Nilijikuta naishi maisha ambayo sikuyategemea ila sina jinsi

Nilijikuta naishi maisha ambayo sikuyategemea ila sina jinsi

Kwenye kumsikiliza siafikiani na nyie aisee.
Jamaa hamtakii mema huyu mwanamke. Ni kawaida ya watu wengi kupenda kuona ex wake akifeli, kwake jamaa ni furaha.

Kuruhusu ukaribu nae ni kujitafutia majanga tu, na pia huenda bibie asiweze kumchomolea mwamba wakarudiana, wakarudia historia ileile au mbaya zaidi ya mwanzo.

Kama kuna mwanga akomae tu, jamaa hana utu kabisa. Anamtafuta ammalize coz nadhani bado anaumia kuhisi kua
Hapa kuna vitu viwili: Msamaha na Ndoa.

Msamaha hauna maana kwamba nakubali, bali kutoa nafasi ya kujifunza na kuendelea. Na hii si kwa anae samehe au anae samehewa, ila wote.

Kwa maneno mengine, anae kataa kusamehe na anae kataa msamaha, wote wanafanya kosa na hivyo wanaharibu hali yao ya ndani. Kwa hiyo wana haribu uhusiano; uhusiano kwanza na Mungu na pili na jamii.

Kuhusu ndoa. Kwa uelewa wangu, ndoa ni jambo la akili, ambapo ikishafungwa haiwezi kufunguliwa kwa sababu yoyote; labda kama hakukuwapo na ndoa.

Kwa hiyo, kama hawa ndugu walikuwa kweli wana ndoa, itabaki hivyo daima kwenye akili na hilo haliwezi kubatirishwa.

Kitu ambacho tunatakiwa kujua ni kuwa, mambo yote mema au maovu, mazuri au mabaya yanayoweza kutupata kwenye ndoa, tunapaswa kuyapokea na kuyavumilia kwa unyenyekevu.
 
Nimetangulia kusema kuwa nimeandika kipande kidogo sana cha mkasa wangu kuna mengi makubwa ambayo sijasema na sijasema kwa sababu maalum, ungejua mkasa mzima natumai usingesema habari za kumsamehe,

Nilishamsamehe wala simhukumu, na yeye hana nia ya kutoa support mpaka akutane na mimi labda kwa kuwa sikueleza bayana kukutana kwake ni kwa namna gani si kuonana tu bali tukutane tukiwa wawili nadhani umeelewa maana yake. Kitu ambacho siwezi ruhusu hata siku moja kitokee.
pole sana, kama hajakuletea mambukizi ya VVU shukuru MUNGU
 
Pole.
Kwa hiyo tukuchangie upate Vyumba viwili?
Sasa sisi tutakuwa na uhakika gani kama wewe ni KE kweli?

Au ni mtu unatafuta tu namna yakuishi?
Hukuna mahali amesema tumchangie, ndugu pole Sana na mitihani ya maisha. YATAPITA
 
Baba Yao kasema yupo tayari kulea watoto wake na kuwahudumia so Cha muhimu watu mlio Katika ndoa wake kwa waume tulize de libolo kwa mke mmoja mlee watoto wenu na sio kila siku mnawaza uzinzi tu mwisho mnawatesa watoto kisa ndoa zenu fake
Ndio maana Kila siku nasema, Tuanzisheni Kapu la JF , ambalo Ndani yake tutadumbukiza Mia mia tu .

Kwa ajili ya watu kama hawa, Mtoa Mada ni Mama mpambanaji sana ,mwenye uchungu na wanawe .



Niwaombe sana WanaJF wanaume Kwa Wanawake wenye Fursa nyingine za Kazi, mmfikirie , mtoa Mada alipata kazi, Kwa Uwezo mkubwa wa akili na uthubutu Alonao, Hatokaa kuomba Kodi.
 
Pole.
Kwa hiyo tukuchangie upate Vyumba viwili?
Sasa sisi tutakuwa na uhakika gani kama wewe ni KE kweli?

Au ni mtu unatafuta tu namna yakuishi?
Hukuna mahali amesema tumchangie, ndugu pole Sana na mitihani ya maisha. YATAPITA
Wanawake ni wanafiki sana na mnapenda kutafuta huruma wakati nyie ndo mnaanzaga kuvuruga nyumba hadi mwanaume anaamua kutokomea kusikojulikana
Kama wanawake wanavuruga mbona unaenda Tena Kwa mwanamke mwingine.Kwanini usikae pekeako?
 
Kama mzazi mwenzio kaonyesha nia ya kiwasaidia watoto wake kwanini unamzuia? Huoni kama unawanyima haki yao ya msingi
Kuwasaidia watoto ni mpaka akutane na mimi faragha? Mwenye nia ya kuwasaidia watoto angewasaidia tu, ndio maana nikikataa analeta maneno kama nilyosema kuwa nina jeuri, kiburi, nitakuwa na mwanaume ambaye ananipa kiburi, na kusema hatawasaidia kwa kuwa nakataa.

Nadhani hamjaelewa, lengo la msaada wake ni mpaka akumbushie na mimi maana yake apashe kiporo, nimeandika bila kufunguka nikajua mnaweza kuelewa.

Mimi na yeye tulishamaliza safari, siwezi kuruhusu hicho kitu kitokee abadani asilani eti ili watoto wapate matunzo.
 
Siwezi kuhukumu moja kwa moja ila kwa hii tabia ya kubeba vyombo waswahili mnazo sana na ni tabia ya dhiki sana
Mwanaume gani wa kubeba vyombo na vitu wanavyotumia wanao?

Mwanaume akapambane na maisha yake ila watoto wana haki na baba mda wote
Hata kama yametokea maudhi na hata mwanamke akaropoka kwa hasira na kusema tu ' kwanza watoto sio wako' kuna DNA na pia unaangalia maneno yametoka kwa sababu zipi

Nakupa pole pia pambana tu na maisha yako na yeye ni lazima ukubali yaishe ili awasaidie watoto wake kwa hali na mali

Kweli kakosea kuondoka hivyo ila ameomba akusaidie na wewe umekataa ni kosa

Watoto pia watasikia mengi na hata kujifunza mengi kutoka kwako na usirogwe ukawa na mchepuko nao wakajua maana ndio yatakuwa majibu ya familia zote na wao watakuchukia sana

Uamuzi ni wako na wewe unajua vizuri kesi yenu
 
Mimi sina tatizo na yeye, nilisha yaacha yapite ndio maana sijihangaishi hata kutaka chochote kutoka kwake wala kujua anakoishi. Na kuhusu watoto wake wala sijawaambia ubaya wowote na wala hawaulizi chochote. Ila mimi kumsikiliza kwa namna ya kuyajenga haitakaa itokee chini ya jua hili hata kwa bahati mbaya.
Pole sana dada upo mkoa gani? Naomba location yako hata pm kama hapa itakuwa ngumu. Kesi kama yako nimewahi ishuhudia kwa ndugu wa karibu kabisa, baba kamkataa mwanae na mkewe, mke kapambana kasomesha mpaka mtoto kapata kazi ndio baba anajitokeza kuomba msamaha ya kuwa ni ujana ulimsumbua. Kukwepa majukumu ni mbaya sana.

Huu ni wakati sahihi wa wana jf kuunlock ID's kusaidia wale ambao itathibitika ni wahitaji wakubwa.
NB: KAMA ITATHIBITIKA.
Acha mama tuitwe mama jamani[emoji24][emoji24]
Mmshike mkono mwenzenu ikiwezekana.
 
Niliachana na aliyekuwa mume wangu miaka 5 imepita, kuachana kwetu kulikuwa kubaya sana kwa mambo mabaya yaliyopita katikati yetu. Sipendi kuyaeleza maana ni mabaya ila nilishayasahau na kuyaacha yapite.

Baada ya kuachana (aliondoka bila kuniaga na kodi ikiwa tunadaiwa miezi 5 bila kulipa) nilibaki na watoto huku nikiwa sina pa kuishi kwani mwezi 1 baadaye mwenye nyumba alinitaka kumuachia vyumba vyake, sina kazi, sina hata kitu kimoja kwa kuwa aliondoka na kila kitu hadi nguo zangu na za watoto na kwenda kusikojulikana alihama nikiwa sipo.

Kabla ya yeye kuondoka nilikuwa sijui kama tunadaiwa kodi, kwa kuwa kodi ya mwanzo ilipoisha alinambia kuwa kodi imeisha na yeye hana pesa kwa kuwa kazini kwake wamepata hasara analipwa nusu ya mshahara ambao ndio tunatumia kujikimu nyumbani.

Tukashauriana nikope pesa kwa ndugu yangu ambaye amekuwa akitusaidia kutukopesha pale tunapokwama na tunamlipa kidogokidogo, nikamtafuta na akatukopesha, nikamkabidhi 1,200,000 ambayo ndio ilikuwa kodi ya miezi 6 nikajua kalipa kumbe kampa mwenye nyumba kodi ya mwezi 1 tu na nyingine sijui alikopeleka hadi leo.

Sasa alipoondoka ndio mwenye nyumba kunitafuta kuwa nadaiwa miezi 5 hadi siku ile na nimeshaanza mwezi wa 6 ivyo ananipa wiki 1 nimuachie nyumba yake, kumbuka hapo nalala chini mimi na watoto kwa kuwa kila kitu kilishaondoka na yeye. Na nafanya kazi ndogondogo kupata chakula cha watoto.

Nikawaza kurudi nyumbani, Kilichonishangaza ni kuona ndugu zangu wote hawapokei simu zangu na wakipokea wananilaumu tu kuwa nimeyatafuta mwenyewe na nisiwasumbue na wanakata simu. Nikawaza nimeyataka yapi? Nimekosea nini? Mbona changamoto zangu pande zote wanazijua kulikoni nalaumiwa leo, nikajaribu upande wa aliyekuwa mume wangu ndio balaa zito.

Mtu 1 akaniambia unajua kuwa Unatuhumiwa kuzaa nje ya ndoa? Nikahamaki, akaendelea kusema baba fulani amewaambia ndugu zako na zake kuwa mtoto huyo mdogo sio wa kwake na ndio maana kaondoka. Nikamwambia hapana haiwezi kuwa kweli kwa kuwa sijawahi kutoka nje ya ndoa hata siku moja. Na kama kasema hayo basi ana lake jambo huenda kaamua kuficha mambo yake kwa kunitwisha mzigo maana tayari alikuwa hana pa kukwepea kutokana na mambo yake.

Basi nikatuma ujumbe mfupi kwa ndugu zangu kuwa, nashukuru kwa kuwa nimejua sababu ya nyie kunichukia ila nawaambia siyo kweli na sijawahi kufanya uchafu huo ila nipo tayari wakapime DNA nchi yoyote na ikibainika ni kweli basi wanihukumu nikazima simu ili nipate muda wa kuwa peke yangu kuwaza nini cha kufanya, nikaanza kuwaza cha kufanya nalia peke yangu.

Nikaanza safari ya kutafuta chumba japo sijui nalipa nini, nikapata mama mmoja nikamweleza hali yangu akanambia nakupa chumba ila utakuwa unanilipa mwezi mmoja mmoja sh. 60000 na mwezi huu nakupa ukae bure utaanza kunilipa mwezi ujao, nikaona chumba ni gharama ila kwangu ilikuwa ahueni maana nina mwezi mmoja wa kuanza maisha kutafuta kodi ya watu.

Nikahamia hapo, na wanangu tukaanza maisha, mwezi mmoja baadae nikapata kazi japo haina mshahara mzuri ila inaniwezesha kupata chakula na kulipa kodi ya 60000 kila mwezi, nikaanza kujibana na kununua vyombo, godoro, kitanda, nguo za watoto nk.

Miezi 7 baadaye nikaja kujua alikokwenda yule mwanaume, na kwamba alipohama alihama na mwanamke mmoja ambaye alikuwa mchepuko wake wa siku nyingi wakaanza maisha yao, nilikutana na ndugu wa huyo mwanamke ndiye aliyenipa taarifa hizo.

Baada ya miaka 2, mwanaume huyo alinipigia simu, akidai anataka kuniona kanikumbuka, nikamwambia huwezi kuniona na wala hutakaa ujue naishi wapi, kwa kuwa sikutaka hata waliokuwa wanatufahamu wajue naishi wapi pia, baada ya kumjibu ivyo akasema kwa kuwa hutaki nikuone basi nilichotaka kusema sitasema, japo nilikuwa na lengo la kuonana na wewe ili nianze kukupa hela ya matumizi ya watoto kwa kuwa umekataa na mimi sihudumii hao watoto, nikamwambia kama wameishi miaka 2 bila huduma yako, basi wataishi tu.

Akawa anaendelea kunitafuta kwa namba mbalimbali huku akifoka na kuniita nina kiburi, jeuri, sina adabu kwake, nitakuwa nimepata mwanaume ananipa kiburi nk, mara aseme nitakuwa nimewalisha watoto sumu kuwa yeye mbaya ila yeye sio mbaya anataka kuwatunza ila mimi ndio nazuia. Mwisho alikata tamaa na sasa imepita miaka 5 nikiwa naishi na wanangu.

Inaniuma sana kuishi na wanangu wakubwa sasa ndani ya chumba 1 kikiwa ndio chumba na ndio sebule kwa kuwa sina uwezo wa kulipia zaidi ya chumba 1 ukizingatia ni wa kiume ila sina jinsi najipa moyo kuna siku nitapata nafasi ya kupata walau vyumba 2 wanangu wakalala tofauti na mimi mama yao.

Nimejitahidi kuandika matukio machache kwa kuyakata sana ili nisiwacoshe
Inafika sehemu unakatana na kitu mpaka unajiuliza mara mbili mbili,ila haya yote ni maisha,kutoka kwenye Imani ya dini ni kwamba Mwenyezi ndio mpangaji
Nataka kusema wewe ni Mwanamke wa Shoka

Sent from my V2204 using JamiiForums mobile app
 
Cha muhimu watu mlio Katika ndoa wake kwa waume tulize de libolo kwa mke mmoja mlee watoto wenu na sio kila siku mnawaza uzinzi tu mwisho mnawatesa watoto kisa ndoa zenu fake
Kwa Mimi nikiwa km Jaji Mfawidhi wa JF ingawa wanasema ili uamue kesi pasina kuacha shaka yoyote yakupasa usikilize pande zote mbili, kwa kutumia principle ya 'judge as Caesar's wife' naona kwa mujibu wa mleta mada, mwenye tatizo ni yeye mwenyewe na sio mwanaume wake kwa sababu moja kuu na yenyewe sio nyingine bali ni kutokua muwazi na anatumia vificho hasemi ukweli maana kuna madudu aliyofanya nyuma ya pazia anayajua yeye mwenyewe na hawezi kuyaweka open hapa na kuthibitisha hilo moja ya madudu ni kumzuia mwanaume kuhudumia watoto wake hilo ni kosa haijalishi amekukosea kiasi gani Ila km watoto ni wake wana haki ya kupata huduma kutoka kwa baba yao, ugomvi wenu ni wenu sio wa watoto mtoa mada tuliza Wenge pokea matunzo ya watoto yakikushinda utaanza kulia kwenye vyombo vya habari kumbe wewe ndio mwenye kiburi, majivuno na kujiona unaeleza amekutafuta sana Ila umekua ukimkwepa hadi ameamua kukata tamaa kwa hio wewe ndio unaewatesa watoto sio mwanaume wako, unasema unalala na watoto wa kiume chumba kimoja uenda ya kua mwanaume wako ameliona hilo na anahitaji kukusaidia Ila ukamletea kiburi, jeuri na kujiona kua peke yako unaweza na hauhitaji msaada wake

Conclusion: jitafakari wewe mzazi km ulizaa nae kweli hao watoto angalieni namna ya kuwatunza hata akiwataka awatunze yeye ili usiishi nao chumba kimoja angalia jinsi ya kusolve hilo tatizo, sio kuongeza tatizo kwa chuki na Mambo yaliyopita

Nb: najua hujaja kuomba msaada
 
Baba Yao kasema yupo tayari kulea watoto wake na kuwahudumia so Cha muhimu watu mlio Katika ndoa wake kwa waume tulize de libolo kwa mke mmoja mlee watoto wenu na sio kila siku mnawaza uzinzi tu mwisho mnawatesa watoto kisa ndoa zenu fake
Baba yao kama walivyo wababa wengine wapuuzi, alikua anatafuta njia ya kujirudi Kwa mwanamke aendelee kupasha viporo.


Lkn pia inawezekana mpaka akataka kujirudi nisababu alipokuja mambo yalibadilika.


Ni chaguzi sahihi sana ALOFANYA mtoa Mada hata kama ana shida ya Uchumi.



Kuhusu wababa kutulia kwenye Ndoa zao, hapa suala ni Akili ya Mwanaume mwenyewe , Kuna hao wanachepuka na kusahau familia, alafu Kuna Mimi, nachepuka lkn Huniambii kitu Kwa Wife na wanangu na wanangu wengine.
 
Pole sana dada upo mkoa gani? Naomba location yako hata pm kama hapa itakuwa ngumu. Kesi kama yako nimewahi ishuhudia kwa ndugu wa karibu kabisa, baba kamkataa mwanae na mkewe, mke kapambana kasomesha mpaka mtoto kapata kazi ndio baba anajitokeza kuomba msamaha ya kuwa ni ujana ulimsumbua. Kukwepa majukumu ni mbaya sana.

Huu ni wakati sahihi wa wana jf kuunlock ID's kusaidia wale ambao itathibitika ni wahitaji wakubwa.
NB: KAMA ITATHIBITIKA.

Mmshike mkono mwenzenu ikiwezekana.
Nimeshatoa mkono wa pole.
 
Mmmmmmhmn ila aisee kuna watu wana laana aisee. Sasa unamuacha mtoto wa watu na mizigo namna hii alafu yeye yupo huko somewhere na mipumbu yake anajiita mwanaume.

Huyu ilitakiwa akamatwe na polisi kabisa awekwe ndani na alipishwe pesa ndefu isiyopungua milioni 5. Halafu apewe masharti ya kulipa kodi, kutoa matumizi ya watoto na mke.

Jamaa mpumbavu sana huyo aisee.
 
m
Kwa Mimi nikiwa km Jaji Mfawidhi wa JF ingawa wanasema ili uamue kesi pasina kuacha shaka yoyote yakupasa usikilize pande zote mbili, kwa kutumia principle ya 'judge as Caesar's wife' naona kwa mujibu wa mleta mada, mwenye tatizo ni yeye mwenyewe na sio mwanaume wake kwa sababu moja kuu na yenyewe sio nyingine bali ni kutokua muwazi na anatumia vificho hasemi ukweli maana kuna madudu aliyofanya nyuma ya pazia anayajua yeye mwenyewe na hawezi kuyaweka open hapa na kuthibitisha hilo moja ya madudu ni kumzuia mwanaume kuhudumia watoto wake hilo ni kosa haijalishi amekukosea kiasi gani Ila km watoto ni wake wana haki ya kupata huduma kutoka kwa baba yao, ugomvi wenu ni wenu sio wa watoto mtoa mada tuliza Wenge pokea matunzo ya watoto yakikushinda utaanza kulia kwenye vyombo vya habari kumbe wewe ndio mwenye kiburi, majivuno na kujiona unaeleza amekutafuta sana Ila umekua ukimkwepa hadi ameamua kukata tamaa kwa hio wewe ndio unaewatesa watoto sio mwanaume wako, unasema unalala na watoto wa kiume chumba kimoja uenda ya kua mwanaume wako ameliona hilo na anahitaji kukusaidia Ila ukamletea kiburi, jeuri na kujiona kua peke yako unaweza na hauhitaji msaada wake

Conclusion: jitafakari wewe mzazi km ulizaa nae kweli hao watoto angalieni namna ya kuwatunza hata akiwataka awatunze yeye ili usiishi nao chumba kimoja angalia jinsi ya kusolve hilo tatizo, sio kuongeza tatizo kwa chuki na Mambo yaliyopita

Nb: najua hujaja kuomba msaada
Mtoa Mada ni Moja ya Wanawake wakweli na wawazi wa kiwango Cha juuu sana, Naam nandio sababu aliamua kusimamia maamuzi yake yakutorudiana na Jamaa Kwa sababu mtoa Mada anajijua ni mtu safi .


Wanhekua ni wale Wanawake wma waruwaru kiguuu na njiaaa, Siku jamaa alomtafuta, kwake angeona ni ahueni ya juuuu sana kwaivo asingzungusha.


Sheria ya mtenda maovu Huwa Iko hivi " Huwa yeye ni mwepesi wa kufurahia Msamaha unaompa as long as anajijua alikosea".
 
m

Mtoa Mada ni Moja ya Wanawake wakweli na wawazi wa kiwango Cha juuu sana, Naam nandio sababu aliamua kusimamia maamuzi yake yakutorudiana na Jamaa Kwa sababu mtoa Mada anajijua ni mtu safi .


Wanhekua ni wale Wanawake wma waruwaru kiguuu na njiaaa, Siku jamaa alomtafuta, kwake angeona ni ahueni ya juuuu sana kwaivo asingzungusha.


Sheria ya mtenda maovu Huwa Iko hivi " Huwa yeye ni mwepesi wa kufurahia Msamaha unaompa as long as anajijua alikosea".
Hapana angekua ni mkweli asingeficha kisa Cha kukimbiwa na mwanaume wake, uongo uanzia hapo maana anaficha source ya tatizo lake
 
Mimi namlaumu mwanaume mwezangu kwakumwacha mke na watoto kama shida ni mwanamke angesaidia watoto.Yasije yakawa ya diamond na Omy Dimpoz.wtoto wemefanikiwa ndo baba unajitokeza. Hata huyo unaesema sio wako akikua bado atakutambua kama babaeke. Mimi naamini kwenye hizo familia zetu ,tunatunza watoto ambao kibaolojia sio wetu, lakini kwakuwa kapatikana katika familia yako huyo ni wako labda mkeo aseme sio wako. HEBU CHUKUA MUDA KUJIULIZA HIVI MTOTO HUWA ANAMCHAGUA BABA AU ANAMCHAGUA AKAZALIWE WAPI NA WAZAZI GANI. Mama pekee ndio mwenye uwezo wakuamua nizae na nani na MTOTO awe wa nani.Baba wewe kazi yako ni kulea.
 
Back
Top Bottom