Mkuu nenda direct jozi, halafu nakazia kuna mdau kasema kaa mbali na wabongo maana wabongo waliowengi michongo yao ni wizi na kuuza dawa japo wapo wachache ambao wana utimilifu na wako na biashara halali, kwa sababu umeshajiandaa kufanya kazi zote ni safi cha kukaa nacho mbali ni kuiba na kununua vitu vya wizi, na kuuza madawa na magendo, jaribu marafiki zako wawe Warundi kwanza kwa kuanzia, wacongo sii mbaya, wapopo hawa ongea nao kimachale sana japo ndio jamii ya kutoka nje ya SA waliofanikiwa halali na kwa haramu, jibane sana foreigner usile madem au wake za watu ukajulikana utaundiwa zengwe kali na usimuamini sana dem wa kizuru, kikubwa jipange kabisa namna utakavyosurvive siku za mwanzo ukiwa jozi, akilini weka wewe ndio master wa safari yako, wasikutishe vifo hata bongo vipo kila siku na hata ukibaki bongo hutaishi milele so fukuzana na ndoto zako hadi utakapoishia maaana wapambanaji hua hawarudi nyuma ni kusonga mbele mwendo wa vitani haijalishi utakutana na magumu mangapi.