Nilivyoyaona maendeleo ya Tanzania baada ya kuwa Ulaya kwa zaidi ya miaka minne

Nilivyoyaona maendeleo ya Tanzania baada ya kuwa Ulaya kwa zaidi ya miaka minne

Kwa ijumla miji ya Tanzania kimpangilio, ni ovyo sana.

DSM, sijui utailinganisha na mji gani!!

Achilia mbali miji ya Ulaya, hata ukilinganisha na miji ya Afrika tu, DSM si lolote, si chochote.

Hayo madaraja yanayoitwa flyovers, si chochote. Nilienda wakati fulani Bamako, Mali, nchi ambayo karibia robo tatu ni jangwa, ina mpangikio mzuri, mara 10 zaidi ya Dar. Flyovers wala siyo kitu cha kuongelea, ni kitu cha kawaida, na sijui zipo ngapi!!

Ukienda tu hapo Maputo, mji umejengeka na kupangwa hasa, japo pembeni kabisa huko, ni takataka. Lakini kati kati ya mji, ni mji hasa. Tunajisifu na daraja la Nyerere, letu ni fupi kuliko la Maputo.

Nenda Harare, Dar ni takataka.

Sisi tatizo letu, mafanikio kidogo, kelele ni nyingi sana.
Tusijidharau kiasi hicho. kikubwa tujue historia. Tanganyika baada ya vita ya kwanza kumalizika ilikabidhiwa kwa waingereza ili waishikirie mpaka tutapo weza jitawala. Hivyo hatukuwa koloni la mwingereza.

Tulikuwa under (British Protectorate) Hii ilimfanya Mwingereza hasifanye maendeleo yoyote ya maana. Kwani alijua kabisa ipo siku anaondoka. Hakuweza kuwekeza kama ilivyokuwa kwa mjerumani. Japo Mjerumani alikaa kwa muda mfupi. Ndo maana wakati wa uhuru Nyerere alienda Umoja wa Mataifa kudai Uhuru kuwambia tuko tayari kujitawala.

Hii ni tofauti na nchi ambazo zilikuwa makoloni kama Zimbabwe, Kenya na zinginezo. Hizi nchi wazungu walikuwa Settlers, walifanya makazi ya kudumu kama ilivyo Maputo. Walijenga na kupangilia miji kama ilivyo Ulaya. Hii ni tofauti na Dar ambayo wewe na mimi tunapata vimishahara vyetu tunajijengea nyumba kulingana na uwezo wetu.

Tembelea nchi ambazo hazikuwa na ma settlers miji yao haijapangika na kuna nyumba nyingi za hali ya chini. Mfano Ethiopia, ni mji mzuri lakini tembea mitaani utajua. Nenda Somalia pia. Ni baadhi tu. Tusijidharau Dar imepiga hatua, Dar ya mika ya 90 haikuwa hii ya leo. Nakumbuka Kariakoo kulikuwa na nyumba za makuti. Nyumba za Miti na tope zikaezekwa kwa mabati chakavu.

Kuna wakati upepo ulivuma na kuondoa paa kadhaa na kuleta maafa. Hiyo ilikuwa 1993. Kariakoo hakukuwa na barabara za lami. Ilikuwa Vumbi. barabara ya kunduchi, Tegeta mwenge balaa ilikuwa unapanda mabasi kama ya mikoani yanaanzia kariakoo, tena ya kusubiria. Mwenge kulikuwa na chai maharage.

Tegeta ndo ilikuwa mwisho wa mji. Huko Boko, Bunju ilikuwa ni kijijini, watu wanalima.

Tujipongeze hata kwa hivi vichache tulivyovipata kwa nguvu zetu. Kubeza haisaidii, kuwa proud na ulichonacho.
 
Mimi sijidunishi. Naipenda nchi yangu. Nimekuja huku chumbani, japokuwa kuna wa mataifa mengine wanaweza kusoma, kuteta ili ikiwa kuna viongozi basi wachukue hatua. NAIPENDA SANA TANZANIA MPAKA KUNA KIPINDI NATOA MACHOZI YA WIVU NIKIONA MIJI YA LEVEL YA KIDUNIA INAVYOPENDEZA ILI HALI SISI TUKIWA NYUMA
Mi nakuelewa vizuri sana. Nimekaa Ulaya pia naelewa jinsi ambavyo kuna utofauti sana wa mazingira na lifestyle za watu baina ya Ulaya na Tanzania.

Ila nikwambie kitu? Si kweli kwamba maendeleo yetu reference yetu inapaswa kuwa nchi za Ulaya au Marekani au wapi kwingineko huko. Hivyo ndivyo akili za kitumwa zilivyo kuwa programmed. Watu huru, akili huru, huwa zinatengeneza maendeleo yake kwa taswira zao wenyewe. Je unafahamu kabla ya ukoloni Afrika ilikuwa na superior civilizations zilizokuwa hazijaiga popote pale bali kwa kupitia ubunifu wake mwenyewe?

Mababu zetu waliishi kwenye nyumba safi tu (hata kama sio za bati), walijitibu magonjwa yao kupitia traditional medicine, waliwasiliana kwa masafa marefu, walifuga na kulima na kujitosheleza chakula, kufarakana na kupatana bila kutumia reference yoyote. Bila ukoloni, I tell you tungekuwa tupo mbali sana kimaarifa, kiteknolojia na kimaendeleo.

Ukoloni ulitulazimisha tuanze kuyaona maendeleo kupitia miwani ya waliotukoloni. Ndio maana hata wewe unahisi vya kwetu bado duni. Kisa reference yako ni Ulaya?
 
Kuna wakati nilikuwa na jamaa waliotoka Ulaya. Tulikuwa kwenye chopa iliyokodiwa toka South Africa. Wale bwana ilikuwa mara ya kwanza kutembelea nchi ya Afrika, nje ya Afrika Kusini.

Tulitua eneo moja mkoani Tabora. Nikawaona wameduwaa. Nikawauliza kuna nini? Wakasema, hawa watu maisha haya wanaoyishi, nikisoma vitabu vya historia kule kwetu, inaonekana ni aheri maisha ya karne ya 18 Ulaya.

Ndiyo maana wenye akili wakimsikia mtu akisema kuwa Tanzania ni tajiri, tupo vizuri - hawawezi kuelewa kama huyo mtu ni mzima kabisa!!
Ndugu yangu wazungu au jamaa zako wakishangaa sijui tunaishije nawe washangae wanaweza kuishije kwenye apartment ambazo ukipiga hatua huko chooni, hatua upo sitting, hatua nyingine chumba cha kulala. Nyumba utazani ni sero

Kuna siku Mzungu mmoja ni msomi ana PhD, aliwahi ishi Tanzania tulikutana nchi moja Ulaya. Akaanza kuleta dharau ati alienda Arusha watanzania tunapanda katika gari na mbuzi. Eti kwanini mbuzi mnyama na watu wanapanda gari moja.

Nilimtazama, nikamwambia mbona nanyi huku Ulaya tunawashangaa mnapanda na mbwa katika gari la abiria, mbwa ni mnyama. Na mnalala nae kitandani. Ni kamuuliza kuna utofauti ipi na Tanzania? Tanzania uliona Mbuzi kwenye gari huku mbwa kwenye gari na wote ni wanyama.

Mzungu alinitazama akanambia, "umenifundisha kitu. Na umenipa challange"! Toka siku hiyo ananiheshimu sana. Tukawa marafiki wakubwa hadi leo. Na baadae alifall in love. Watanzania tusipende jidharau.
 
Mi nakuelewa vizuri sana. Nimekaa Ulaya pia naelewa jinsi ambavyo kuna utofauti sana wa mazingira na lifestyle za watu baina ya Ulaya na Tanzania.

Ila nikwambie kitu? Si kweli kwamba maendeleo yetu reference yetu inapaswa kuwa nchi za Ulaya au Marekani au wapi kwingineko huko. Hivyo ndivyo akili za kitumwa zilivyo kuwa programmed. Watu huru, akili huru, huwa zinatengeneza maendeleo yake kwa taswira zao wenyewe. Je unafahamu kabla ya ukoloni Afrika ilikuwa na superior civilizations zilizokuwa hazijaiga popote pale bali kwa kupitia ubunifu wake mwenyewe? Mababu zetu waliishi kwenye nyumba safi tu (hata kama sio za bati), walijitibu magonjwa yao kupitia traditional medicine, waliwasiliana kwa masafa marefu, walifuga na kulima na kujitosheleza chakula, kufarakana na kupatana bila kutumia reference yoyote. Bila ukoloni, I tell you tungekuwa tupo mbali sana kimaarifa, kiteknolojia na kimaendeleo.

Ukoloni ulitulazimisha tuanze kuyaona maendeleo kupitia miwani ya waliotukoloni. Ndio maana hata wewe unahisi vya kwetu bado duni. Kisa reference yako ni Ulaya?
Dunia yote inaangalia west kama reference ya maendeleo. Si China wala Russia wanafanya hivyo. Technology ya China miaka yote imekuwa ni copycat. Viongozi wetu wote wamekuwa wanafanya reference ya Ulaya
Wewe ulitaka nitumie model ipi ya maendeleo?
 
Leo ndo nimemuelewa JPM kuhusu watoto wetu kuijua historia ya nchi yao.... Ukijua mmetoka wapi, mkoa wapi na mnaenda wapi unaweza kuja na uzi tofauti na huu.
 
Mtoa mada yaani umejitahidi sana kuongea hali halisi

Mimi maisha yangu yote ninaishi Tz na nimebahatika kidogo tu kutembea karibia mabara yote ukitoa mawili tu ya America Kusini na Kaskazini

Yaani huwa nikiongea na watu kwamba bado tupo nyuma sana kwa mipango miji na hata jiji kama Dar ambalo ni kioo na lango la nchi naishia kuwa mpole tu maana naonekana najidai labda kwa kuwa nimetembea kidogo baadhi ya miji ya wenzetu

Kuna vitu vidogo tu lkn bado tumelala usingizi hasa na sijui idara zetu na hata wasomi wetu wa mipango miji wanaonaje, yaani ukitoa uchafu kuna maeneo mengi usiku ni giza hasa (Kwa Dar) lkn ilipaswa kuwa na taa za barabarani na jingine dogo tu hatuna mabango ya maana kuonesha mitaa yetu na barabara zetu na wapi upo na ukienda wapi panaitwaje yaani ni shaghala baghala, sasa ukute watu wakionyesha hayo maendeleo unaweza cheka tu na kukaa kimya na mbaya muelekeo wetu kama Taifa ni kuacha legacy ya vitu, barabara, madaraja na miundo mbinu kwa jumla lkn ukiona viwango vya hivyo vipaumbele vyetu unajua bado tuna kazi sana

Nacho ona kwa Dar au Tanzania nzima ni eneo la kuanzia Morroco pale kuelekea Mwenge at least linaleta picha fulani ya jiji la maana vinginevyo bado sana mliokabidhiwa mamlaka tokeni mjifunze miji inavyotakiwa kupangwa ( hata kwa taa za barabarani na mitaa na mabango Ya kuonyesha ulipo na uendako) tafadhali kinyume chake tukubali sisi ni Taifa masikini sana
 
Kwetu Mwanza. Nitapaongelea siku ingine. Lengo siyo kujionesha, ama kwamba napachukia nyumbani. TANZANIA NI KWETU. LENGO LANGU NI KWAMBA TUNATAKIWA KUJITATHMINI. KUDHANI TUMEFIKA KUNATUPOTOSHA.
Lengo lako linaweza kuwa ni zuri, ila presentation yako ni very poor. Kwa watu wanaojua 'Participatory Evaluation Process' ya kuhamasisha watu kujitathimini na kuleta mabadiliko, your presentation is a 95% assured failure. Kwa kukuemisha kidogo: kuhamasisha kwa kukandia ufanisi wake huwa ni mdogo sana.
 
Mtoa mada yaani umejitahidi sana kuongea hali halisi

Mimi maisha yangu yote ninaishi Tz na nimebahatika kidogo tu kutembea karibia mabara yote ukitoa mawili tu ya America Kusini na Kaskazini

Yaani huwa nikiongea na watu kwamba bado tupo nyuma sana kwa mipango miji na hata jiji kama Dar ambalo ni kioo na lango la nchi naishia kuwa mpole tu maana naonekana najidai labda kwa kuwa nimetembea kidogo baadhi ya miji ya wenzetu

Kuna vitu vidogo tu lkn bado tumelala usingizi hasa na sijui idara zetu na hata wasomi wetu wa mipango miji wanaonaje, yaani ukitoa uchafu kuna maeneo mengi usiku ni giza hasa (Kwa Dar) lkn ilipaswa kuwa na taa za barabarani na jingine dogo tu hatuna mabango ya maana kuonesha mitaa yetu na barabara zetu na wapi upo na ukienda wapi panaitwaje yaani ni shaghala baghala, sasa ukute watu wakionyesha hayo maendeleo unaweza cheka tu na kukaa kimya na mbaya muelekeo wetu kama Taifa ni kuacha legacy ya vitu, barabara, madaraja na miundo mbinu kwa jumla lkn ukiona viwango vya hivyo vipaumbele vyetu unajua bado tuna kazi sana

Nacho ona kwa Dar au Tanzania nzima ni eneo la kuanzia Morroco pale kuelekea Mwenge at least linaleta picha fulani ya jiji la maana vinginevyo bado sana mliokabidhiwa mamlaka tokeni mjifunze miji inavyotakiwa kupangwa ( hata kwa taa za barabarani na mitaa na mabango Ya kuonyesha ulipo na uendako) tafadhali kinyume chake tukubali sisi ni Taifa masikini sana
Nimekuelewa ndugu. Kwa waliotembea wanaweza kuelewa. Ila wengi hata huu uzi wanaona ni majivuno.

TUNA SAFARI NDEFU SANA
Leo ndo nimemuelewa JPM kuhusu watoto wetu kuijua historia ya nchi yao.... Ukijua mmetoka wapi, mkoa wapi na mnaenda wapi unaweza kuja na uzi tofauti na huu.
Sihitaji kujifunza history ya nchi yangu mara nyingine maana naifahamu na pia nalipenda taifa langu kwa dhati ya moyo. NASIKITISHWA NA MIPANGO MIJI YA NCHI YETU.
 
Masahihisho : Hakuna daraja la Kijazi pale panaitwa Kijazi Interchange , kama hujui uliza kwanza bhana , hata pale Tazara panaitwa Mfugale flyover
 
Hii excuse haijawahi kuwa valid, mbona nchi kama Korea, china, taiwan, Singapore tumepata Uhuru nao Sawa lakini kwenye miundo mbinu wamepiga hatua Sana?
Unajua china ilipata uhuru lini ?
 
Sihitaji kujifunza history ya nchi yangu mara nyingine maana naifahamu na pia nalipenda taifa langu kwa dhati ya moyo. NASIKITISHWA NA MIPANGO MIJI YA NCHI YETU.
Uwezo wako wa kufikiri ni wa kati... Wenye uwezo angalau wa kueleweka wanakuja na mapendekezo baada ya kuonyesha tatizo hawaji na ukosoaji na kebehi pekee...

Nchi kama Tanzania hakuna kisichokuwa kipaumbele ndio maana huijui historia ya nchi yetu na hutaki kujifunza... Hatua za maboresho ya miundo mbinu, mazingira, afya, uzalishaji, usafirishaji, elimu, ajira na huduma za jamii zinahitaji fedha kununua teknolojia, ujuzi na mitambo, tafiti, kulipa ujira nk...

Ukiwa na hali tuliyonayo kama nchi unawezaje kubeza tulichonacho... Anza kujiuliza wewe mpaka sasa umechangia kiasi gani kuleta mabadiliko chanya kwenye nchi yako...nini mchango wako ...anzia ndani ya familia yako anzia hapo Mwanza alipo mama na baba yako umechangia kipi kuleta mabadiliko chanya kwa exposure uliyopata nje ya nchi... Umewezaje ku transform kilichopo kuwa bora kama ulichojifunza ulaya?
Ikiwa unaponda tu bila mapendekezo basi huitambui nafasi yako katika nchi na jamii in general.

Nitakupa mfano mdogo sana jiji la Dar (sasa Ilala) na zamani Mzizima kabla ya Sultan Seyyid Majid wa Zanzibar kuibatiza Mzizima jina jipya la Dar es salaam ni moja ya mji mkongwe... then 1891 Ujerumani walifanya mji mkuu wa kibiashara mpaka walipojenga reli ya kati 1904 Dar-Kigoma waliushikilia mpaka waliposhindwa vita ya kwanza then uingereza ika takeover mpaka 1961 ....maana yangu ni nini muda wote huo mji ulikuwa unaendelea kuongezeka wakazi na makazi kwa kasi kiasi kwamba uwezo wa serikali ya kiraia kuuhudumia mji ulikuwa mdogo... Sasa leo hii ndio hizo pangua pangua, bomoa bomoa zinakuja kutokana na jiographia ya Dar kumekuwa hakuna mbadala kwa baadhi ya maeneo kuruhusu ujenzi wa kisasa unao utaka... Madaraja ya coco nk nikatika kuufungua mji na kupunguza compessision cost, kupunguza relocation endapo utawatoa watu katika maeneo yao.... Utaona mifumo ya maji safi na taka ilivyozidiwa [iliundwa kuhudumia watu laki 4.5 leo wapo 6m+] na sasa inaboreshwa na kuanzisha mipya...

Walau umekiona ulichokiona na ukaweza kufanya mlinganyo kuliko kisingekuwepo kabisa...

Anyway ulitoa mawazo yako nimekuelewa hata kama sikukubaliana nawe. Maana kumwelewa mtu kunasaidia kujua uwezo wake.
 
Tanzania in ukweli usiopingika imepiga hatua kubwa kwenye ujenzi wa miundo mbinu
1.madarja makubwa + madogo
2.usafiri was angaa
3.usafiri wa majini
4.miundo mbinu mashuleni
5.miundo mbinu mahospitalini.nk
 
Back
Top Bottom