Ni wimbo gani unaoutafuta sana bila mafanikio?
Wadau kwema humu?
Naomba mwenye nyimbo hizi zilizoimbwa na Banana Zorro.
1. Niamini
2. Nieleze
Halafu kuna wimbo wa Mike Tee a.k.a Mnyalu kamshirikisha Banana Zorro unaitwa Mtumishi wako.
Natanguliza shukran zangu. Mwenye nazo hizo au mmoja wapo akiuweka hapa ani tag au ani quote.
 
Mimi siku nyingi sana natafuta nyimbo zifuataz:

1. Wimbo wa Salim Ahmed Salim, ulipigwa miaka ya mwanzoni ya 90, wakati mheshimiwa huyu akiwa Katibu Mkuu wa OAU, una maneno mazuri sana ya kumpongeza. Ulipigwa na kundi la Zaita Muzika, la akina Supreme Ndalakasheba. Una maneno baadhi yake yanasema "Aee aee Afrika aee, OAU itashinda, Salim Ahmed Salim, dua zetu zikufikie aee...."


2. Natafuta pia nyimbo za kwaya ya Iringa, album yao ilikuwa inajulikana kama KUNDI LA NZIGE


Nitafurahi sana kama kuna mtu ata-acknowledge kwa kunipatia nyimbo hizi
Huu wa Salim Ahmed Salim nimeuona huu hapa; usikilize ni mzuri mno

 
Original tracks za chidumule album yesu ni bwana especially original form ya nyimbo hizi
Libarikiwe neno hili
Ya nini mizigo hiyo
Please mwenye access nazo
 
Back
Top Bottom