Hii ni Tz nzima, nina sista wangu anafundisha shule ya sekondari huko Singida anasema watoto huko ni amsha popo kila siku kesi tu mara huyu kakutwa na yule huyu sijui kafumaniwa wapi huko huyu mara ana mimba mpk hivi juzi kati kuna mtoto wa form 2 aliwatamkia kabisa walimu wake kwamba yeye huo mchezo kaanz tokea la saba na mpk sasa hawezi tena kukaa bila kuufanya, tena hawa watoto ni waongo balaaa kama hujui kuwahoji kwa technic watakupiga chenga ya mwili mzima mana sista anakwambia jinsi wanvyowahoji mpk waje kukubali hizo kesi zao inabidi tu usiwe na kichwa chepesi ndio utawaweza lasivyo utadanganyika tu na utaona kama kweli wanasingiziwa. Au kama vip ww jaribu kwenda shule yoyote Tz hii yenye wasichana ukaongee na mwalimu wa nidhamu ili akuhadithie mabalaa ya wanafunzi kama hujajishika kichwa basi utakua na robo ngumu. Mkuu hii dunia siku hzi imevaa kaptula
Sent from my SM-G900I using
JamiiForums mobile app