Nimeamini masharti ya marehemu wakiyasema kabla ya kukata roho

Nimeamini masharti ya marehemu wakiyasema kabla ya kukata roho

kaka we shika nilivyokuambia, kichwa kiangalie mnakotoka na miguu mnakokwenda. Nina mambo mengi tu kwa mfano ukitaka namna ya kumkamata mwanga ama mchawi akiingia nyumbani kwako sema tu nikumwagie hapa, dawa za kumvuta mwanamke ama mwanaume akufuate popote ulipo hata kama ni usiku ninazo pia, ila haifanyi kazi kwa mke / mme wa mtu - sina uchoyo na hii elimu maana na mimi nilipewa bure.

Masuala ya kazini pia yako - vyeo, mshahara nk
Unajadili Mada au unatangaza Biashara?
 
andaa mshumaa
andaa sindano
andaa kitambaa cheupe
andaa tunda unalolipeda sana kulila
andaa udi
andaa chumvi ya mawe

ukimaliza kuviandaa ni PM tumalize kazi.
Kwahiyo uliusubiri Uzi wangu huu ndiyo utangaze Biashara yako hii Ndugu?
 
Wanama said:
Embu lete iyo ya kumvuta mwanamke Kuna pisi apa imekula pesa zangu sanaa
Siku hizi wanaume wanaloga wanawake kuliko wanawake walivyodhaniwa


andaa mshumaa
andaa sindano
andaa kitambaa cheupe
andaa tunda unalolipeda sana kulila
andaa udi
andaa chumvi ya mawe

ukimaliza kuviandaa ni PM tumalize kazi.

😳😳😳
 
Tusidanganyane hapa. Hizi ni hadithi za Abunuasi tu. Eti jeneza linagoma kubebeka??

Acheni hekaya zenu za vijiweni na imani potofu zilizojaa udanganyifu. Hizi porojo hazina ukweli wowote. Mtu akifa, amekufa. Hana uwezo wa kufanya chochote kwa walio hai.
Unamwambia nani sasa🤫🤫
 
kauli za mwisho za mtu ziheshimiwe mfano babu yangu aliagiza akifa azikwe kavalia suti yake nyeupe na alikua kaipasi vyema kaihifadhi ktk begi, nikafunga safari hadi kijijini nikaichukua akavalishwa then ndo tukampeleka kumzika nyumbani kwake.

Ni jambo jema pia kama ni swala lipo ndani ya uwezo wenu mkashindwa kutimiza huwa yanatokea yakutokea unless otherwise mseme muweke kikao jeneza likiwa hapo mzungumze then mfuate udOngo wa nyumbani kwake ndo mumzikie kama mdau juu hapo alivyoelezea.

Ndugu wakigombana wakafikia hatua ya kuambiana nikifa usinizike jaribuni kuwapatanisha kivyovyote ikiwezekana iyo kauli ifutwe kabisa.
 
Tusidanganyane hapa. Hizi ni hadithi za Abunuasi tu. Eti jeneza linagoma kubebeka??

Acheni hekaya zenu za vijiweni na imani potofu zilizojaa udanganyifu. Hizi porojo hazina ukweli wowote. Mtu akifa, amekufa. Hana uwezo wa kufanya chochote kwa walio hai.
Uje tuu ukiuke maagizo yake maneno mengi ya nini? Ila usisahau kuleta mrejesho
 
Waafrika na Jadi zetu...
Huenda tumekua bara maskini kwa kuacha kuendeleza Mila na Desturi zetu
Watu wanaendekeza Mila za kufirana za wazungu,dini zao na upuuzi mwingine kama huo wa kufanywa misukule ya kusubiria miujiza huku wajanja wanawakula.

Ndio maana nilishaachaga mambo ya kijinga mimi,India Wana Mila zao wako vizuri,wajapan,wachina,wakorea,waarabu nk kote wanafanya Mila zao wameendelea.Huku kulikojaa mijinga sasa duu.
 
Akikataa kuzikwa eneo A, akang'ang'ania kuzikwa eneo B. Na ninyi ndugu kwa sababu za msingi sana mkaona azikwe eneo A msipate shida sana. Kukwepa hayo mabalaa tumeni ndugu mmoja wa Kiume eneo B akachukue udongo kidogo katika kisado aulete eneo A...
Yesuuuuu mbona vinatishaa hivyooo
 
Huyo marehemu ni mpumbavu? Sasa kuna faida gani? Umekataa asije kukuzika lakini mali zako anatumbua na hawara yake? Halafu unakimbilia kufumbua macho ndani ya jeneza, hivi ana akili kweli huyo mume? Na ndiyo maana akapewa sumu. Alitakiwa na yeye kulipa kisasi kabisa, sio kujifumbulisha fumbulisha macho, shame on him!
Sasa akija kukuzika ndio ataacha kutumbua mali? Hapo unamkomoa kinafsi,kwanza hiyo marehemu alikuwa hajamchukia vizuri angekuwa kajiapiza sawasawa mbona hako kamwanamke mungezika na polisi kadhaa
 
Back
Top Bottom