Nimepata mtoto wa kiume usiku huu, baada ya kuwa kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka 7

Nimepata mtoto wa kiume usiku huu, baada ya kuwa kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka 7

Tafiti nyingi sana zinaonyesha kwamba kiini au chanzo cha Migogoro mingi sana pamoja na vyanzo vya ugomvi au Mauaji kwa wanandoa wengi sana hapa duniani ni wivu wa mapenzi, kukosa uaminifu katika ndoa (infidelity) au Wanaume kubambikiwa watoto ambao kimsingi sio watoto wao halisi wa kuwazaa (not biological Fathers). Visa vingi sana vya Mauaji ya wanandoa hususani kwa akina mama na watoto wao huwa vinahusiana na suala la hili la Wanaume kubambikiwa watoto, mambo yanapokuja kujulikana hadharani wakati tayari mwanaume ameshaingia gharama kubwa katika malezi ya watoto ambao baadaye inakuja kuthibitika kuwa siyo wake matokeo yake huwa ni mabaya Sana kupita kiasi.
Hivyo basi, njia pekee ya kuweza kuepukana na dhahama au mabalaa kama hayo ya Mauaji kwa wanandoa ni kuchukua tahadhari kubwa katika hatua za mapema, yaani kuwapima DNA watoto wanaozaliwa, Kama matokeo yatakuja tofauti kabisa na matarajii, basi mwanaume atakuwa na nafasi ya kuweza kujiepusha na gharama zisizomhusu za malezi ya watoto ambao siyo wake. Aidha, mtoto husika ataweza kupata malezi kutoka kwa baba yake halisi. Na mwisho kabisa, kupima DNA Mapema pia itasaidia Wanandoa kuwaepusha na janga kubwa la Migogoro ya hatari kati yao ambayo mara nyingi sana husababisha madhara makubwa sana yasiyorekebishika ktk siku za usoni, ikiwamo na mifarakano mikubwa na Vifo.

Kinga ni Bora kuliko Tiba, Kupanga ni Kuchagua!
The choice is yours.
Kiongozi mbona inaonekana kama una busara ila tu unajichetua!??

Ushawahi siku Moja kumshauri baba yako afanye hivo kwako au Kwa ndugu zako??

Hivi unahisi hakuna namna nyingine ya wewe mwanaume kuhakiki hili jambo Kwa mazingira??

Mim binafsi Nina uhakika mkubwa saana juu ya hili.

Nilichukua tahadhari mapema na nilimwambia mwenyewe kuhusu hili kutokana na changamoto tuliyoipata

Uhakika nizaidi ya hiyo DNA
 
Nakushauri upime DNA ili kujihakikishia umiliki w huyo mgeni mpya aliyewasili hapa duniani leo hii.
Kipimo Cha furaha uliyonayo leo hii itakuwa sawa sawa na kipimo Cha huzuni utakayopata wakati utakapokuja kugundua kwamba kumbe wewe ni baba mlezi tu wa huyo mgeni mpya aliyewasili.

Kwa leo sitaweza kukupongeza kwa ugeni wako huo hadi hapo baadaye nitakapopata majibu ya uhakika ya DNA Test kuhusu huyo mgeni wako.

Kwenye ndoa zenu kuna watoto wetu.
Huo uchokozi
 
Nakushauri upime DNA ili kujihakikishia umiliki wa huyo mgeni mpya aliyewasili hapa duniani leo hii.
Kipimo Cha furaha uliyonayo leo hii itakuwa sawa sawa na kipimo Cha huzuni utakayopata wakati utakapokuja kugundua kwamba kumbe wewe ni baba mlezi tu wa huyo mgeni mpya aliyewasili.

Kwa leo sitaweza kukupongeza kwa ugeni wako huo hadi hapo baadaye nitakapopata majibu ya uhakika ya DNA Test kuhusu huyo mgeni wako.
Ramli chonganishi. Muache huyo bwana usimharibie siku yake
 

Kuna msemo wa kiarabu usemao "inna baada Sabri, bushraa" yaani hakika Kila baada ya subra ni habari njema.

Hakika ndo ninavoweza kusema baada ya kuishi na mke wangu Kwa zaidi ya miaka 7 bila mtoto.

Hatimae Leo tarehe 27.07.2024 naandika historia mpya na njema katika mgongo wa ardhi hii ya dunia kwakuwa na mtoto wakiume.

Haikuwa rahisi ila kwakuwa nilimwachia mungu, naamin Leo ameamua kunijibu.

Hakika subra ni dawa na ponyo tosha Kwa wanaadamu.

Baada ya miaka mingi ya majuto na machozi Kwa mke wangu hatimae Leo amemuona mwanae mwenyewe.

Nashukuru mungu nami alinipa subra na uvumilivu wakuamini kuwa ipo siku tutapata mtoto.

Asikuambie mtu ni mtihani mkubwa saana kuwa kwenye ndoa na ukakosa mtoto Kwa muda mrefu.

Mungu alinipa maneno ya kumfariji Kila nilipomuona mke wangu analia.

Hakika nilikuwa mnyonge saana, ila usiku wa Leo mwanangu amenipa nguvu kubwa saana.

Amefuta Kila aina ya huzuni na kufanya nisahau Kila uchungu niliowahi kuwa nao.

Mungu nitunzie mwanangu, nitafanya Kila niwezalo huyu mtoto aishi Kwa furaha.

Hata kama nikiondoka Leo katika dunia hii najua kuwa nimeacha mtoto.

Tafadhali, nakuomba mungu usinicheleweshee na ndugu zake.

Mungu wape subra na uwafanyie wepesi wale wote wanaopitia katika mtihani huu, hakika wewe ndo mjuzi wa Kila kitu. Kwako halicheleweshwi jambo isipokuwa pale utakapo.

Hakika wamesubiri basi wape shufaa nao waone kizazi Chao.

Ameeeen!​
Hongera na kwa Kuzaliwa Kwake tu huko tarehe hiyo 27 kama ya GENTAMYCINE tegemea Mwanao kuwa na Nyota kali.
 
Mkuu nami naungana na wengine kukupa hongera
Nikijaribu kuvaa viatu vyako,furaha yako naiona. Hongera sana na Muombe Mungu akukuzie mwanao katika nyanja zote zaidi kimo akili na maarifa
 
Nakushauri upime DNA ili kujihakikishia umiliki wa huyo mgeni mpya aliyewasili hapa duniani leo hii.
Kipimo Cha furaha uliyonayo leo hii itakuwa sawa sawa na kipimo Cha huzuni utakayopata wakati utakapokuja kugundua kwamba kumbe wewe ni baba mlezi tu wa huyo mgeni mpya aliyewasili.

Kwa leo sitaweza kukupongeza kwa ugeni wako huo hadi hapo baadaye nitakapopata majibu ya uhakika ya DNA Test kuhusu huyo mgeni wako.
Huu ni upuuzi mkubwa,,,kama ingekuwa hivyo je,huyu mwanamke angesubir miaka yote hiyo?

Wakati mimi ndani ya miaka hiyo nilikuwa na wawili

Tuache kuwakosesha furaha watu kwa mitazamo ya kipuuzi
 
mshukuru Mungu wa kweli, usimshukuru huyo mungu wa kiarabu. pia, subiri akue, sitaki kukukatisha tamaa. punguza munkari. sitaki kufafanua zaidi ya hapo ila mshukuru Mungu kwa ajili ya mkeo pia.
Huyu naye ni mpuuzi mmoja,,,kuna mungu wa kiarabu?
 
Tumshukuru Mungu kwa kukupa furaha ya moyo wako, nakupongeza kwa uvumilivu ulionao wewe na familia yako. Mungu ni mwema sana na humjalia mja wake kwa wakati.
Ila Acha hayo mengine ya kupima sijui nini, mtoto ni wako. Acha kuiga wala kufuata hayo maneno. Endelea kufurahia upendo
 

Kuna msemo wa kiarabu usemao "inna baada Sabri, bushraa" yaani hakika Kila baada ya subra ni habari njema.

Hakika ndo ninavoweza kusema baada ya kuishi na mke wangu Kwa zaidi ya miaka 7 bila mtoto.

Hatimae Leo tarehe 27.07.2024 naandika historia mpya na njema katika mgongo wa ardhi hii ya dunia kwakuwa na mtoto wakiume.

Haikuwa rahisi ila kwakuwa nilimwachia mungu, naamin Leo ameamua kunijibu.

Hakika subra ni dawa na ponyo tosha Kwa wanaadamu.

Baada ya miaka mingi ya majuto na machozi Kwa mke wangu hatimae Leo amemuona mwanae mwenyewe.

Nashukuru mungu nami alinipa subra na uvumilivu wakuamini kuwa ipo siku tutapata mtoto.

Asikuambie mtu ni mtihani mkubwa saana kuwa kwenye ndoa na ukakosa mtoto Kwa muda mrefu.

Mungu alinipa maneno ya kumfariji Kila nilipomuona mke wangu analia.

Hakika nilikuwa mnyonge saana, ila usiku wa Leo mwanangu amenipa nguvu kubwa saana.

Amefuta Kila aina ya huzuni na kufanya nisahau Kila uchungu niliowahi kuwa nao.

Mungu nitunzie mwanangu, nitafanya Kila niwezalo huyu mtoto aishi Kwa furaha.

Hata kama nikiondoka Leo katika dunia hii najua kuwa nimeacha mtoto.

Tafadhali, nakuomba mungu usinicheleweshee na ndugu zake.

Mungu wape subra na uwafanyie wepesi wale wote wanaopitia katika mtihani huu, hakika wewe ndo mjuzi wa Kila kitu. Kwako halicheleweshwi jambo isipokuwa pale utakapo.

Hakika wamesubiri basi wape shufaa nao waone kizazi Chao.

Ameeeen!​
Wa kwako..??
 
Najua namna gani ulivyo na furaha. Mungu aizidishe furaha yako mara dufu.

Ndugu yangu alisubiri miaka 8 bila ya mtoto. Can u imagine? Tena wote wakiwa na afya njema bila tatizo lolote. Kila kitu kipo sawa, ila mimba haikamati.

Kila upande ukaanza kuinyooshea kidole upande mwingine. Upande wa mume (sisi) tukaanza kusema ndugu yetu hana shida. Tufanye mpango *mke wa pili.

Upande wa mke unamuasa ndugu yao, agawe uroda kwa wanaume wengine. Wamfungulie jamaa njia 🤣🤣🤣. Duh!
.
Tafrani tupu. Maneno mengi sana. Lakini wenza wale waliamua kusubiri. Waliamua kuupa muda uamue.

Baada ya miaka nane ya msoto, hatimaye wakabarikiwa kupata mtoto wa kike, mrembo kweli kweli. Mchangamfu na mjanja sana. Huna haja ya kuulizia kama ni wa babaye, unahitimisha tu.

Bahati ilikuwa kwao. Walioana wangali vijana. Sasa wana watoto watano wenye furaha kubwa.

Usikilize maneno ya watu. Hawajui mateso uliyopitia. Furahia na umshukuru Mungu. Mrejeshee sifa na utukufu. Binadamu hawa wanaokutia wasiwasi ndiyo wale waliokuwa wanakusimanga wewe na mkeo. Kisa mmeshindwa hata kupata mtoto mmoja.

Leo wanaibuka na kukutia hofu, ili uendelee kuishi kwa wasiwasi. Binadamu hajawahi kueleweka.

Kila la kheri.
Asante sana,,,uishi maisha marefu
 
Back
Top Bottom