Ni Tanzania pekee ambapo ujinga unatetewa na kundi kubwa la watu

Ukiona nchi ambayo bado ina shule ambazo wanafunzi wanakaa chini hosipitali hazina dawa maeneo kibao hadi baadhi ya miji haina maji safi na salama, viongozi wakitembelea magazi ya hadi bilioni shilingi katikati ya ushuru mkubwa kuliko nchi yeyote duniani basi tambua raia wa nchi hiyo ni watu wasiojitambua na kwamba watawala wamewafanya mifugo yao.
Watawala kwa Tanzania hakuna tofauti na mfugaji aliyeweka mbuzi zake kwenye zizi anaziswaga apendavyo
 
Yupo mahali ambapo muumba wake ameona kazi yake njema na amempenda zaidi!.Kama alichokifanya ni dhuluma basi watanzania hususan masikini wanaufurahia sana huo udhulumaji na wala hawatomsahau kamwe! Kama dhuluma zilitoa pesa kwenye mifuko ya MAFISADI zikawapelekea mahospitali, Elimu bure, miundombinu Bora, maji n.k basi hakika hiyo ilikuwa dhuluma nzuri sana!

Dhuluma mbaya ni maskini anapotuma vijisenti vya matibabu kwa mgonjwa wake anapikatwa kodi! Dhuluma ni pale wananchi wanateseka huduma mbovu za afya serikali inatumia mabilioni kufanya royal tour! Dhuluma ni wananchi kutozwa kodi za kila aina ili kiongozi apande ndege kuhudhuria kikao kujadili athari za gesi ya ukaa!
 
 
Maskini wa Tanzania wana husda, wanataka watu wote wawe kama wao. Walishangilia matajiri walipofilisiwa na viongozi walipotumbuliwa kumbe njaa ikazidi kuwapiga wao
 
Wewe unaishi wapi mkuu.? Wewe mtu wa taifa gani.?
 
Dhuluma kuu ni kumsema vibaya marehemu ambaye ni barafu wa moyo wa raia wanyonge huku ukitetea wanyonyaji
 
iko dhahiri sana, uwakilishi wa wananchi una dosari kubwa ni matokeo ya kukandamizwa kwa demokrasia, tuna wabunge waliochaguliwa na mkurugenzi wa tume ya uchaguzi, kazi yao ni kulia na kupiga sarakasi bungeni na hayo ma covid 19
Sasa kuna haja gani kuwa na demokrasia inayotetea unyonyaji badala ya kuleta equity kwenye jamii? Mafisadi oekee ndio mtatetea huu udhalimu.
 
Sasa kuna haja gani kuwa na demokrasia inayotetea unyonyaji badala ya kuleta equity kwenye jamii? Mafisadi oekee ndio mtatetea huu udhalimu.
 
ukiona mtu ana hasira na maiti hali mbaya sana
 
sisi wafuasi wa jiwe tuna akili,sio watu wa kufuata kila ushauri maana wengine tunawajua.
 
 
Upuuzi tu. Huyo azarry na ben saa nane wakipotea kwa upingaji wao maendeleo, na hiyo 1.5 tr hewa ndio utalinganisha na maendeleo makubwa yaliyofanyika kwenye uwekezaji kwenye miundombinu afya na uboreshaji wa utawala kwa kupunguza rushwa na ufisadi?
Nani anayemtuma mwenzake, mpiga au mpigiwa kura?
 
Kwa mtazamo wangu jiwe kama mwanadamu mwingine yoyote Yule ana mazuri yake na mapungufu yake,Hilo lipo wazi kabisa.

Kwa maoni yangu alifanya mengi mazuri Kwa inchi hii ambayo hata mwananchi wa kawaida aliweza kuyaona,aliwatetea wanachi wake na kujitahidi kupunguza changamoto zao Kwa kiasi Fulani.

Inchi ilipofikia kipindi kile ilimhitaji mtu kama yeye kuyaweka mambo Sawa,maana Uhuru ulizidi Sana,ilifikia kipindi eti watu wanaenda kufanya mikutano ulaya Kwa ishu zinazo husu mambo ya hapa Tanzania,ukiuliza eti Tanzania haina sehemu za kufanyia vikao? Ebu angalia inchi ilipokuwa imefikia,nadhani wote mnakumbuka Ile ishu ya kupakwa rangi ndege za ATCL, ilikuwa ikatumike zaidi ya SHS mil 200 eti kupaka rangi ndege,mwisho wa siku watanzania walipaka Kwa mil 5 ingawa jembe akawaongezea ikafika 10,sasa ebu angalia Hali jinsi ilivyokuwa mbaya.

Kuna watu walikuwa wanalipwa mshahara mpaka milioni 40,wengine hela za maendeleo zilikuwa zinawekwa benki wapate riba huku miradi ikicheleweshwa Kwa manufaa Yao,kwahiyo hayo ni machache Tu, ilihitajika kuwa na kiongozi wa Kariba Ile ili walau kuyaweka mambo Sawa, sisemi aliweza kufanikiwa Kwa asilimia zote lkn alifanya alichoweza.

Itakuwa si Busara kumlaumu jiwe Kwa kila kitu,na kuona mabaya yake Tu,hapana tuwe wa kweli wa nafsi zetu Kwa kumpongeza Kwa mazur aliyofanya pia. Itoshe kusema kuwa alifanya kile alichoweza kufanya,na tukiacha unafiki pembeni wengi wetu tunaukubali mchango wake.

Natambua kuwa vile vile pia kama kiongozi yoyote hakosi mapungufu ya kiutawala,hata mwalimu Nyerere binafsi alikiri kuna mambo alikosea kama kiongozi wa Taifa,na jiwe naye hawezi kuepukana nayo.

Kuendelea kumsema marehemu haitabadilisha chochote,ni busara ya kibinadamu kujadili wakati uliopo kwani huu TUNAWEZA kuubadilisha,Ila wakati uliopita ushapita hakuna cha kufanya,wakulungwa walisema yaliyopita sindwele Bali tugange yajayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…