Nimedokezwa: MOU 30 alizosaini Rais Dubai zikiwekwa hadharani, waTanganyika wote tutalala uchi barabarani

Nimedokezwa: MOU 30 alizosaini Rais Dubai zikiwekwa hadharani, waTanganyika wote tutalala uchi barabarani

Kunataarifa zindai kwamba kuna hati za maelewano zipatazo 30 zilisainiwa na Rais katika ziara yake ya Dubai.

Pia inadaiwa, huu mkataba wa Bandari ni moja tu kati ya vilivyomo kwenye maelewano hayo. Pia kuna sekta zingine kama posta nk.

Inasemekana kwamba, MOU hizo zote zikiwekwa wazi, basi waTanganyika wote mtalala uchi barabarani mkigalagala na kulia.

Ombi, MOU hizo zote 30 alizosaini, ziwekwe wazi.
hata ufiche wee kuna siku litafichuka tu. Mungu yupo.
 
Nini tofauti ya Agreement na mkataba?
Agreement ni makubaliano kwa kiswahili. Pia limetumika neno 'azimio' la makubaliano wakati suala la DP World linakwenda bungeni. Makubaliano yaliyofikiwa bungeni ndio yanayokwenda kutengeneza mikataba ya kibiashara.

Mkataba ni kile kinachozaliwa kutokana na makubaliano mara nyingi huwa ya mdomo. Katika kutunza kumbukumbu ndio pande mbili huandikiana yale wanayotaka yaongoze ufanyaji biashara yao.
 
Mkuu @paschalmayala una andiko lolote kuhusu hizi hekaheka za DP World?Naomba link kama umeandika
 
Daah, hatari, ila..

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

Tanganyika wazanzibar wanachukua Mali yetu kisa Cha muwekezaji jamani.
WHY WHY BANDARI ZA ZANZIBAR No. KUWA FAIDA WACHUKUE WAO TU YOTE HATA TANGANYIKA ISIPATE FAIDA YA 0TZS. HUKU MASIKINI WAKIUMIZWA NA KODI YA MIAMALA NA KILA SEHEMU IMEJAA KODI WHY HUYO ASEMEHEWE KODI HAMUONI KUWA HAO JAMAA WANAJILIPA KWENYE BANDARI KAMA WENGINE WALIVYOKWISHAJILIPA KWENYE UMEME, GESI NA MAFUTA WAO TU NDIO MADILA BASI PAMOJA NA SUKARI.

WATU MMELALA SIJUI MTAJUJA KUWAAMBIAJE WAJUKUU ZENU WATAKAPOKUWA HAWANA PA KWENDA NA KUTUMIKISHWA KAMA PUNDA NA HUKU WEWE UMESHIBA LEO PEKEE.

JAMANI ACHENI UOGA KIZAZI CHA AKINA NYERERE WALITESEKA SIE TUWE HURU WHY SIE TUNAKUWA WAOGA NA ASKARI ANAGANYA KAZI KAMA ROBOTI ANAUA MTU ANAYETETEA TAIFA KISA CHA AJIRA YAKE AMBAYO KWANZA INAMFANYA AWE MASIKINI.
ANGALIENI NCHI YETU IMESHAUZWA IMEISHA PORI TENGEFU, MADINI YAMEISHA YOTE WANAWAPA WATU KWA GAWIO LA SIRI KIVYAO NA SIO LA SERIKALI.

BAADAYE UNAKAMULIWA KODI MPAKA VIMA YAISHE.


YAANI HUJIULIZI UNALIPWA SALARY KODI, UKITOA HELA BANK KODI, UKIITUMA KODI, UKIITOA ULIYOTUMIWA KODI, UKINUNUA KITU KODI , YAANI KUNA KODI NYINGI MNO UNALIWA MPAKA UNAKUJA KUIPATA HELA YAKO.
HUKU WATU WAKIWAPA MA EX WAO GARI ZA 500M.
Endeleeni kusubiri hayo majibu
 
Mi nadhani napia sinauzoefu sana kuhusu hiyo mikataba kwa mna Dhani tatizo lilitokea wapi mpaka kufikika makubaliano ya kukabidhiana hizo lasilimali za in inchi pengine watu walijisahau wakaupiga mwingi wakamsahau mwenyewe jamani mina pitatu
 
Agreement ni makubaliano kwa kiswahili. Pia limetumika neno 'azimio' la makubaliano wakati suala la DP World linakwenda bungeni. Makubaliano yaliyofikiwa bungeni ndio yanayokwenda kutengeneza mikataba ya kibiashara.

Mkataba ni kile kinachozaliwa kutokana na makubaliano mara nyingi huwa ya mdomo. Katika kutunza kumbukumbu ndio pande mbili huandikiana yale wanayotaka yaongoze ufanyaji biashara yao.
Sijauliza ‘tafsiri’ ya neno ‘agreement’ , bali nimeomba tofauti ya maana ya neno ‘agreement’ na neno ‘mkataba’ , tofauti za hayo maneno mawili ni nini?

Kwamba mkataba huzaliwa baada ya makubaliano, na makubaliano huzaliwa baada ya nini? Yaani onyesha tofauti kwa criteria moja kwa maneno yote mawili
 
Kunataarifa zindai kwamba kuna hati za maelewano zipatazo 30 zilisainiwa na Rais katika ziara yake ya Dubai.

Piash inadaiwa, huu mkataba wa Bandari ni moja tu kati ya vilivyomo kwenye maelewano hayo. Pia kuna sekta zingine kama posta nk.

Inasemekana kwamba, MOU hizo zote zikiwekwa wazi, basi waTanganyika wote mtalala uchi barabarani mkigalagala na kulia.

Ombi, MOU hizo zote 30 alizosaini, ziwekwe wazi.
Sgr , tanesco ,ttcl
 
Walie tu? Mwenye wivu ajinyonge, bado yupo kwenye MoU wakati sasa hivi watu wapo kwenye mikataba kedekede na mingine ishaanza kazi. Jionee:

On 28, Tanzania’s Zanzibar and Oman Investment Authority signed a memorandum of understanding on Thursday to implement a port master plan on the Indian Ocean coastline of the archipelago. The agreement calls for the development of major ports in the coastal areas of Mangapwani and Bumbwini in the Zanzibar Islands.

f75c6c5fa093c7916415572b2365e63b.jpg


According to the memorandum, the two parties will cooperate to build a large modern port in Mangapwani, about 25 kilometers north of Malindi Port on San Island, for loading and unloading containers, general cargo, and oil and gas.

a749066a033b02dc2019bb93786da965.jpg


Mwini said that this is a major measure taken by the San government to develop the blue economy. It will develop San into a commercial and tourist center in East and Central Africa through the construction of necessary infrastructure in the future. He instructed Sang's relevant government departments to immediately conduct a feasibility study on this multi-billion-dollar project and make sure to make it a success. He also said that the Sang government will retain the plan of the previous government to build a new port in Mpiga Duri (about 3 kilometers north of Malindi Port) and build the port into a fishing port. The existing Malindi Port will be transformed into a special tourist port.Editor/Huang Lijun
Hizo ni picha tuuu , uhalisia inakuwa zero
 
Sijauliza ‘tafsiri’ ya neno ‘agreement’ , bali nimeomba tofauti ya maana ya neno ‘agreement’ na neno ‘mkataba’ , tofauti za hayo maneno mawili ni nini?

Kwamba mkataba huzaliwa baada ya makubaliano, na makubaliano huzaliwa baada ya nini? Yaani onyesha tofauti kwa criteria moja kwa maneno yote mawili
Agreement ni kile kilichokwenda bungeni na ni summary ya lengo zima la mikataba inayokwenda kusainiwa kati ya wazalendo na hao DPW.

Makubaliano ya DPW kati ya wanasheria wao na hawa wa kwetu yamechukua mwaka mzima kuweza kuandikwa.

Huwezi kuweka kila kitu kwenye makubaliano unachofanya ni kufupisha lengo zima la uwekezaji na huko kwenye mikataba ndio unakwenda kuweka kila kitu na mjadala wa kuandika mkataba unakuwa mrefu kuliko huo wa kupitisha azimio ndani ya bunge kwani huko ndio inakuwepo hatima nzima ya uchumi wa nchi kwa miaka mingi ijayo.

Huko ndiko kwenye ukomo, wanaosema mkataba hauna ukomo wanamaanisha makubaliano bila ya kujua, wanachokilenga ni hiyo mikataba ya kibiashara yenye ukomo kutegemea aina ya biashara zinazokwenda kufanyika.
 
Agreement ni kile kilichokwenda bungeni na ni summary ya lengo zima la mikataba inayokwenda kusainiwa kati ya wazalendo na hao DPW.

Makubaliano ya DPW kati ya wanasheria wao na hawa wa kwetu yamechukua mwaka mzima kuweza kuandikwa.

Huwezi kuweka kila kitu kwenye makubaliano unachofanya ni kufupisha lengo zima la uwekezaji na huko kwenye mikataba ndio unakwenda kuweka kila kitu na mjadala wa kuandika mkataba unakuwa mrefu kuliko huo wa kupitisha azimio ndani ya bunge kwani huko ndio inakuwepo hatima nzima ya uchumi wa nchi kwa miaka mingi ijayo.

Huko ndiko kwenye ukomo, wanaosema mkataba hauna ukomo wanamaanisha makubaliano bila ya kujua, wanachokilenga ni hiyo mikataba ya kibiashara yenye ukomo kutegemea aina ya biashara zinazokwenda kufanyika.
Kipi hasa kinafanya kilichopelekwa bungeni kiwe ‘Makubaliano’ , na hicho kinachokuja kuwa ‘mkataba’? What are the distinctive criteria between the two?

- Kwamba mkataba ukiandikwa kwa kifupi unabadilika na kuwa makubaliano?

- Kwamba mkataba ukichukua mwaka mzima kuandikwa unabadilika na kuwa makubaliano?

- Kwamba mkataba ukiwa haujawekwa kila kitu unabadilika na kuwa makubaliano?

- Kwamba mkataba wa pili ukiandikwa baada ya wa kwanza, ale wa kwanza unabadilika na kiwa makubaliano?
 
 
Back
Top Bottom