Ni wimbo gani unaoutafuta sana bila mafanikio?
Natafuta ule wimbo usemao.. "tumetoka kwetu mahenge.. Tumekuja darisalaam.."
Na ule wa olduvai band usemao ".. baba kaleta panya, we uchicheme panya chema chamaki nchangaa..."
Na ule wa inafrica band uitwao indege
 
Wadau mwenye nyimbo za mwinjuma muumini kwenye ile albam ya tunda maisha kitendawili weka ata albam nzima af ni pm nikupe posho kidogo
Kweli?? Nitumie namba yako nikutumie kwa whatsapp saivi afu ww utaziweka huku, mi mshamba kidogo sijui kuweka jf
 
Mm nataka ule wimbo unaoanza kwenye kipindi cha shilawadu, nilipenda ile michano..
 
Mkuu,,
Kama umechota uhitaji wangu..

Huu wimbo nautafuta sana lakini siupati..

Elimu ya mjinga ni majungu-R.I.P banza stone..TOT PLUS.

"Bora ukose Mali upate akili".
[emoji1] ngoja nifahamu namna ya ku-upload nitauweka hapa na kukutag pia.
 
Wimbo flani hivi mashairi yake yanasomeka - [emoji444]" baada ya kumaliza masomo nilipata kazi, wazazi wangu walinihusia jinsi ya kuishi na walimwengu"......-Halaf kibwagizo- " nawashukuru wazazi wangu wakati wote, ushauri wao uliniletea mafanikio mema sasa naishi na watu vizuri oooooh jamaa"

Wapi ntaupata bandugu?
Ninao kwenye laptop kuuweka ndio tatizo.
Juwwata kipindi hicho.
 
Kuna ka nyimbo alishirikishwa Juma Nature kiitikio chake kinaimba ' kila nitakalolifanya mie kwao baya/ watu wana, hawana wanalolifanya ni roho zao mbaya / watu bwana "

Nikiupata nitashukuru
 
Back
Top Bottom