Ni Tanzania pekee ambapo ujinga unatetewa na kundi kubwa la watu

Ni Tanzania pekee ambapo ujinga unatetewa na kundi kubwa la watu

Katika kipindi cha Mwaka mmoja na miezi michache nchi yetu inashuhudia utawala unaolinda Viongozi mafisadi, wafanyabiashara wakubwa na watumishi chawa na kutojali haki na heshima za raia wa hali ya chini kama kiini na chachu ya maendeleo kupitia makusanyo ya kodi na tozo za kinyonyaji.

Watanzania wote wasio viongozi,wafanyabiashara wakubwa watumishi wenye nyadhifa za juu serikalini wamekatwa mkia na kuwa hawana tofauti na wakimbizi nchini.

Mustakabali wote wa mipango, maendeleo na matumizi ya nchi yako kwa kikundi cha watu wachache "Oligarchs" ambao ni wanasiasa wa CCM na wafanyabiashara wakubwa tokana na fedha wanazokwapua toka kwa raia kupitia kodi na tozo za kinyonyaji pamoja na kuuza rasilimali za taifa.

Tunatumaini ipo siku yatakwisha haya ila hatuna hakika tutakuwa katika hali gani hio siku ambayo haya yatafikia tamati. Tumerudi nyuma kihatua kwa 99% toka ambako tulikuwa tunaelekea kimaendeleo na utunzaji wa rasilimali za taifa.

Zile zama za shamba la bibi zimerejea kwa kasi kubwa na sasa yote yanafanyika bila vazi la uwoga wala aibu mbele ya raia. Maisha yanapanda kwa kasi ya ajabu, tozo lukuki, kila kitu bei juu. Miradi haiendelezwi, ni udokozi unafanyika bila soni watu wanalambishana asali huku wananchi hawaelewi hatma yao ya kesho.

Mamlaka zimejipanga kunyonya raia kwa kisingizio kuwa ni kuleta maendeleo ambayo ni kiini macho. Maendeleo hayo hayo ambayo yanakopewa hela kwa matrillion ndio hayo hayo yanayokusanyiwa tozo. Msimamizi yupo ila hatuoni hatua za kiuongozi anazochukua.

Sina budi kusema tuliingia choo cha kike kwenda kinyume na ukuu wa Mungu kwa kujifanya tuna akili sana. Mama kazi yake halisi ni kuzaa, kulea na kusimamia nyumba sio majukumu mazito ambayo tumemtwisha. Kwa upande wa mafisadi na ma chawa kwao awamu hii ni bora kuliko iliopita ila raia wa hali ya chini ni msiba usio na wafariji.

Tusijizime data, hio kazi na uchawa unaoringa nao baada ya miaka 5-10 watoto wako hawatafaidika nao kwa lolote lile. System inazidi kuoza kwa comfort ya muda mfupi.
Sukuma gang kazini
 
Sasa Zitto kupata fursa ya kuwashauri kuhusu maziko yenu wapenzi wa jiwe ndiyo mumnunie?Siyo haki!Ameoata fursa kaitumia.Siyo fulusa wala furusadi!
sisi wafuasi wa jiwe tuna akili,sio watu wa kufuata kila ushauri maana wengine tunawajua.
 
Aliyesema ule msemo wa "Don't underestimate the power of stupid people in groups" nafikiri alikuwa na maana sana.
I can relate with the current regime chawaz
Jenga hoja mkuu, hoja hujibiwa na hoja si vihoja
 
Kama wenzangu walivyosema, mwenye enzi Mungu alituamulia ugomvi huu, je kuna haja ya kuendelea kutetea ujinga huo mwingi uliopita? Tumuombe Mungu atuvushe na atupe mapito na mwisho mwema. Asanteni
Tuwaondoe na wale wapuuzi wote kule bungeni, yaani tuvunje tuanze upya ila Kwa namna ilivyo pale kumejaa vilaza tupu wanaowaza uchaguzi Mkuu tu
 
kwa hiyo mnagoma kujizika kwa sababu bado hamjaonja asali?Tangu uhuru wa nchi mlikuwa wapi?Acheni ulafi,kufeni!😂😂😂😂
hilo la kuonja asali hatuna tatizo nalo,ila hili la kumsakama mwamba wetu,ndio litafanya hata hizo asali mzitapike hata kwa matundu ya nyuma.

mmeamua kula asali kuleni wacheni kelele mtapaliwa,inaua hiyo.
 
Tuwaondoe na wale wapuuzi wote kule bungeni, yaani tuvunje tuanze upya ila Kwa namna ilivyo pale kumejaa vilaza tupu wanaowaza uchaguzi Mkuu tu
inabidi muendelee kumuomba Mungu aue bunge zima,au hawezi kuua watu wengi😅😅😅
 
Toa hoja acha mihemuko, yule aliyekua anapora hela za watu kwenye mabenki? Aliekua anakopa pesa kwenye benki za biashara kimya kimya na kukudanganya miradi inaendeshwa kwa pesa zetu? Huyo aliyekua anatesa na kununua wapinzani au yule aliyekua anatumia pesa za serikali kukaa chato na delegation yake miezi sita?
Huyo huyo wala haujakosea! Huyo aliyepora pesa za mafisadi akajenga Tanzanite bridge ili watanzania ambao wengi ni masikini wapite! Huyohuyo aliyekopa kimya kimya bila kusumbua wananchi habari za tozo za kipuuzi! Huyohuyo aliyesweka ndani wapinzani uchwara waliosimama barabarani kuzuia grader lisitengeneze barabara watu wanufaike na maendeleo! Huyohuyo aliyezuia utoroshaji wa madini na kuongeza mapato ya ndani! Huyuhuyo aliyedhibiti uzembe na ufisadi serikalini!
Huyohuyo wala haujakosea!

Anaitwa Mwamba wa Afrika/Shujaa wa Karne !
 
Tuwaondoe na wale wapuuzi wote kule bungeni, yaani tuvunje tuanze upya ila Kwa namna ilivyo pale kumejaa vilaza tupu wanaowaza uchaguzi Mkuu tu
iko dhahiri sana, uwakilishi wa wananchi una dosari kubwa ni matokeo ya kukandamizwa kwa demokrasia, tuna wabunge waliochaguliwa na mkurugenzi wa tume ya uchaguzi, kazi yao ni kulia na kupiga sarakasi bungeni na hayo ma covid 19
 
Huyo huyo wala haujakosea! Huyo aliyepora pesa za mafisadi akajenga Tanzanite bridge ili watanzania ambao wengi ni masikini wapite! Huyohuyo aliyekopa kimya kimya bila kusumbua wananchi habari za tozo za kipuuzi! Huyohuyo aliyesweka ndani wapinzani uchwara waliosimama barabarani kuzuia grader lisitengeneze barabara watu wanufaike na maendeleo! Huyohuyo aliyezuia utoroshaji wa madini na kuongeza mapato ya ndani! Huyuhuyo aliyedhibiti uzembe na ufisadi serikalini!
Huyohuyo wala haujakosea!

Anaitwa Mwamba wa Afrika/Shujaa wa Karne !
Dhuluma haijawahi kuliweka taifa lolote salama pamoja na mdhulumaji, yuko wapi huyo mdhulumaji mkuu?
 
Back
Top Bottom