Ni wimbo gani unaoutafuta sana bila mafanikio?
Mimi natafuta nyimbo mbili lakini sijui zinaitwaje na wala kaimba Nani.mmoja una kipengele kinaimbwa_ Mjini umekuja juzijuzi kwenu ulikuwa unafuga mbuzi.sikujua kuwa ni nuksi mpenzi umemkuwadia mdosi._mwingine kuna kipengele kiko hivi= Hoi hoi hoi mimi naliaa Hoi hoi hoi parapanda italia. Yaani nazitafuta sana
Nyimbo inaitwa rafiki - Sumalee
 
Kuna wimbo unaimbwa- Mama mdogo alinichukua kijijini,alimuahidi mambo mengi Dada yake,kwamba atanisomesha- chorus- kama una pesa oya oya nitumie nauli nirudi Nyumbani,mwenye nao jamani
 
Wakuu Mimi natafuta sana wimbo wa KIPEPEO WA BIMA LEE ORCHESTRA. Wimbo uliimbwa na Max Bushoke. Miaka ileeeeee.Atakenipatia Wimbo huo nitampatia pesa ya MB kadhaa.
 
Sidhani kama unaitwa asu ila kwenye hiyo album ambayo wimbo ASU upo ndipo ulipo huo wimbo nadhani unaittwa reila kama sikosei
Wimbo unaitwa mimi nawe, kama sikosei ndani wanaimba " ewe lela ewe rose mimi nawe mpaka milele"
Misambano + Leila
 
Kuna wimbo unaimbwa penzi la ndoa ni tamu Caz t kashirikishwa- mwenyenao tafadhari.mwingine unaimbwa-ukiona panafuka moshi ujue pana moto
 
'Kifo hicho hakikimbiliki' cjui ni kwaya gani imeimba ni kawimbo kana hisia hivi, cjui ni ya songea!?
Kifo hicho Kifo hicho hakikimbilikiiihiiii, imekuwa vita Marehemu angekimbia,x2, huu ombo huumba sana REDIO maria, uliimbwa Songea na Halimataya maarufu wa 1990s mama JOHN wa Lizaboni rip. Nahisi mdingi anayo pale home. Shida Ni kuihamishia toka kwenye tape.
 
Kuna ule wimbo wa Jamboo..enzi zile tukiuskia tunajua ni time ya kuamka kwenda shule...ulikua unatukata stim kinyamaaaa
 
'Naomba unipende kama nilivyo mi msela' sikumbuki umeimbwa na nani

Dah uliimbwa na cheleaman kutoka Iringa. 2006 Nilikuwa pale nikiwa simu nokia 2100 Nilienjoy kuusikia ukirudiwa mars kwa mara. Ninayo ngoja nifanye mpango. Dah inagoma
 
Back
Top Bottom