Nilikuwa mfuasi wa Trump Kwa Muda Mrefu sana Ila Kwa Hili la Kusitisha Misaada na Ruzuku upande wa Afya Sikubaliani nalo, amekosea sana

Nilikuwa mfuasi wa Trump Kwa Muda Mrefu sana Ila Kwa Hili la Kusitisha Misaada na Ruzuku upande wa Afya Sikubaliani nalo, amekosea sana

Tuna Mikataba Nao ya Ruzuku na Ndo maana Tunalalamika kama Tusingekuwa na Mikataba nao tusingelalamika
Hamna mkataba wa ruzuku duniani baina ya taifa moja na lingine.
Kuna mkopo tu tena wenye benefits pande zote

Msaada si lazima , tatizo lenu mnakata kufanya ni jukumu. Trump yupo pale kwa mafuaa ya wa america si ya mtanzania
 
Disease burden ya wakorea kusini, wajapan, Russia, Norway na hata hao wamarekani ni nani Huwa anawabebea?
Mmarekani, Korea ,Japan russia ndo wamiliki Wa Big Pharm wao ndo hutengeneza madawa..
Unahisi wanahitaji Msaada wa Madawa na Chanjo??
 
Watajua tu thamani ya kidoge kimoja, si vilikuwa bure wakaona mambo ni rahisi!
Subiri muda si mrefu zitakuja nyuzi za malalamiko humu watu kutomudu huduma za matibabu na dawa
Sasa hapo wataanza Kulalamilia Hospitali..
Mfano ukaenda Muhimbili ukaambiwa Matibabu yako ni Tsh Laki tano na Umepimwa tu na Ukapewa Dawa za malaria na Antibiotic
 
Yeye anafanya hivyo kwa ajili ya maslahi ya nchi yake wewe unapaswa kupeleka lawama zako kwa serikali yako ambayo kwa miaka 60+ ya uhuru bado ni omba omba licha ya kua na rasilimali za kila namna
 
Nchi za Afrika Zote haziwezi kutoboa kwa Disease Burden Iliyopo Ngoja Twende statistically..

  • Riport ya mwaka jana Tanzania Kwa sasa Ina WAVIU- 1.7Milion na waviu wanaotumia ARV ni 1.4 Milion
  • Waliokuwa wana Ugonjwa wa Malaria walikuwa ni zaidi ya Milion 1
  • Watoto waliopatiwa Chanjo ni zaidi ya Milion 1
  • Watu waliotumia Njia za Uzazi wa Mpango ni zaidi ya Milions
  • Wagonjwa wa TB kwa mwaka Jana walikuwa zaidi ya Laki mbili
Hakuna Nchi narudia tena Hakuna nchi wala Chama Kinachoweza Kubeba Hiyo burden Bila Kuhitaji Msaada..
unajua Chanjo moja ni Bei gani? Unajua ARV Drugs Ni Tsh ngapi Kopo Moja? Unajua Uzazi wa Mpango Hata Kidonge tu Circle mpja Ni Tsh ngapi??
Niliwahi kusikia kile kikopo cha dawa za kufubaza VVU cha kutumia mwezi mmoja gharama yake ni zaidi ya USD 500.

Pana kutoboa kweli hapa?
 
Siku ya Januari 20, 2025, Rais wa Marekani Donald Trump alisaini agizo la rais (executive order) lililosimamisha kwa muda wa siku 90 utoaji wa misaada nje ya Nchi, ikiwemo programu muhimu za afya kama Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na UKIMWI. "President's Emergency Plan for AIDS Relief " (PEPFAR).

Kusitisha Huku Progran Hizo kutaathiti Dawa za Virusi vya UKIMWI (ARV), Dawa za kifua kikuu (TB), na Dawa za malaria na Dawa za Uzazi wa Mpango..

Ukiachana na Kuathiri Upatikanaji wa Dawa Taarifa ya USAID kuhusu Kupunguza kusitisha Misaada ya Viti hivyo Kumeanza Kuleta Effect kwa Baadhi ya NGOs Mashirika Mengi..

Yanayohusika na Utoaji wa Dawa za ARV,Kifua kukuu na Ukoma,Uzazi wa Mpango,na malaria yameanza Kuyumba na wote wameanza Kutoa Notice kwa wafanyakazi wao kusubiri na Kuangalia kama Marekani itarudisha Panga kwenye ala bhasi watarudi kazini...

Takribani Wafanyakazi wa Mashirika Tanzania 2900s Wanaenda Kupoteza Kazi kutokana Na upuuzi na Ego ya Trump..

Poleni Afya, Poleni Wafanyakazj wenzangu na Mostly Poleni wagonjwa ambao mnaenda Kuathiriki kwa Order hii Isiyo na Mashiko..
_____________________________________

Waafrika Tujitegemee:
Uhuru kenyata

View: https://youtu.be/wYpSNxTxXE0

Kwani wewe ni mlipa kodi wa USA?
 
Siku 90 Ni nyingi sana Kama Hatuna Stock ya Kutosha..
Nakubaliana na Wewe kabisa..Hii iwe Wake up Call kwetu..

Ila Kwa akili ya Trump vipi kama Hatorudisha maana Kabla ya POTUS alivunja Mkataba wa WHO
Tanzania tunatakiwa kufanya reform kwenye mambo mengi sana mkuu huu ndio ukweli mchungu ambao viongozi wetu hawataki kuusikia.
Kuna mambo hayataki siasa ila sisi tunaingiza siasa maswala ya Afya, ulinzi, elimu ni sekta za muhimu sana zinazohitaji big brain tu kuziendesha.
Leo trump katufinya kidogo tumeshaanza kupoteana vipi akiamua ku -drill more deep lazima twende kupiga magoti.
Rejea kauli ya mkuu wa mkoa wa jiji pendwa majuzi hapa kuhusu mama mjamzito inatoa picha how Tanzania is...
BTW Ubalozi wa marekani ulikemea mauaji ya mzee wetu aliyetekwa mchana kwenye bus tukawaambia wasitupangie vivyohivyo na sisi tusiwapangie .
TRUMP anatoa somo la uongozi kwa waafrika we need to change.
 
Huyo ni rais wa USA sio rais wa Tanzania. Jukumu lake ni kuipambania USA na sio kuisimamia Tz!

Hizi shida za Tz usimlalamikie Trump mlalamikie Samia, pia jilalamikie wewe kwa kuwa na akili fupi ya kuendelea kuichagua ccm wakati unaona kabisa hamna kitu wanafanya.

mkuu, umemaliza!

mnalia hamna dawa ila msafara wa Rais magari ya kifahari 110?!

stupid!


JESUS IS LORD&SAVIOR
 
Tanzania tunatakiwa kufanya reform kwenye mambo mengi sana mkuu huu ndio ukweli mchungu ambao viongozi wetu hawataki kuusikia.
Kuna mambo hayataki siasa ila sisi tunaingiza siasa maswala ya Afya, ulinzi, elimu ni sekta za muhimu sana zinazohitaji big brain tu kuziendesha.
Leo trump katufinya kidogo tumeshaanza kupoteana vipi akiamua ku -drill more deep lazima twende kupiga magoti.
Rejea kauli ya mkuu wa mkoa wa jiji pendwa majuzi hapa kuhusu mama mjamzito inatoa picha how Tanzania is...
BTW Ubalozi wa marekani ulikemea mauaji ya mzee wetu aliyetekwa mchana kwenye bus tukawaambia wasitupangie vivyohivyo na sisi tusiwapangie .
TRUMP anatoa somo la uongozi kwa waafrika we need to change.

Lisu for change!
 
Hamna mkataba wa ruzuku duniani baina ya taifa moja na lingine.
Kuna mkopo tu tena wenye benefits pande zote

Msaada si lazima , tatizo lenu mnakata kufanya ni jukumu. Trump yupo pale kwa mafuaa ya wa america si ya mtanzania
Mkuu Kama Kitu hukifahamu Sema!
Moja ya mikataba muhimu ni PEPFAR (President's Emergency Plan for AIDS Relief), ambayo ilianzishwa mwaka 2003 na Rais George W. Bush, ikiwa na lengo la kupambana na HIV/AIDS katika nchi za Afrika na duniani kote...
Mkataba Huu ndo trump Ameusimamisha..
 
Siku ya Januari 20, 2025, Rais wa Marekani Donald Trump alisaini agizo la rais (executive order) lililosimamisha kwa muda wa siku 90 utoaji wa misaada nje ya Nchi, ikiwemo programu muhimu za afya kama Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na UKIMWI. "President's Emergency Plan for AIDS Relief " (PEPFAR).

Kusitisha Huku Progran Hizo kutaathiti Dawa za Virusi vya UKIMWI (ARV), Dawa za kifua kikuu (TB), na Dawa za malaria na Dawa za Uzazi wa Mpango..

Ukiachana na Kuathiri Upatikanaji wa Dawa Taarifa ya USAID kuhusu Kupunguza kusitisha Misaada ya Viti hivyo Kumeanza Kuleta Effect kwa Baadhi ya NGOs Mashirika Mengi..

Yanayohusika na Utoaji wa Dawa za ARV,Kifua kukuu na Ukoma,Uzazi wa Mpango,na malaria yameanza Kuyumba na wote wameanza Kutoa Notice kwa wafanyakazi wao kusubiri na Kuangalia kama Marekani itarudisha Panga kwenye ala bhasi watarudi kazini...

Takribani Wafanyakazi wa Mashirika Tanzania 2900s Wanaenda Kupoteza Kazi kutokana Na upuuzi na Ego ya Trump..

Poleni Afya, Poleni Wafanyakazj wenzangu na Mostly Poleni wagonjwa ambao mnaenda Kuathiriki kwa Order hii Isiyo na Mashiko..


Yaani kodi za wamarekani ndio tunawanunulia Watu wetu dawa halafu Kodi zetu ni za safari na kula Bata na magari ya kifahari .

Hivi mtu kama Mwigulu anashindwa kununua gari lake mwenyewe la Kifahari kama alivyokua Marehemu Prof . Maji Marefu Mb. wakati huo?

Kwa nini tunashindwa kujitegemea kwa miaka yote ya uhuru . Wazungu wanafanya biashara zao wanalipa kodi sisi huku Wafanyabiashara wakubwa wanakwepa kodi na kusamehewa kodi . Yaani ujinga mtupu. Kwa nini pawe na misaada kwenye nchi yenye mabilionea wengi kama Tanzania lakini wanakwepa kodi na hakina jitihada za kuziba mianya ya kukwepa kodi zaidi ya kuzidi kupeana mianya ya kukwepa kodi na kujilimbikizia mali.

Kuna taasisis kama EWURA inaingiza mabilioni ya pesa kupitia mafuta ,maji na umeme .Je ,wanalipa kodi au PAE ni kwa wafanyakazi wenye vimishahara vya kuweka kwenye pochi ya mfukoni basi. ?

Kuna mahoteli huko Serengeti ,Mikumi na Loliondo yanainguza mabilioni ya pesa kwa siku . Je,wanalipa kodi inavyotakiwa au ni rushwa na tozo huko juu kwa juu .

Mo, ana Malaki ya ekari za ardhi . Je, anazilipia ipasavyo au anazitumia kwenye mikopo yake bila kuyaendeleza ? Mkonge unauzwa nje kwa maelfu ya Tani ,Je, kodi inalipwa ipasavyo.?
Mafuta yanayoingizwa nchini ,mitandao ya simu, TANESCO, gesi , Makaa ya mawe yanayosafririshwa nje kwa mamilioni ya tani tena kwa kutumia magari ya wakubwa .Je, yanalipiwa kodi inavyotakiwa ?

Madini ya dhahabu,nikeli , Tanzanite ,Almasi ,rubi ,viwanda vya maji yanayouzwa kwa bei inayokaribiana na mafuta toka Urusi je wanalipa kodi kwa mauzo ya kila sekunde mpaka vijijini , viwanda vya sementi ,Viwanda vya pombe vyenye wateja wengi sana je vinalipa kodi ipasavyo , viwanda vya sukari ,ngombe zinazochinjwa kwa maelfu kila siku ,je,zinalipiwa kodi ipasavyo au ni rushwa na kukwepesha kodi kisa Marekani watatoa misaada kwa kuwapigia magoti shingoni ukiwa umevaa mkufu wa dhahabu na kidani cha green safaya.?

Tatizo ni nchi maskini au ni viongozi wasio na kitu kichwani lakini mifuko imefurika kwa mapesa ya ujanja ujanja ?
Soko la ndani kubwa sana ukilinganisha na nchi kama Kenya Uganda na Rwanda lakini bado kodi inakua ni ya wachache na tozo zinaishia mifukoni mwa Wazabuni na wakurugenzi wanaowapa tenda hizo .Jioni mabaa yamejaa watu walioshiba vidonge vya ARV wakiwa wanakula Bata na mademu bia tamu na nyimbo nyingine kama vile ,"kama umenipenda basi nitongoze "

Ni vyema tukawakataa viongozi wasio faa na wabunge wao ili nchi ipige hatua na kuachana na misaada yenye masharti . Huu uwe ni wakati wa kujipanga kwani Trump ametikisa kiberiti tukadhani kimejaa kumbe hakina njiti.
 
Tanzania tunatakiwa kufanya reform kwenye mambo mengi sana mkuu huu ndio ukweli mchungu ambao viongozi wetu hawataki kuusikia.
Kuna mambo hayataki siasa ila sisi tunaingiza siasa maswala ya Afya, ulinzi, elimu ni sekta za muhimu sana zinazohitaji big brain tu kuziendesha.
Leo trump katufinya kidogo tumeshaanza kupoteana vipi akiamua ku -drill more deep lazima twende kupiga magoti.
Rejea kauli ya mkuu wa mkoa wa jiji pendwa majuzi hapa kuhusu mama mjamzito inatoa picha how Tanzania is...
BTW Ubalozi wa marekani ulikemea mauaji ya mzee wetu aliyetekwa mchana kwenye bus tukawaambia wasitupangie vivyohivyo na sisi tusiwapangie .
TRUMP anatoa somo la uongozi kwa waafrika we need to change.
Kabisa
 
Back
Top Bottom