Ni smart TV gani 4K kwa sasa ipo vizuri sana?

Ni smart TV gani 4K kwa sasa ipo vizuri sana?

Google now kuna baadhi ya search ukitafuta inafanya kazi kama AI Open(chatgpt)hawakuletei Web iliyoandika,wanaleta data ambazo zipo rated Web nyingi....
Nmekupata unachomaanisha wana sum up statistics za website zilizoandika sio kama ni hivyo nimekupata mkuu
 
Si sawa, kwenye TV cha muhimu ni ubora wa kioo. Sio sawa kabisa na simu. Simu ina mambo mengi maCPU, maGPU huko na makolokolo kibao.

Turudi kwenye TV sio simu hizo Samsung ni nzuri lakini ni overpriced. Ukinunua Samsung ya milioni 1 unachomzidi mwenye Hisense ya laki sita ni jina la brand tu yaani laki nne yote unakuwa umelipia brand na laki sita ndio actual value ya product
Lakini kuna baadhi ya Tv zina mambo mengi kama simu tu, lakini mpaka upate smart tv zinazo tumika ulaya kwasababu Smart TV za Dunia ya kwanza zina mambo mengi kuliko smart tv za kariakoo au zinazo letwa nchini.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Chief-Mkwawa Ufafanuz kidogo hapa. Ni ipi nzuri kati ya Google Tv vs Android Tv based on their x-sticks
Kwa ufahamu wangu Google TV na Android TV ni kitu kimoja atleast kwa miaka ya karibuni.

Zamani miaka iliopita Google TV ilikuwa kwenye chromecast ilikuwa ni OS tofauti kabisa.

Ila Chromecast za sasa na Tv zote ambazo zinatumia Google TV ni android tv, Google TV ni launcher tu on top of Android TV.
 
Lakini kuna baadhi ya Tv zina mambo mengi kama simu tu, lakini mpaka upate smart tv zinazo tumika ulaya kwasababu Smart TV za Dunia ya kwanza zina mambo mengi kuliko smart tv za kariakoo au zinazo letwa nchini.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Hata Ulaya Zipo smart za kutosha tu zisizo na mambo mengi.

Zipo Proprietary Os kama
-Roku TV
-Tizen ya Samsung
-Web Os ya LG
-Vidaa ya Hisense etc

Zote hizo hazina mambo mengi haijalishi unanunua wapi ulaya ama kariakoo utakuwa umefungiwa.

Zipo Os ambazo zipo open kama Android tv, Harmony ya Huawei na os nyengine ambazo zinabase na Distro za linux zipo open haijalishi unanunua TV wapi.

Pia waweza badilisha TV yoyote ile kwa kutumia tv box ikawa smart kadri unavyotaka.
 
Wadau nilikuwa na smart TV 4 K nchi 50 wale wajaa laana wakasepa nayo.

Nina Samsung Hd nchi 32 ilikuwa chumbani ndio nimeileta sebuleni yani tofauti ni kubwa sana.

Sasa nimeokota pochi la mzungu nataka ninunue TV ya kweli nirudi kwenye modern life.

Karibuni kwa ushauri.
Next time funga tracker kama ni tv yenyewe kubwa na ni top brand.
 
Kama hujui features bora ukae kimya tu, , kioo cha amoled kinagharimu mara tatu zaidi ya lcd, na aliyetumia amoled huwezi mrudisha kwenye lcd .
Hujui features za magic remote na inaonyesha hujawai tumia , unhejaribu ungenielewa
Pungufu moja la hisense ni sound quality ,

image-2023-01-20-20:08:48-018.jpg

Magic remote ni hiyo kwa wasio ijua. hii remote ikiharibika bei yake dukani haipungui 200k yaani ni sawa na TV ya Aborder ya 32" [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
View attachment 2489230
Magic remote ni hiyo kwa wasio ijua. hii remote ikiharibika bei yake dukani haipungui 200k yaani ni sawa na TV ya Aborder ya 32" [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
Bora umesaidia, ila wabongo ukiwatajia bei tu wanaweza ku assume unajidai
,wape na features za hiyo remote ili wajue
By the way lg thinQ app ina uwezo wa kufanya kaz kama hiyo remote
 
Wakuu kwema? Samahani kwa budget ya 400k naweza pata tv gani nzuri inch 32 ambayo ni HD?

PS niko mbeya
 
Sharp hata kwenye fridge wapo njema sana.
Bado kwenye fridge lg anaongoza kwa africa
Lg ndo alikuwa wa kwanza kuleta linear compressors,ambazo zina inverter,
Sharp ana vitu imara sana ila tech zake sio nzuri
 
Kwa upande wa Tv na home theater SONY wanaongoza,
Kwa upande wa smartphone SAMSUNG wanaongoza
Ac, washing machine, fridge ni LG.
Chaguo ni lako
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hamn tv hapo
sas usiombe ukutane na cam za tbc
Nakupa research mzee nenda kweny vibanda umiza na sehemu za betting zile Tvs zao zinapiga kazi kama zikiwasha saa moja asubuhi mpaka saa 6 usiku then angalia zile brand ni za wapi? Then uje kukuta izo LG ,Samsung ,Sony ni nadra sio Tvs za kazikazi ni ubishoo.
 
Wakuu kwema? Samahani kwa budget ya 400k naweza pata tv gani nzuri inch 32 ambayo ni HD?

PS niko mbeya

Kaka TV ya 32" ni ndogo japo sijui matumizi yako. Go for atleast 43. pia ongeza pesa kidogo kufikia 550k utapata TV nzuri ya level yako.
 
Back
Top Bottom