Nimefedheheka sana na kuamua kuzima Runinga. Yaani walimu wanatumika kisiasa kumpigia kampeni Rais Samia 2025! Huku wamejaa dhiki

Mpwayunga aondolewe Ban
 
Hii sio justification ya wao kutumika kisiasa. Acha upimbi.
Hili ndilo tatizo kubwa la watu wenye akili ndogo. Huwa mnapenda mawazo na mitazamo yenu kuungwa mkono, hata kama ni ya kipuuzi.

Ukiulizwa hao walimu waliojitokeza kwenye hayo maadhimisho, wanawakilisha asilimia ngapi ya walimu wote nchini, sidhani kama una jibu. Mnaleta dharau zenu za kipuuzi kwa watu ambao wanajiendeshea maisha yao wenyewe, huku nyinyi mkiishi kwa wazazi wenu! Too low.
 
Hongera sana kwa uungwana unaouonyesha. Unajua humu JF mi nilidhani watu wote wana akili na ni thinkers kumbe sivyo! Mtu anaanzaje kuwatukana Walimu namna hiyo? Watu ambao hawamnyanyasi wala kumuonea, na anaacha wanaomuone kila siku (mfano:traffic police barabarani)?

Halafu kesho na keshokutwa Walimu wakiona hawa wananchi wamezidi 'kuwananga' wakaamua kususa kuwasimamia ipasavyo watoto wa jamii (wanafunzi), tutakuwa na taifa la namna gani hatimaye? Leo taifa linalia watoto wanapandikizwa ushoga na usagaji wakiwa mashuleni, sasa badala ya jamii kuwatia moyo Walimu ili kuwe na makazo katika kwanusuru watoto na janga hilo na mengineyo, wanajitokeza wapuuzi fulani kutwa nzima wao ni kutukana Walimu tu. Na jitu la hivyo linaona ni ujanja kufanya hivyo.
 
Kuongoza nchi ya Tanzania ni kazi nyepesi mno, sababu wajinga tupo wengi kuliko werevu.
 
Dhana ya ualimu ni wito ndio matokeo yake hayo,hata penye kutaka haki unataka huruma ya wakuu,kwa TZ kuwa mwalimu ni adhabu kali,hauna tofaut na mtoto ambae hawez fany chochote mpaka mzaz aruhusu,BURE KABISA
 
Ndugu yangu, siyo walimu.
Ukisikia kuna Chama Cha Walimu (CWT) au Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) ni MAGENGE ya unyonyaji kwa Wafanyakazi.

TUCTA hawana lolote jipya zaidi ya kuungana na Serikali kwa lengo la kuwaumiza Wafanyakazi.
 
Dhana ya ualimu ni wito ndio matokeo yake hayo,hata penye kutaka haki unataka huruma ya wakuu,kwa TZ kuwa mwalimu ni adhabu kali,hauna tofaut na mtoto ambae hawez fany chochote mpaka mzaz aruhusu,BURE KABISA
Mmekazana na Walimu utadhani hii nchi kada nyingine zote zinajua kudai. Hivi juzi CAG ameibua ufisadi mkubwa uliofanywa na 'wakubwa' ndani ya Police Tanzania juu ya fedha za maafa wanazochangia mapoti, umeona kuna pot kasimamia kucha jambo hilo? Ingekuwa hizi hela ni za Walimu msingewatukana Walimu kweli?

By the way, kada nyingi tu hapa nchini mambo hayako OK. Hata kule jeshini kuna unyanyasaji wa maslahi, sema nidhamu ya kijeshi inawafanya wajeda wa-mute tu kisabuni, ila hayo hamuyaongelei.

Vipi Vyama vya Siasa vilivyonyimwa haki enzi za JPM vilifanya nini? Na wewe unaweza kufanya nini? au ndo kujitia ushujaa usionao? Umewahi kuingia barabarani lini kudai haki yako?
 
K
Kada nyingine za kitaaluma nazo zinalipwa kama wabunge Hadi ila mfano muwatolee Walimu tu?
 
Wewe ni mpuuzi mkubwa. Yaani hao sio wawakilishi wa walimu hapa Tanzania? Kuishi kwa wazazi sio hoja ya kutunyima uhuru wetu wa kujadili taifa letu. Wewe kenge.
 
Mungu huwa hakosei kwenye maamuzi yake😁😁😁 nilipomaliza kidato cha sita matokeo yangu hayakuwa mazuri nilipata daraja la nne maadui zangu walifurahi sana wakasema mwizukulu mgikuru ndio ameishaa hivyooo. Wenzangu waliofauru vizuri wakaenda kusoma wote ualimu na wakapata mkopo kwa asilimia 80. Mimi nikajipanga baada ya miaka kadhaa niikaenda kusoma kozi ya afya kwa ngazi ya diploma na leo nina furaha kuliko wale jamaa zangu😁
 
Wewe ni mpuuzi mkubwa. Yaani hao sio wawakilishi wa walimu hapa Tanzania? Kuishi kwa wazazi sio hoja ya kutunyima uhuru wetu wa kujadili taifa letu. Wewe kenge.

Badala ya kujibu maswali niliyokuuliza, unakimnilia kutukana!! Hili ndilo tatizo la kukulia kwenye malezi duni. Unajifanya mjuaji, kumbe kichwani hamna kitu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…