu huwezi taifisha jambo ambalo halijahodhiwa. Licha ya kuwa ruthless Kwenye biashara ya utumwa and other miseries mwarabu ni mtu wa sadaka sana. They gave kuliko kumiliki and waliopewa ni wakoloni. Sewa haji alicomision ujenzi wa shule ya Mwambao na hospitali ya Bagamoyo I grew up in Bagamoyo and nina hadithi yakukupa.

Alicomission majengo mengi pia ambayo baadae yalitwaliwa na kuwa ofisi za serikali mfano Arab Tea House. Very fine establishments. Mwarabu hakuwahi kuwa mtawala wa Tanganyika hata kipindi anafanya biashara (utumwa na the likes) bado Tanganyika ilikuwa na viongozi wao and they actually Traded na mwarabu as they liked.

Tumetarnish sana image ya mwarabu kwasababu ya utumwa na tumesahau mchango wa viongozi wetu wenyewe kwenye hilo. Wakati mwarabu anatua pwani ya Bagamoyo alikuta Chief Pazi ni mtawala and they respected each Other na jamaa akawa anampa ramani ya namna yakupata watumwa wakinyamwezi. Machief wa kinyamwezi wamechangia sana kwenye hii biashara.

Back to the topic....muarabu hakuwahi kujijenga nje ya mwambao wa pwani na huko ndiko utakapoona legacy yake kwenye hizo shule na huduma zingine. Nimesemea mwambao sababu naifahamu lakini najua zitakuwepo nyingi shule za ufadhili wa waarabu from Lamu to zanzibar.
 
Mwarabu alitawala lini TANGANYIKA? Maana hata biashara ilikuwa karne ya 18 huko, Nchi yetu ilitawaliwa na WAJERUMANI NA WAINGEREZA (WALISHIKIA TU).
Hata hao wajerumani hawakujenga sana Shule zaidi ya Makanisa, na Ofisi zao kama ile IKULU yetu.

Watanzania kwann kila siku mnapenda kutumia matako kwenye kufikiria??

Swali lilipaswa kuuliza ni nchi gani iliwahi kutawaliwa na Waarabu? Then anzia hapo kuuliza kama walijenga shule au hapana.
Mwarabu hakutwala bali, alikua mfanya biashara, ila wengi hapa hatuijui historia ya Tanganyika, tunaiongelea Tanzania.
 
Waarabu hawa kujenga shule ila tunapata faida kutoka kwenye magofu yao ya kaole bwagamoyo na mji mkongwe Zanzibar na kuingineno watalii wanachangia pesa nyingi sana kupitia magofu hayo ya kilwa nk

Wazungu walijenga shule ambazo kabwela uwezi soma shule hizo walio soma shule hizo ndio walio kuwa vibaraka wao mpaka kesho
Sasa akili za aina hii kweli utaona umuhimu wa elimu? Serious kabisa mtu mzima amevaa bakuli kichwani anakwambia magofu ya Bagamoyo ni bora kuliko shule? Serious??....
 
Taja shule zilizojengwa na waarabu. Haya uliyoaandika ndiyo ujinga wenyewe. Unauliza hivi unajibu vingine. Amesema waarabu ila tayari umeenda kwenye udini. Hapa hatuongelei udini. Kuna waarabu waislamu, wapagani na wakristo. Uliambiwa Wajerumani au wazungu ni wakristo tu? Kuna wapagani na waislam pia.
Ujinga wako uko wazi, ila mjinga huwa hajielewi kuwa mjinga.

Hakuna mada ambayo haina yatokana yo, Ukieleza sababu za Wamissionali kujenga makanisa shule na hospitli unawafungua watu wanaopenda kujifunza, histolia unajio wa koloni Tanganyika.
 
Tanganyika haikutawaliwa na mwarabu, halafu shule zote zilizojengwa na wakoloni Wazungu zilitokana na unyonyaji na ukandamizaji dhidi ya mtu mweusi.
 
Tanganyika haikutawaliwa na mwarabu, halafu shule zote zilizojengwa na wakoloni Wazungu zilitokana na unyonyaji na ukandamizaji dhidi ya mtu mweusi.
Unyonyaji na ukadamizaji waliofanya waarabu wenyewe haukusaidia kujenga shule ila ulisaidia kujenga makanisa tu
 
Sema tu waislamu walinyang’anywa viwanja vyao hata ilipo DUCE ni kiwanja chao
Si tunazungumzia viwanja au shule? Kama kila taasisi ikisema irudishiwa hivyo unavyoviita viwanja basi unaeza kuta huyo mwanao anayesona hiyo shule ya kata yuko seminarini
 
Mwarabu alitawala lini TANGANYIKA? Maana hata biashara ilikuwa karne ya 18 huko, Nchi yetu ilitawaliwa na WAJERUMANI NA WAINGEREZA (WALISHIKIA TU).
Hata hao wajerumani hawakujenga sana Shule zaidi ya Makanisa, na Ofisi zao kama ile IKULU yetu.

Watanzania kwann kila siku mnapenda kutumia matako kwenye kufikiria??

Swali lilipaswa kuuliza ni nchi gani iliwahi kutawaliwa na Waarabu? Then anzia hapo kuuliza kama walijenga shule au hapana.
Mvaa kobazi umekuja speed sana.
 
Da! Maisha yamebadilika sana, enzi hizo Forodhani Sec. School tunasoma na watoto wa vigogo, yaani ni STK na STJ zinapishana kuleta na kufuata pisi kali za Barabara za Bagamoyo na Mwai Kibaki.. Siku hizi ni wanahesabika watoto wa mjumbe wa nyumba 10 kumkuta Shule ya Kata...
Halafu kuna dizaini ya akina "Chivaro" nao tulikuwepo.
 
Sasa akili za aina hii kweli utaona umuhimu wa elimu? Serious kabisa mtu mzima amevaa bakuli kichwani anakwambia magofu ya Bagamoyo ni bora kuliko shule? Serious??....
Hiyo elimu uliyo/ mliyonayo haina faida kwa taifa
Nenda Oman,dubai,Qatar kuwait jibu utalipata
 
Back
Top Bottom