Kwamba uwekezaji ndio umeanza kufanyika leo Tanzania ?!!! Miradi mingapi na Ubinafsishaji upi ambao umekuwa positive..., Mwisho wa siku ni watu kuja kuandika vitabu na kuomba misamaha kwamba walikosea walichofanya
Kwahio kwa akili yako unadhani effect ya Bandari Kuu ya Tanzania ni kwa wale ambao wapo kwenye vicinity ya Bandari pekee; na Nani aliyekwambia watu wanapinga kumpa mtu lease / uendeshaji (hata aliyekuwa pia si alipewa mkataba) au hayo huyajui ? Tena na mkataba ule ulikuwa mbovu (kwahio walewale ambao walileta mkataba mbovu ambao ilibidi uwe wa miaka mitano ya uchunguzi alafu iongezwe iwe kumi badala yake hata kabla ya miaka mitano kuisha ikaongezwa kuwa kumi na tano)....; Kwamba hawahawa walioharibu jana leo ndio tuwaamini kwamba wanachosema ni sawa and they will do the right thing ?!!! (No Question Asked)!!! Kwa kufanya hivyo tutakuwa hatutekelezi wajibu wetu kama walipa kodi
Kwamba bila DPW wala bila kurekebisha vitu watu wanavyolalamika au labda kupunguza muda wa lease / tender au kuondoa exclusivity hizo shughuli hazitarahisishwa...; tena sababu jamaa watakuwa na mandate bila kuingiliwa na kuchunguzwa kwa undani usishangae kuona madawa ya kulevywa na vitu vya ajabu ajabu vikazagaa (after all it depends katika makubaliano tumewapa leeway kiasi gani)
Aisee hao pingapinga ndio wanatakiwa sababu through challenges na criticism watu ndio wanaboresha; kwani hao pingapinga walipinga kuwahi asubuhi au huenda mchakato ulivyokwenda na value for money baina ya uwekezaji na matokeo..., By the way Usafiri Dar ?!!! uliza kipindi cha UDA katika its peak na zile basi Icarus Kumba-Kumba wakwambie mambo yalikuwaje na usafiri huu ulikuwaje....; Tusichanganye mambo utendaji mbovu, wizi, uwekezaji na usimamizi mbovu..., they are not necessarily the same; uwekezaji sio uhakika wa kuondoa wizi; na wala kushika wezi na kuwawajibisha hakuhitaji uwekezaji (If anything Serikali ndio inabidi ianze ku-perform)