Nimechoshwa na Huu umungu mtu unaooneshwa na serikali! Mpaka Sasa Mshahara haujatoka? Mnatuchukuliaje?

Tulieni nyie, tuulizeni wenzenu tulioko mashirika binafsi huwa tunalipwa tarehe ngapi na hatuna kelele.
Jifunze nidhamu ya pesa, usiishi kwa tarehe za mshahara.
Sasa unalinganisha mshahara wa mashirika binafsi na wa wafanyakazi wa umma mbona ni mbingu na dunia labda mashirika binafsi uchwara ,
 
Nani aliwaambia mchague kijani?haya ndio madhara yake.wenzenu wako bungeni wanaendelea kula Bata na nyie endeleeni kwenda kukopa kwa mangi
 
Ushamba tu unakusumbua. Fanya mshahara kuwa ziada
 
sasa serikali imefanya nini tena wakati rais wa tucta kasema mshahara uwe unatoka tarehe 28-30 mnataka nini tena
 
Haha uliza awamu ya nne watu walikuwa wanaishije.
 
sasa serikali imefanya nini tena wakati rais wa tucta kasema mshahara uwe unatoka tarehe 28-30 mnataka nini tena
Rais wa tucta ni nani ndani ya nchi hii? sio mwajiri bwana iyo kauli ipuuzwe na kama ni kweli kasema mlio Wanachama wa tucta mnajua cha kufanya moja nikujivua uanachama abaki mwenyewe , mbona simple.
 
Samahani kuingilia Kesi ila nahisi wewe Ndo hufahamu..

Serikali inamifumo yake ya Kiutaratibu ya Utendaji kazi..

Ikiwemo Tarehe, Mwezi na mwaka..
MWezi wa serikali kwa mwaka 2023/2024 Tangu June 2023...
Ulianza Tarehe 24 mpaka tarehe 23.. ya Kila mwezi..

Na mwaka wa Serikali Huanza (July 1 ni mwanzo wa mwaka) mpaka june tarehe 30 (Ambayo ni mwisho wa Mwaka)..

January sio mwanzo wa Mwaka Kiserikali japo Kijamii january ni mwezi wa mwanzo au Mwanzoni mwa mwezi kiserikali..

Vivo hivyo Tarehe 21 mpaka tarehe 23 Ni mwisho wa Mwezi kiserikali....

Kiserkali (upande wa Mishahara) Tarehe 30 sio mwisho wa mwezi ila Terehe 30 ni siku ya Kufunga hesabu za mwezi..

Watumishi toka mwaka huu wa 2023/2024 na miaka mingine ya Nyuma Umeanza wamekuwa Wakipokea Mshahara tarehe 21 mpaka 23..

Hivyo kuvuka Tarehe 23 Huesabika ni siku zaidi ya 30 za Kiutumishi (Kama utapiga hesabu vizuri)..

Kwa siku ya Leo ni Tarehe 1 Ya mwezi Mwingine yaani siku ya 32 ya mwezi mwingine japo kulimgama na mwezi uliopita Mshahara uliingia Tarehe 21 kwahyo keo ni Tarehe 33 Tangu wapokee Mshaahara..

Nadhani utakuwa umenielewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…