Nimeibiwa simu na mwizi ametoa pesa tiGO Pesa!

Nimeibiwa simu na mwizi ametoa pesa tiGO Pesa!

Ni Rahisi sana mtu akiweza kupata NIDA yako.Tigo wana huduma ya Kuweka Upya PIN kwa kutumia NIDA namba ambayo maswali yake wakala wao wa usajili anaweza kujibu na kufyatua Password yako Fasta.Nashauri TIGO waondoe hiyo huduma
Hili mawakala wote wanalijua. Mtu akipata namb yako ya nida anatoa hela mm nimepruv kwa macho yangu. Bidada kaenda kwa wakala na sim ya baba yake na katoa hela
 
Kuna kibaka mmoja, alikua akiiba tu simu cha kwanza ni kutoa hela iwe tigo iwe voda cha kwanza anafanya muamala.....

Sijui hata ni akili gani zinatumika.
Kun namna majina yako kamili yanampa nida. Na anatoa hela kabisa... hiki kitu kuna wakala wa tigo aliwah nisimulia inakuaje ila sijatilia umakini kumsikilizaga tu lakin wanatoa hela wezi wazoef
 
It is almost impossible.

Uliibiwa kwenye mazingira gani,

Inawezekana ulikua umelewa kabla ya kuipoteza simu.
 
Kuna kipindi serikali ilizitaka kampuni za simu kuweka PIN kwenye laini ili kulinda wateja,mfano ukinunua laini mpya inakuwa tayari na PIN,unabadilisha unaweka ya kwako,hiyo inakusaidia pale unapoibiwa simu au laini,mtu akitaka kuweka hiyo laini yako kwenye simu nyingine au kama simu yako ikazima, inamlazimu kuweka PIN ya laini...hii inazuia mwizi au mtu asiyehusika kutumia laini yako kama ukiibiwa au kupoteza bahati mbaya.... Halotel wanayo huduma hii kwenye laini zao mpya,ila Tigo na Vodacom bado laini zao hazina hiyo option.
Mimi line yangu ya voda inayo pin ukiwasha lazima uweke so voda wanayo option hii
 
Ni Rahisi sana mtu akiweza kupata NIDA yako.Tigo wana huduma ya Kuweka Upya PIN kwa kutumia NIDA namba ambayo maswali yake wakala wao wa usajili anaweza kujibu na kufyatua Password yako Fasta.Nashauri TIGO waondoe hiyo huduma
Aisee 😯
 
Bora tigo mimi ukinipa lain ya eatel yoyote na usinipe nida wala pin yako ya eatel money kama unapesa humo naitoa safi kabisa bila kusumbuka na hata ukienda polis watakwambia umetoa mwenyewe kiufupi kampun zetu za simu haziko security sana kwa wajanja
Mnatutisha wakuu, hizi akiba zetu tutahifadhi wapi sasa?
 
Tigo wana makosa.

Wafute mianya ya mwizi kupata access ya namba ya siri.

Kuna mdau hapo katoa mbinu rahisi tu ya kudukua hiyo namba ya siri tena ukisaidiea kwa 100% na hoahao tigo.
Hiyo huduma ipo ili kurahisha upatikanaji wa namba ya siri kwa walio sahau.

Pia laini ikikaa muda mrefu bila kutumika huwa wana reset namba ya siri automatic kwenda 0000
 
Hiyo mbona rahisi sana Cha kwanza anatoa line kama simu yako Ina password,anajipigia ,
Akishapata namba yako anaenda Kwa wakala wale wasajiri Laini anajifanya amesahau namba NIDA yake ,wale akiwapa namba yako tu wakicheki kwenye vile vifamoko vyao NIDA yako hiyo chap inakuja na majina yako yote matatu,

Baadae ya hapo anapigia tu Customer care na kuwaambia amesahau password yake ,wao wanachoomba ni namba za NIDA ,majina matatu na mwaka wa kuzaliwa ambao ni tayari upo Kwa namba ya NIDA yako ,
Baadae ya hapo anabadilishiwa password ye anaenda kutoa pesa yako Kwa Raha mustareheee.


Hiyo process yote kwa mwizi mzoefu haizidi ata Nusu saa .

Nb
Ukipotelewa na simu pigia customer care mapema wablock line yako kuepuka mambo kama hizi.
 
Sure ,kuguess password ni ngumu sana hasa hizi zenye 3 attempts hata ukiweka mwaka wa kuzaliwa ,hata mimi nikikwambia nimezaliwa kati ya mwaka 1952 hadi 1970 kuguess mara tatu hautoboi....Kuna loophole za ma agent/customer care na wezi kushirikiana.
Ndomana kuna boss wangu mmoja anakaukwasi fulani
Lkn mambo ya kuweka hela tigo,mpesa sjui atumie app za kibenki hataki kusikia
Mambo mengi anafanya benki mguu kwa mguu 😄

Ova
 
Hiyo huduma ipo ili kurahisha upatikanaji wa namba ya siri kwa walio sahau.

Pia laini ikikaa muda mrefu bila kutumika huwa wana reset namba ya siri automatic kwenda 0000
Ndo hapo tigo inabidi warekebishe, maana huo tayari ni mwanya wa kuibiwa kizembe tu.

Na maswali yao ya nida huwa ni mepesi kwa mtu anaekujua.
 
Sure ,kuguess password ni ngumu sana hasa hizi zenye 3 attempts hata ukiweka mwaka wa kuzaliwa ,hata mimi nikikwambia nimezaliwa kati ya mwaka 1952 hadi 1970 kuguess mara tatu hautoboi....Kuna loophole za ma agent/customer care na wezi kushirikiana.
Mtu anaibiwa sim,watu wanakwala hela kama ziko tigo pesa,wakitoka hapo line yako hyo hyo wanaikopea hela pia 😄

Ova
 
Back
Top Bottom