Kwa hiyo ukisomeshwa bure hutakiwi kuhoji chochote kile ambacho ni Cha hovyo kutoka serikalini?
AMENKuwa kiongozi Jamhuri ya wadaganyika hata kichaa inawezekana tu ,Leo hii wote waimba mapambio sijui wataficha wapi sura zao au na wao watacheza kulingana na mdundo unavyopigwa ?
Cha kutuokoa kama nchi ni katiba mpya tu vinginevyo tutakuwa tunaendelea hatua tatu mbele halafu tunakuja rudi nyuma hatua hamsin
Ndio maana umesema ni wewe , kaa ukifahamu kuna watu walihitaji chanjo pia kwanini wanyimwe haki hiyo na kushurutishwa kunywa michanyato.Kwani kuna ubaya upi kutumia vitu hivyo! mbona sisi huku mtaani nilivitumia na akuna Mtu aliyeguswa na coronavirus,na mpaka Sasahivi akuna aliyepigwa chanjo na tunadunda kama kawa.Sio kila kitu anachofanya mzungu kinafaa asilimia zote,ndio Maana kwenye fom zao za chanjo walijiondoa pamoja na serikali ili likitokea jambo wasilaumiwe.
Lissu again has proven them WrongRipoti za Mruma na Osoro juu ya Barrick/Acacia kulimbikiza deni hadi kufikia Trln 425 zilizua mjadala mkubwa ambapo aliyekuwa mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu alizikosoa na kuziita ni “Professorial Rubbish Report”.
Lissu alitoa ushauri wake kuwa kutokana na repoti hizo Barrick hawatalipa hilo deni na wakilazimishwa wakienda MIGA watashinda. Lissu alibezwa alipuuzwa na baada ya siku chache alimiminiwa risasi kuwa ni msaliti anayeshirikiana na mabeberu.
Barrick walitoa fedha za (Good faith) US$ 300M sawa na tsh 700b tu kati ya deni lote.
Jana Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba kwa niaba ya serikali amesema serikali imeisamehe Barrick/Acacia deni lote.
Uungwana ni vitendo mnyonge mnyongeni lakini haki zake apewe, Tundu Lissu aombwe radhi.
June 19, 2017
View attachment 2366316
Prof Muruma na Usoro walikuwa sahihi ispokuwa yale ni maslahi ya watu wa ccm na( strong people)Watasamehe vipi kitu wasicho dai kwa accacia?
Labda wasamehe tozo
Mkuu waombe Moderators waweke hiyo VIDEO hapo juu...lilikuwa swala la Muda tuu...pengo la Chadema huko Bungeni hata chekechea Analitambuwa....
MIGA naona wengi wetu wameshikilia kushtakiwa lakini wamesahau tulifikaje huku. Serikali yetu sikivu ilianza kutishia KUTAIFISHA mali za acacia na ndipo lissu akashauri mkienda kichwa kichwa mtapelekwa mahakamani. Kama nia yenu ni hiyo lazima kwanza mjitoe MIGA. JPM akaspin kuwa lissu anasema tukiwachukulia hatua acacia tutashitakiwa. Wengi wakamwamini JPM na kumuona lissu mtu wa ajabu. Serikali hawakutaifisha hivyo issue ya Miga ikawa mfu.Aliyesema tutashitakiwa Miga aombwe msamaha kwa lipi au atuombe radhi sisi kwa aliyotuhadaa kwa kutaka kututia uwoga
Na JPM angeliogopa tusingepata 700b yetu
Yeye Lissu atuombe msamaha sisi
Tundu alikinukisha sana. Sema rubish ilizingua sana
Mwigulu amethibisha jana kuwa serikali imenyosha mikono.MIGA naona wengi wetu wameshikilia kushtakiwa lakini wamesahau tulifikaje huku. Serikali yetu sikivu ilianza kutishia KUTAIFISHA mali za acacia na ndipo lissu akashauri mkienda kichwa kichwa mtapelekwa mahakamani. Kama nia yenu ni hiyo lazima kwanza mjitoe MIGA. JPM akaspin kuwa lissu anasema tukiwachukulia hatua acacia tutashitakiwa. Wengi wakamwamini JPM na kumuona lissu mtu wa ajabu. Serikali hawakutaifisha hivyo issue ya Miga ikawa mfu.
Lissu ni foreseerKila kitu kilifanywa kwa usiri mkubwa, halafu Magufuli akawa anawahadaa wetu kwa kuwaita viongozi wa dini , sijui makundi mbalimbali kwenye hizo hafla za utapeli wake. Cha kushangaza watu walikuwaje wajinga kiasi kile cha kuamini maigizo yale.
Halafu bunge lilikuwa halishirikishwi kabisa kwenye mambo yale, kisa Magufuli alikuwa hataki yajadiliwe bungeni maana wabunge wa upinzani wataweka wazi mambo hayo. Mambo haya ndio yalipelekea Magufuli anajisi chaguzi za nchi hii na kujaza wanaccm aliowataka yeye ili kusitokee yoyote wa kuhoji. Jambo hili ndio lilipelekea Lisu kupigwa risasi.
ForeseeKuna watu wanaon mbali haswaaaa
Kamwambie Mwigulu uone kama atakuelewa.....mzee wa ya ya ya!!Huyu msaliti akae hukohuko.
Lissu the winner againBora kitu kuliko kukosa kitu
Wangelipa hata asilimia 20% ya deni lote japo kwa awamu, kulipa tsh. 0.7tril kati ya tsh. 400+trilion ni dharau au walitulisha propaganda hawa inzi wa kijani. Pumbafu.Pia unaweza kukokotoa namna hii.
300 000 000 ÷ 191 000 000 000 =
(3 ÷ 1910 ) × 100 = 0.157 %
Barrick wamelipa 0.16% ya deni lote.
Makisio ya haraka ni sawa na mtu akuibie sh 1000 halafu wewe ukubali akulipe senti 16.