Nilivoachwa kikatili na mpenzi wangu wa kwanza

Nilivoachwa kikatili na mpenzi wangu wa kwanza

Mlipo kutana na Dr H mlirudiana?. Baada ya kujua kama ilikuwa umbeya wa mwanaume wa mtaani?.
Hapana hatukurudiana Tena had now Kila mtu anamaisha yake sijui hata anaishi wapi ila ameshaoa nilipewa taarifa na dadayake
 
Hapana hatukurudiana Tena had now Kila mtu anamaisha yake sijui hata anaishi wapi ila ameshaoa nilipewa taarifa na dadayake
Ok pole sana maisha yana mapito mengi sana. Nilicho jifunza maishani mpenzi wa utotoni,shuleni hatokuwa mwenza wa maishani.
 
Ok pole sana maisha yana mapito mengi sana. Nilicho jifunza maishani mpenzi wa utotoni,shuleni hatokuwa mwenza wa maishani.
Ni kweli kabisa Huwa ni kupunguzia maji mwilini Kwa vilio hamna chochote
Kuna wakat najionaga mjinga kweli 😀😀
 
Hii wiki Niko very happy ngoja niwape kisa nilivyoachwa na mpenz wangu wa kwanza😃😃

Miaka mingi nyuma nilikuwa na rafikiyangu ambae ni jirani yetu pia alinizi kama miaka miwil umri, alikuwa anansoma shule ya boarding hivo tulikuwa tunaonana kipindi cha likizo.

Rafik yangu alikuwa ni wale watoto kwenye zile familia maarufu mtaani tumuite Irene
Siku moja tukiwa tunapiga story akanambia ana ujumbe kutoka Kwa H tumpe Hilo jina
nikamwambia anipe akaingia ndani akaja na barua 😃akasema Itabid nirudishe majibu kunamtu apewe aende nayo maana hayupo Kwa Sasa

Nikaichukua nikasema hebu nikaifungue nikiwa home bhana nafungua nakutana na ujumbe maridadi kweli kweli.

Barua ya mapenz iliyoshiba kweli kweli maneno matamu mwanzo Hadi mwisho nakupenda nying sana huku mwisho na dedication za kutosha nlisoma Ile barua huku natabasamu vibaya mno 😃😃

Kuhusu H
Ni mkaka fulani mpole sana ni binamu wa rafikiyangu hivo nilikuwa namuona maranyingi akija kutembea kwa shangazi yake huku mtaani kwetu.

Alikuwa anasoma shule moja ya kubwa ya seminary hapo mkoani babayake alisoma pamoja na mama yangu enzi hizo hivo namfahamu japo hatukuwa na ukaribu

Ile barua nilifurahia mno H alikuwa kijana smart sana,na hii ndo Ilikuwa mara ya kwanza kwangu kuvutiwa na mvulana nikamwambia akamwambie anipe muda nifikirie nitampa majibu wakat huo H alikuwa likizo Dar Kwa nduguzake wengine so barua alimpa rafikiyake wakiwa shule Ili inifikie Kwa urahisi na sikuwa natumia simu kipindi hiko.

Bas bhana feeling Kwa H zikaanza japo sikuwa naelewa Kwamba mapenzi ndio yalivo nikawa naona ni busara kuisoma Ile barua Kila mara Kwa kuirudia rudia😃😃😃

Baada ya wiki 2 nikaenda kwao na Irene Ile nafika sebuleni namkuta H kajaa tele nikaona aibu sana akanisalimia nikakaa kwenye kochi kiroho kinadunda sana nikaona hapa siwezi nikaaga nikaondoka muda huo H akanikata jicho la wizi wizi 😃

Wazazi wao hawakuwepo mda huo mara Irene akaniita niende kuongea na H

Akatoka nje nikamfuata tukakaa sehemu nyuma ya nyumba ya shangazi yake

Akauliza kuhusu jibu lake nikaanza kujizungusha zungusha nikakataa H alilalamika sana nikaona machozi yanaanza kumtoka 😭

Akabembeleza sana mwisho nikakubali wakat huo tumekaa mbali kidogo hivo hatukushikana hata mkono H akaaga akaondoka.

Safari ya mapenzi ikaanza
Kimbele mbele kikazidi 😃😃
Ilikuwa siku chache aondoke shule na Huwa akiwa shule hatumii simu mm pia sikuwa na simu kabisa akaja kuniaga akaondoka

Inaendelea sio ndefu
Pole sister maswali yangu ya logarithms hadi leo bado tu
 
Sasa log tu zinakushinda, tukikupa calculus utaweza kweli? Au complex numbers and imaginary numbers, hiyo ni pure mathematics ya advance.
Sasa zitanisaidiiaje wakat wa kusonga ugali hizo imaginatory sijui nn numbers jamn 😄
 
Sababu ni kweli ninakumbukumbu had za chekechekea hapa nilipo Nina afya njema,sinywi pombe sivuti bangi so akili yangu ni ngumu kusahau nakumbuka had nilosoma nae vidudu Kwa sura na matukio Yao yote
Mie vidudu namkumbuka mtu mmoja tu, nilimpenda yule mtoto kwa siku ya kwanza naanza pale Mabatini chekechea Ilala Shauri Moyo. Nakumbuka kabisa alivaa gauni jeupe kama la harusi kudadeki zake.
 
Mie vidudu namkumbuka mtu mmoja tu, nilimpenda yule mtoto kwa siku ya kwanza naanza pale Mabatini chekechea Ilala Shauri Moyo. Nakumbuka kabisa alivaa gauni jeupe kama la harusi kudadeki zake.
Hahaha ikaishiaje!
 
Mie vidudu namkumbuka mtu mmoja tu, nilimpenda yule mtoto kwa siku ya kwanza naanza pale Mabatini chekechea Ilala Shauri Moyo. Nakumbuka kabisa alivaa gauni jeupe kama la harusi kudadeki zake.
Chekechea mkuu 😄😄
 
Back
Top Bottom