1 Mungu akanena maneno haya yote akasema,
Kutoka 20:1
2 Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.
Kutoka 20:2
3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
Kutoka 20:3
4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
Kutoka 20:4
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Kutoka 20:5
6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.
Kutoka 20:6
7 Usilitaje bure jina la Bwana, Mungu wako, maana Bwana hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.
Kutoka 20:7
8 Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.
Kutoka 20:8
9 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;
Kutoka 20:9
10 lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.
Kutoka 20:10
11 Maana, kwa siku sita Bwana alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo Bwana akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.
Kutoka 20:11
12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.
Kutoka 20:12
13 Usiue.
Kutoka 20:13
14 Usizini.
Kutoka 20:14
15 Usiibe.
Kutoka 20:15
16 Usimshuhudie jirani yako uongo.
Kutoka 20:16
17 Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako.
Kutoka 20:17
Sent from my SM-A315F using
JamiiForums mobile app