Kuna rafiki yangu Mmarekani aliwahi kaniambia Mnawezaje kuishi sehemu mko congested namna hii.
Watu wanalazimisha kuigeuza Nyeusi kuwa Njano.Kwetu Mwanza. Nitapaongelea siku ingine. Lengo siyo kujionesha, ama kwamba napachukia nyumbani. TANZANIA NI KWETU. LENGO LANGU NI KWAMBA TUNATAKIWA KUJITATHMINI. KUDHANI TUMEFIKA KUNATUPOTOSHA.
Kwa hiyo unaniambia tangu watu waumbwe hapa duniani hakukuwa na maendeleo hadi tusubiri miaka ya karne ya 20 na 21 tudese kwa kikundi fulani cha watu wanaoishi West kujua nini maana ya maendeleo? Mbona hizo ni fikra duni sana yaani....! Yaani wewe kwa akili zako mababu zetu wa karne na karne zilizopita hawakuwa kupata ladha ya mafanikio, yaani ni sisi tu tuliopata bahati ya kuishi karne ya 21 kujua nini maana ya maendeleo. Tena kwa definition yako narrow ya maendeleo ni maendeleo ya West, vinginevyo hujaendelea au kufanikiwa!Dunia yote inaangalia west kama reference ya maendeleo. Si China wala Russia wanafanya hivyo. Technology ya China miaka yote imekuwa ni copycat. Viongozi wetu wote wamekuwa wanafanya reference ya Ulaya
Wewe ulitaka nitumie model ipi ya maendeleo?
Ok. Nitajie zote ulizotaja na mwaka kila nchi ilipata uhuru, vingenevyo nitajua hujui kitu kabisaNimetaja nchi nne tofauti kipi kilichofanya uitaje China pekee yake?
Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Uwezo wako wa kufikiri ni wa kati... Wenye uwezo angalau wa kueleweka wanakuja na mapendekezo baada ya kuonyesha tatizo hawaji na ukosoaji na kebehi pekee...
Nchi kama Tanzania hakuna kisichokuwa kipaumbele ndio maana huijui historia ya nchi yetu na hutaki kujifunza... Hatua za maboresho ya miundo mbinu, mazingira, afya, uzalishaji, usafirishaji, elimu, ajira na huduma za jamii zinahitaji fedha kununua teknolojia, ujuzi na mitambo, tafiti, kulipa ujira nk...
Ukiwa na hali tuliyonayo kama nchi unawezaje kubeza tulichonacho... Anza kujiuliza wewe mpaka sasa umechangia kiasi gani kuleta mabadiliko chanya kwenye nchi yako...nini mchango wako ...anzia ndani ya familia yako anzia hapo Mwanza alipo mama na baba yako umechangia kipi kuleta mabadiliko chanya kwa exposure uliyopata nje ya nchi... Umewezaje ku transform kilichopo kuwa bora kama ulichojifunza ulaya?
Ikiwa unaponda tu bila mapendekezo basi huitambui nafasi yako katika nchi na jamii in general.
Nitakupa mfano mdogo sana jiji la Dar (sasa Ilala) na zamani Mzizima kabla ya Sultan Seyyid Majid wa Zanzibar kuibatiza Mzizima jina jipya la Dar es salaam ni moja ya mji mkongwe... then 1891 Ujerumani walifanya mji mkuu wa kibiashara mpaka walipojenga reli ya kati 1904 Dar-Kigoma waliushikilia mpaka waliposhindwa vita 1940s then uingereza ika takeover mpaka 1961 ....maana yangu ni nini muda wote huo mji ulikuwa unaendelea kuongezeka wakazi na makazi kwa kasi kiasi kwamba uwezo wa serikali ya kiraia kuuhudumia mji ulikuwa mdogo... Sasa leo hii ndio hizo pangua pangua, bomoa bomoa zinakuja kutokana na jiographia ya Dar kumekuwa hakuna mbadala kwa baadhi ya maeneo kuruhusu ujenzi wa kisasa unao utaka... Madaraja ya coco nk nikatika kuufungua mji na kupunguza compessision cost, kupunguza relocation endapo utawatoa watu katika maeneo yao.... Utaona mifumo ya maji safi na taka ilivyozidiwa [iliundwa kuhudumia watu laki 4.5 leo wapo 6m+] na sasa inaboreshwa na kuanzisha mipya...
Walau umekiona ulichokiona na ukaweza kufanya mlinganyo kuliko kisingekuwepo kabisa...
Anyway ulitoa mawazo yako nimekuelewa hata kama sikukubaliana nawe. Maana kumwelewa mtu kunasaidia kujua uwezo wake.
Pole mkuu. Ndiyo madhara ya kujikuta upo upande huo.Huna unalojua kilaxa wewe.
Ukweli uambatane na ushauri namna ya kufikia hicho kiwango mnachokiona huko ng'ambo! Ukweli huku unachombeza kwa lugha zisizo na staha, tunarudi kwenye lugha za kuudhi.Kuwaambia watu ukweli unaoonekana kama matusi ya mjivuni anayetukana kwao baada ya miaka michache ya kukaa Ulaya kunataka diplomasia ya hali ya juu sana.
Hapo ndipo nilipoanza kuona 'mwamba' anatembea ameinama kisa eti akisimama mbingu itamuumiza utosi wake!Mwamba analalamika ulaya hakuna neti lakini halalamiki ulaya hakuna mbu
Rwanda kwenye usafi wako vizuri mkuu,kwa jiji kama dar nilitegemea mtu kama kunenge angesimamia usafi na vile kujaribu kupunguza wafanyabiashara wadogo wadogo kwa kuwatafutia maeneo mengine ya kufanya biasharaUmeongea ukweli mkuu,
Nchi zetu za kiafrica tuna janga kubwa la kukosa right leadership Hali iliyofanya tushindwe kusimamia mambo ya msingi km mipango miji na usafi
Ukiangalia nchi kama Tanzania leadership chain imepararaizi kila kitu mpaka rais au waziri mkuu aseme
Wabunge, madiwani, wenyeviti wa mtaa hawa wote ni kama hakuna wanalofanya kila kitu wameiachia serikali kuu ifanye
At least nchi km Rwanda wamejitahidi Sana Leo hii Rwanda ukienda Hadi vijijini ni kusafi si mchezo coz Hadi wenyeviti wa mtaa wanatimiza wajibu wao ipasavyo.
Jamaa mzushi tu,wengine tunaishi kwa watu toka 2005 na tukirudi nyumbani unaona kuna kijihatua kimepigwa,shida ya dar uchafu tu na vile vibanda vya wafanyabiashara vilivyozagaa bila mpangilio kila mahali ndio vimeharibuKuna ukweli fulani hivi...
Ukienda nchi za wenzetu ukakaa muda kidogo na ukirudi hapa... dah!! Unapaona pa hovyo sana...
Summer ulaya kuna mbu tena ile mimbu mikubwa unaweza kudhani spider,uzuri wake mbu wale awaambukizi malariaMkuu wangu KWA swala la mbu
Nikujulishe mbu wanapatikana kwenye tropical climate , Africa karibu yote iko kwenye tropical area kasoro the most south na the most north ambazo ni subtropics
Kushangaa mbu Africa naona ni kukosa tu uelewa mbu anazaliana KWA wingi Africa sababu ya hali ya hewa ,Ulaya hakuna mbu si KWA sababu wamemdhibiti hapana ni KWA sababu hali ya hewa hairuhusu kuzaliana huko
Kushangaa ugonjwa wa malaria Africa ni sawasawa na kushangaa ugonjwa wa Frost bite Ulaya , Africa KWA namna yoyote hatuwezi kuugua FROST BITE sababu ya hali ya hewa huo ni ugonjwa wa maeneo ya extreme cold wala Ulaya huwezi kukuta malaria maeneo yao mengi ni frigid na malaria inastawi kwenye tropical climate
Acha ulimbukeni!! Ndiyo najifariji kwani kujifariji dhambi??? si ndivo nilivyo?? Siwezi jikataa kamwe uswahilini kwetu piga ua galagaza! naweza pabadilisha pakawa pazuri washamba mnaita uzunguni!Wabongo tukiambiwa ukweli tunalialia Sana.
Tembeeni nchi za watu muone tulivyo nyuma.
Siku moja nenda katembee hata hapo windhoek - Namibia uje kusimulia hapa wenzenu wanavyoishi.
Hakuna mtu anapenda kuishi maisha ya kijinga ya uswahili. Sema ni umasikini tu tunashindwa kuishi maeneo mazuri usijitetee eti unapenda uswahilini sema huna hela ya kuishi sehemu Bora.
Diamond kazaliwa Tandale ila leo anaishi mbezi beach kwani Tandale hapaoni.
Mama Diamond anaishi zake madale.
Mbosso alikuwa anaishi huko uswazi mbagala Ila sasa hivi anaishi zake Mbweni.
Lavalava Yuko upanga.
Hawa ni mastaa wachache ninaowajua walikuwa wanaishi Uswazi ila baada ya kuzipata wamehama Uswazini na kutuacha sisi masikini.
Maisha ya uswazi Ni umasikini tuache kujifariji na vitu vya kipumbavu.
Naona unaleta stress zako kujibu Mambo usiyoelewa.Acha ulimbukeni!! Ndiyo najifariji kwani kujifariji dhambi??? si ndivo nilivyo?? Siwezi jikataa kamwe uswahilini kwetu piga ua galagaza! naweza pabadilisha pakawa pazuri washamba mnaita uzunguni!
Hiyo sinza, mbezi beach, msasani yalikuwa mashamba ya mpunga.enzi hizo!
Nimekaa Evertone green, Downing street maisha yangu ya utoto lkn mabatini Mwanza sikupabagua hata chembe na leo hii ni zaidi ya palivo kuwa.
Siyo siri Watu mliokulia mashambani mna shida sana.mkiona vimiji vidogo vidogo!
Hao ni wanaume wenzako walijenga miji yao na wewe kajenge kwenu pawe pazuri uwazidi.
Nenda Machame, kanyigo-Bukoba! Kenyamanyori-Tarime.kirigiri ni zaisi ya Ulaya. Kericho rural area -kenya.
Quachasnake -lesotho. Ubirunga-wastern cape nk huko ni zaidi ya Ulaya.
Hutarudi na ujinga huu hapa tena kajenge mwenyewe kwenu usibabaike na vimiji vya watu.
Humu humu tu tumejitahidi sana kuliko hata hayo majinga yako.
Wachaga hoyeee!! Wakurya. wajita wahaya hoyeeeee!!! huko ni zaidi ya huo utoporo wako! Huku ukijichanganya tu umekiwa km wao! Hkn ubaguzi mkioleana ndo kabisaaaa! Ni shimbonyi ahafoo tuuu!! Mpaka basi.
Najua kule kwenu ukerewe mnalogana sana. Ndo maana unatamani vimiji vya wenzako!
Dsm yetu iache km ilivo!!! Tunapenda kwa jinsi tulivyo usituletee ulimbukeni wako huo!!!
Tumetoka mbali na siasa zetu za jiji!!!! Endelea kubeba ma box.