Nimefuta Biblia kwenye simu yangu

Nimefuta Biblia kwenye simu yangu

Sasa nimeamini kuwa dini ni kwaajili ya maskini na waoga tu.

Mpaka leo hakuna mwanadamu au kitu chochote ikiwemo Mungu alitethibitisha kuwa Mungu yupo.

Kila mtu atakuthibitishia kwa maandiko ambayo yameandikwa kwa mkono wa mtu.

Ukiondoa maandiko hakuna mtu wa dini kukuthibitishia uwepo halisi wa Mungu.

Waislamu kwa kitabu chao watakuthibutishia uwepo wake, Wahindu, Wabudha, Waktisto n.k watakuthibutishia uwepo wa Mungu kwa maandiko na hadithi tu ila hawataweza kukuthibitishia kwa njia nyingine ya reality.

Kwa taabu wanazopata watu duniani ni kama nature ndio inatawala.

Haiwezekani Mungu ambaye wanasema aliupenda ulimwengu aruhusu vita, ubakaji, kuchinjana, kudhulumiana, ufukara, njaa n.k huku hivyo vitu ni vidogo kwake angevikomesha ndani ya sekunde.

Je, Mungu kazidiwa utu na upendo na mwanadamu?

Hii amani na hali ya maendeleo tunayoiona ni fikra na utu wa binadamu kwa ulimwengu.

Binadamu anaunda mabaraza ya kitaifa kupambana na majanga mbalimbali, pasipo na haya mabaraza Dunia isingekalika kabisa kwa idadi hii ya watu ilivyo kwa sasa.

Illusion ndizo zinatawala watu ndio maana kila dini na dhehebu wanajiona kuwa wako sahihi na wana ushahidi kuwa dhehebu lao ndilo sahihi mbele za Mungu na wao tu ndio wataingia mbinguni au peponi.
Wewe sio mkristu
 
Dadeki
Nje ya maandiko hawezi kukuthibitishia uwepo wa Mungu.
Hata afanye nini, hawezi
Nje ya hivyo vitabu vya uongo na propaganda hakuna mtu anaweza mthibitisha Mungu mfano chukua hicho
Biblia au Quran Halafu mtafute mhadzabe mmoja umpe akishike na akifunue uone kama kitamuongoza kumjua huyo Mungu namaana Gani kusema hivyo.

Mungu ilipaswa atambulike automatically Kwa watu bila watu kuaminisha watu Kwamba yupo kama mtoto anavyozaliwa hajui kitu ila anafundishwa ila Kuna vitu huwezi mfundisha ni nature kama kuhisi Njaa au kugusa moto atajua ni hatari bila hata kufundishwa na mtu
Huyo Mungu alishindwaje kutufanya kumjua direct bila hekaya za kiyahudi na kiarabu?
 
Sasa Bwana Ali imekuaje ukamiliki Biblia kwenye simu yako.
 
Na ww tuthibitishie kuwa Mungu hayupo

Au kwa urahis unadhan hivi vitu vyote unadhan mwanzo wake n nn??
Vilijitengeneza??
 
Wewe umetokana na manii na mungu akakufanya kuwa kiumbe hai ukakaa kwenye tumbo la mama yako miezi 9 akakupa akili na uwezo wa kukufanya mpaka unaandika hapa ujiulizi haya yote anayafanya nani.

Kuzunguka kwa jua, nyota zimejipanga kubadilika kwa majira sayari zimejipanga, kwenye mwili wako kila kiungo kimejipangalia ujiulizi nani anafanya? Hizo ndo ishara za mwenyezi mungu
 
Na ww tuthibitishie kuwa Mungu hayupo


Au kwa urahis unadhan hivi vitu vyote unadhan mwanzo wake n nn??
Vilijitengeneza??
Utadhibitishaje kitu ambacho hakipo kua hakipo Arif?
Halafu unaamini Ili vitu viwepo lazima kuwe na kitu kiwe kimetengeza haya nikuulize nani aliyemtengeneza aliyetengeneza vitu?
 
Dadeki
Nje ya maandiko hawezi kukuthibitishia uwepo wa Mungu.
Hata afanye nini, hawezi
Tena mwambie akimaliza utafiti wake atakufa tu na hajui anaenda wapi baada ya kifo chake ata akikesha maktaba kufanya uchunguzi wake
 
Wewe umetokana na manii na mungu akakufanya kuwa kiumbe hai ukakaa kwenye tumbo la mama yako miezi 9 akakupa akili na uwezo wa kukufanya mpaka unaandika hapa ujiulizi haya yote anayafanya nani
Kuzunguka kwa jua, nyota zimejipanga kubadilika kwa majira sayari zimejipanga, kwenye mwili wako kila kiungo kimejipangalia ujiulizi nani anafanya? Hizo ndo ishara za mwenyezi mungu
Hizo ni blabla tu haya nikuulize na wewe ni nani aliyetengeneza huyo Mungu na kumpa uwezo wa kutengeneza hivyo unavyodai ni Kazi yake Yaani Ulimwengu vitu vyote?
Maana kama unaamini binadamu aliumbwa lazima muumbaji ana muumbaji wake pia maana hiyo ndio kanuni ya maisha katika ulimwwngu wetu!
 
Tunakemea Mapepo na Kwa Jina La Yesu Kristo Mwokozi Wa Mwanadamu Yanatokaaaaaa!
 
Kila unalojaribu kwa kutokutukmia akili na unafeli umefikia hatua ya kusema hakuna Mungu..subir majawbu yake
 
Sasa nimeamini kuwa dini ni kwaajili ya maskini na waoga tu.

Mpaka leo hakuna mwanadamu au kitu chochote ikiwemo Mungu alitethibitisha kuwa Mungu yupo.

Kila mtu atakuthibitishia kwa maandiko ambayo yameandikwa kwa mkono wa mtu.

Ukiondoa maandiko hakuna mtu wa dini kukuthibitishia uwepo halisi wa Mungu.

Waislamu kwa kitabu chao watakuthibutishia uwepo wake, Wahindu, Wabudha, Waktisto n.k watakuthibutishia uwepo wa Mungu kwa maandiko na hadithi tu ila hawataweza kukuthibitishia kwa njia nyingine ya reality.

Kwa taabu wanazopata watu duniani ni kama nature ndio inatawala.

Haiwezekani Mungu ambaye wanasema aliupenda ulimwengu aruhusu vita, ubakaji, kuchinjana, kudhulumiana, ufukara, njaa n.k huku hivyo vitu ni vidogo kwake angevikomesha ndani ya sekunde.

Je, Mungu kazidiwa utu na upendo na mwanadamu?

Hii amani na hali ya maendeleo tunayoiona ni fikra na utu wa binadamu kwa ulimwengu.

Binadamu anaunda mabaraza ya kitaifa kupambana na majanga mbalimbali, pasipo na haya mabaraza Dunia isingekalika kabisa kwa idadi hii ya watu ilivyo kwa sasa.

Illusion ndizo zinatawala watu ndio maana kila dini na dhehebu wanajiona kuwa wako sahihi na wana ushahidi kuwa dhehebu lao ndilo sahihi mbele za Mungu na wao tu ndio wataingia mbinguni au peponi.
Mpumbavu husema hakuna Mungu, zab 13
 
  • Thanks
Reactions: ABJ
Waje hapa wathibitishe tuamini
Wewe ulisikia wapi hili suala la madai ya kuwepo Mungu lilitokana na uthibitisho hadi sasa ndio uone umekuja kugundua kuwa hakuna huo uthibitisho? Msingi wa madai ya kuwepo Mungu umejengwa kwenye imani hivyo ni suala la kuamua kuamini au kutokuamini na ndio maana unaona kuna madai ya dini/miungu mingi tu na kila mmoja anashikilia imani yake(mungu) kuwa ndio sahihi maana hivyo ndivyo anavyoona na ndio maana akakubali kuamini.

Sasa hayo ya kutokuwepo au sijui kushindwa kuthibitisha kuwepo kwa Mungu yanatoka wapi? kilichokusudiwa hapa ni kukubali kwako(imani) kuwepo kwa ambacho hukioni wala hukisikii(Mungu) hilo ndio lililokusudiwa hivyo si kwamba uthibitisho umekosekana. Maana huyo Mungu anayedaiwa kuwa muweza wa yote basi angetaka kuwa kila anayezaliwa lazima awe anamjua yeye basi nafikiri angefanya kila mtu azaliwe akiwa teyari anamjua huyo Mungu na hivyo kusingekuwa na mabishano ya kuwa yupo au hayupo lisingekuwa jambo la imani tena.
 
Umechelewa Sana kutambua Hilo mkuu,
Kwanza hongera kwa kujitambua
Pili nakazia
Mungu ni propaganda za zama za Giza
(Dark ages)
Kuamuni Kwamba Kuna Mungu muweza wa yote na muumbaji wa mbingu na ardhi ni Uwendawazimu
Ambao hata unishawishi Kwa kutumia maneno Gani siwezi kuukubali
Mungu,shetani,malaika,mizimu,majini &co ni fiction characters walobuniwa kama
Marvel movies walivyobuni nchi ya Wakanda na Azgard na kiuhalisia hakuna kitu kama hicho!
Kama ambavyo unaamini unaakili na hujawahi ziona nayo ni propaganda za zama za giza kaka uko sahihi usikubali mtu akuambie unaakili wewe huna akili ndugu wanakudanganya
 
Hizo ni blabla tu haya nikuulize na wewe ni nani aliyetengeneza huyo Mungu na kumpa uwezo wa kutengeneza hivyo unavyodai ni Kazi yake Yaani Ulimwengu vitu vyote?
Maana kama unaamini binadamu aliumbwa lazima muumbaji ana muumbaji wake pia maana hiyo ndio kanuni ya maisha katika ulimwwngu wetu!
Ijulikane au isijulikane huyo aliyemuumba Mungu,awepo au asiwepo ila hoja ya msingi hapo ni hilo dai la Mungu kuwa ndio mtengenezaji/muumbaji mfano huu ulimwengu.
 
Ijulikane au isijulikane huyo aliyemuumba Mungu,awepo au asiwepo ila hoja ya msingi hapo ni hilo dai la Mungu kuwa ndio mtengenezaji/muumbaji mfano huu ulimwengu.
hahahahah hii Kali Sasa Yale Yale ya Atake asitake tutamuongezea miaka Magufuli tutamlazimisha
unataka uyaaply hapa kwenye vitu seriously au sio?
😁😁😁
 
Back
Top Bottom