Nimefukuzwa kazi kisa kugoma kumfatia bosi vitumbua vya mia tisa

Nimefukuzwa kazi kisa kugoma kumfatia bosi vitumbua vya mia tisa

Haya mabo sio ya kuchekea hata siku moja

Na si afya kwa masilahi mapana ya taifa.

Kwa vigezo hivi wafanya kazi wa wahindi na waarabu wamejikuta wakigeuzwa nyuma kisa huu huu upuuuzi wa kumuona bosi ni Mungu
Yaani kufuata tu vitumbua ng'ambo ya barabara unaona umedhalirishwa? Kwani angefuata angepungukiwa nini? Ngoja sasa kaende mtaani kakakumbane na moto wa Hangaya!
 
Haya mabo sio ya kuchekea hata siku moja

Na si afya kwa masilahi mapana ya taifa.

Kwa vigezo hivi wafanya kazi wa wahindi na waarabu wamejikuta wakigeuzwa nyuma kisa huu huu upuuuzi wa kumuona bosi ni Mungu
unajiona umeandika point? acha ujinga wewe,kamtafutieni kazi mwenzenu sasa
 
Yaani kufuata tu vitumbua ng'ambo ya barabara unaona umedhalirishwa? Kwani angefuata angepungukiwa nini? Ngoja sasa kaende mtaani kakakumbane na moto wa Hangaya!
Ukijua maana na thamani ya utu ndio utajua ukubwa wa maamuzi ya mleta mada asee.

Kuna visa vingi vya namna hii na madhara yake huwa ni makubwa saana

Kuna dereva mmoja alikuwa anaendesha kosta la tajiri mmoja.
Sasa yeye ni dereva cha kushangaza yule bosi siku moja akamtuma kumpelekea nguo kwa dobi ila akaambiea asiende na gari kwa kuwa siku hiyo alikuwa ilikuwa mapumziko, jamaa akaenda
Siku iliyofuata bosi akamtuma maziwa sehemu aliyoweka bili jamaa akaenda
Sasa siku moja si akamtuma kwenda kumwaga takataka jamaa akaenda hapo huyo jamaa anafanya hivyo ili kulinda udereva wake
Kituko: siku moja amekuja kupaki mke wa bosi akamwita akamwambia paki ukimaliza uje ukamwage huu uchafu chooni mtoto kamaliza kujisaidia

Aseee jamaa alirudi kwenye gari akawasha na kulitoa mkuku akampitia mtoto wa bosi, mke wa bosi na gari ikaingia mpaka ndani na kumkuta bosi kapumzika kwa sofa nae kule na wooote wakawa wamepoteza uhai lakini dereva alifia hospitali kwa kauli moja tuu
Tufike sehemu ujue umemwajiri mtu kwa kazi gani.
 
Yaani kufuata tu vitumbua ng'ambo ya barabara unaona umedhalirishwa? Kwani angefuata angepungukiwa nini? Ngoja sasa kaende mtaani kakakumbane na moto wa Hangaya!
Ukijua maana na thamani ya utu ndio utajua ukubwa wa maamuzi ya mleta mada asee.

Kuna visa vingi vya namna hii na madhara yake huwa ni makubwa saana

Kuna dereva mmoja alikuwa anaendesha kosta la tajiri mmoja.
Sasa yeye ni dereva cha kushangaza yule bosi siku moja akamtuma kumpelekea nguo kwa dobi ila akaambiea asiende na gari kwa kuwa siku hiyo alikuwa ilikuwa mapumziko, jamaa akaenda
Siku iliyofuata bosi akamtuma maziwa sehemu aliyoweka bili jamaa akaenda
Sasa siku moja si akamtuma kwenda kumwaga takataka jamaa akaenda hapo huyo jamaa anafanya hivyo ili kulinda udereva wake
Kituko: siku moja amekuja kupaki mke wa bosi akamwita akamwambia paki ukimaliza uje ukamwage huu uchafu chooni mtoto kamaliza kujisaidia

Aseee jamaa alirudi kwenye gari akawasha na kulitoa mkuku akampitia mtoto wa bosi, mke wa bosi na gari ikaingia mpaka ndani na kumkuta bosi kapumzika kwa sofa nae kule na wooote wakawa wamepoteza uhai lakini dereva alifia hospitali kwa kauli moja tuu
Tufike sehemu ujue umemwajiri mtu kwa kazi gani.
 
Nilisomaga mtandaoni kuna ajali ya ndege ilitokeaga kama sio 2014! Kwa mujibu wa taarifa za kisanduku cheusi ndege ilidondoshwa kwa makusudi kwa sababu dakika chache sana kabla ya kudondoka ilisikika sauti ya mtu anayegonga kwa nguvu mlango kama mtu anayetaka kufunguliwa katika mlango wa chumba cha marubani.
Hii inaonesha aliyeiangusha ndege kwa makusudi ni rubani msaidizi na aliyekuwa anagonga ni rubani kwa sababu kuna sauti ilinaswa kabla ya hapo ilisikika rubani mkuu akimuaga msaidizi kwamba anaenda kujisaidia, hivyo msaidizi akaitumia hiyo fursa kujifungia na kuilazimisha ndege ishuke chini kwa nguvu na kusabisha ajali.

Ripoti zinasema kabla ya pale huyo jamaa alikuwa kama ana msongo wa mawazo na alikuwa anajitapa kuwa siku moja atakumbukwa kwa sababu atafanya tukio la kukumbukwa.
Alikuwa analalamika kuwa anatumikishwa na rubani kufanya kazi ambazo hakusomea.
Kuna siku alipigana makonde na rubani kisa aliambiwa ahesabu abiria akasema sio kazi yake, yeye amesomea kurusha ndege.
Nadhani upo kwenye kundi

Naomba link ya hii story
 
Nilisomaga mtandaoni kuna ajali ya ndege ilitokeaga kama sio 2014! Kwa mujibu wa taarifa za kisanduku cheusi ndege ilidondoshwa kwa makusudi kwa sababu dakika chache sana kabla ya kudondoka ilisikika sauti ya mtu anayegonga kwa nguvu mlango kama mtu anayetaka kufunguliwa katika mlango wa chumba cha marubani.
Hii inaonesha aliyeiangusha ndege kwa makusudi ni rubani msaidizi na aliyekuwa anagonga ni rubani kwa sababu kuna sauti ilinaswa kabla ya hapo ilisikika rubani mkuu akimuaga msaidizi kwamba anaenda kujisaidia, hivyo msaidizi akaitumia hiyo fursa kujifungia na kuilazimisha ndege ishuke chini kwa nguvu na kusabisha ajali.

Ripoti zinasema kabla ya pale huyo jamaa alikuwa kama ana msongo wa mawazo na alikuwa anajitapa kuwa siku moja atakumbukwa kwa sababu atafanya tukio la kukumbukwa.
Alikuwa analalamika kuwa anatumikishwa na rubani kufanya kazi ambazo hakusomea.
Kuna siku alipigana makonde na rubani kisa aliambiwa ahesabu abiria akasema sio kazi yake, yeye amesomea kurusha ndege.
Nadhani upo kwenye kundi

Hakuna kitu inaudhi kama pale unafanya kazi yako kwa weledi halafu mtu kwa mamlaka aliyonayo anakunyanyasa
 
Kwa akili yako nani alikuwa anakuwezesha kununua hizo nguo za kuulamba mkanda nje?

Kwa hiyo wewe ulitaka kumpanda kichwani bosi wako?

Wewe kustahili hata kuwa house girl!!!
Kwahiyo unaona sahihi kutumwa vitumbua...alafu ata Maboss wastaarabu wana namna ya kuagiza hata anaeagizwa anachukulia Kama kafanya msaada...ukute huyo fala alituma Kama anatuma mtoto
 
Naomba link ya hii story
Siwezi kukumbuka link ya story ya miaka 6 au saba iliyopita.
Tafuta taarifa za ajali ya ndege kwenye milima ya alpes iliua watu zaidi ya mia. Fuatilia taarifa za rubani msaidizi aliyekuwa na miaka chini ya 30 wakati huo matukio aliyofanya siku chache kabla ya ajali.
Mojawapo ni kutumwa na rubani mkuu kazi anazodai yeye hakusomea kama anavyolalamika mtoa mada kutumwa vitumbua 9 kitu ambacho hakusomea.
 
Wewe ulitaka usimamishwe kwa kosa gani labda, au unamchagulia bosi wako kosa la kukusimamisha kazi....
 
Vitu vingine n kutumia busara dawa jeur kibur

Hiyo busara itumike kwa nani? Mtuma vitumbua au mtumwa vitumbua?

Hivi ukiwa boss unaweza kufika officin ukamtuma officer wako vitumbua? Halafu ukamfukuza kazi sababu tuu hajaenda kukununulia vitumbua?

Huyu muafi kuna kitu hajasema Labda hiyo ilikua kati ya yale majukumu yake....

Au alikula vitumbua vya boss halafu akaambiwa akanunue vingine na yeye akagoma😂😂😂😂😂😂
 
Aya Sasa kaombe kazi kwa muuza vitumbua sasa,mda mwingine uishi Kwa kupotezea tu .Nikishajua Boss wangu ni wa aina gani wala hainisumbue mpe anachotaka mpotezee ,alewe sifa we mambo yako yaende .
 
Aaah achana nae mimi nakuunga mkono kwa huo msimamo Bora Hata angekuagiza vya buku, maana vya mia tisa afu uanze kusubiri na hio chenji sh mia, afu mtu umevaa tetroni yako na jua likuwakie ufe bure.
[emoji3][emoji16][emoji1787][emoji1787]
 
Habari zenu

Katika hali isiyo ya kawaida siku ya leo nimepewa rasmi barua ya kuachishwa kazi kwa kosa la utovu wa nidhamu

Shughuli ilianzia Alhamisi iliyopita mida ya saa tatu bosi aliniita ofisini na kuniagiza vitumbua vya mia tisa

Kwakweli kulingana na nilivyokuwa mimi mtu mzima nimevaa nimependeza, nimechana nywele vizuri na nimechomekea

Nilikuwa nimevaa yale mashati ya kuwaka waka yale ya tetroni na nimechomekea na kuvaa suruali ya kitambaa nimechomekea, kitendo cha bosi kuniagiza vitumbua vya mia tisa kwangu niliona kama ni fedheha kubwa sana.

Yaani mimi nitoke ofisisni niende nje eti nimeagizwa vitumbua? Nilimwambia bosi kuwa sitaweza kwenda maana nina kazi na niko bize.

Mimi nina mke na watoto uniagize vitumbua?

Ijumaa nilisimamaishwa kazi na leo rasmi nimeachishwa kazi

Hivi hii ni sawa kweli?
Kuachishwa kazi peke yake haikutosha, ilifaa uchapwe na viboko ukamuonyeshe mkeo!
 
Yu
Habari zenu

Katika hali isiyo ya kawaida siku ya leo nimepewa rasmi barua ya kuachishwa kazi kwa kosa la utovu wa nidhamu

Shughuli ilianzia Alhamisi iliyopita mida ya saa tatu bosi aliniita ofisini na kuniagiza vitumbua vya mia tisa

Kwakweli kulingana na nilivyokuwa mimi mtu mzima nimevaa nimependeza, nimechana nywele vizuri na nimechomekea

Nilikuwa nimevaa yale mashati ya kuwaka waka yale ya tetroni na nimechomekea na kuvaa suruali ya kitambaa nimechomekea, kitendo cha bosi kuniagiza vitumbua vya mia tisa kwangu niliona kama ni fedheha kubwa sana.

Yaani mimi nitoke ofisisni niende nje eti nimeagizwa vitumbua? Nilimwambia bosi kuwa sitaweza kwenda maana nina kazi na niko bize.

Mimi nina mke na watoto uniagize vitumbua?

Ijumaa nilisimamaishwa kazi na leo rasmi nimeachishwa kazi

Hivi hii ni sawa kwel
Bandika picha yako jinsi ulivyovaa siku hiyo hadi boss wako akamwacha sekretari wake akamuua kukutuma wewe huenda kuna external force.
 
Back
Top Bottom