Nimesikitika baada ya kuona Nigeria ina GDP karibu mara tano ya Tanzania

Nimesikitika baada ya kuona Nigeria ina GDP karibu mara tano ya Tanzania

Kumbe nchi yetu imezidiwa kiasi hiki na nchi yenye boko haram? Yaani kweli wao wanakaribia gdp ya bilioni 400 usd wakati sisi tupo kwenye bilioni 80s usd?
Kinachokusikitisha ni nini? 60% ya Uchumi wao unategemea Mafuta na hao ndio Wanaongoza Kwa mafuta Afrika unategemea nini?

Unadhani wangekuwa wanategemea mahindi na migomba na Madini ya kubahatisha bahatisha Kwa idadi Ile ya watu wangekuaje?

Mwisho mlaumuni Baba yenu wa Taifa Kwa ujamaa wake wa miaka 25 ambao hakuna Cha maana ulisaidia as far as economy is concerned.
 
Kwenye uchumi huwa wanalingaisha nchi zinazoendana...huwezi lingaisha Tanzania na marekani au nakuwait....popoluation it's matter kwenye GDP ndio maana mwisho wa siku Kuna kitu kinaitwa GDP PER CAPITA yaani wanagawa hiyo GDP Kwa popoluation. ..
Sasa kama ni hivyo aliyelinganisha Tanzania na Nigeria alitumia vigezo gani? GDP ni pato la taifa. Pato zima la taifa ni matokeo ya kodi, mikopo, grants utalii na kila kitu. Hii haitegemei sana population bali uwekezaji katika nchi husika. Ndio maana Israel inatuzidi GDP licha ya kuwazidi population.
 
Kinachokusikitisha ni nini? 60% ya Uchumi wao unategemea Mafuta na hao ndio Wanaongoza Kwa mafuta Afrika unategemea nini?

Unadhani wangekuwa wanategemea mahindi na migomba na Madini ya kubahatisha bahatisha Kwa idadi Ile ya watu wangekuaje?

Mwisho mlaumuni Baba yenu wa Taifa Kwa ujamaa wake wa miaka 25 ambao hakuna Cha maana ulisaidia as far as economy is concerned.
Kila siku 'alaumiwe Nyerere kwa kuharibu uchumi na sera mbovu ya Ujamaa'. Haya nyinyi aliowaachia nchi mmefanya lipi la maana hadi sasa?

Ndo maana hata nchi zilizoendelea ninatunanga tuache kulia lia eti Ukoloni umetusababishia umasikini. Sasa mko huru na bado hamuendelei.
 
Kila siku 'alaumiwe Nyerere kwa kuharibu uchumi na sera mbovu ya Ujamaa'. Haya nyinyi aliowaachia nchi mmefanya lipi la maana hadi sasa?

Ndo maana hata nchi zilizoendelea ninatunanga tuache kulia lia eti Ukoloni umetusababishia umasikini. Sasa mko huru na bado hamuendelei.
Msingi uliharibiwa kwahiyo nyumba haitakuwa imara.
 
Kila siku 'alaumiwe Nyerere kwa kuharibu uchumi na sera mbovu ya Ujamaa'. Haya nyinyi aliowaachia nchi mmefanya lipi la maana hadi sasa?

Ndo maana hata nchi zilizoendelea ninatunanga tuache kulia lia eti Ukoloni umetusababishia umasikini. Sasa mko huru na bado hamuendelei.
Msingi mbovu unaleta ugumu kwenye muendelezo maana hakuna kazi ngumu kama ya kubadili fikra za watu waliozoea rojo.mfano mzuri ni sera za Mwendazake Bado watu wanahusudu ujamaa.

Kwa hiyo kama Nchi tutakuwa tunaenda mbele na kurudi nyuma kulingana na milengo ya siasa.

Hata hivyo tukijitahidi kufikia growth rate ya 7% Kwa miaka 10 mfululizo tunaweza mshusha Kenya na Angola ila kuizidi South Africa haitakuja kutokea kamwe.
 
Hauko sahihi. High population sio kigezo cha GDP, bali ni uimara wa uchumi wa nchi.
Kwanini Qatar inaizi GDP Tanzania? Je, nao wana population kubwa kuliko Tanzania?
Unabisha nini Sasa Mzee? Kulisha population kubwa kama hiyo unadhani wanahitaji uzalishaji kiasi gani? Automatically tuu GDP itakuwa kubwa.

Pili idadi hiyo ya watu inakuhakikiahia soko ambalo ndio kitu Cha muhimu kabisa
 
Moja ya changamoto ya GDP haileflect uhalisia wa maisha ..ndio maana huku kwetu tuna lugha maarufu UCHUMI WA KWENYE MAKARATASI yaani BOT inatwambia UCHUMI umekua lakini maisha ya wananchi bado Duni..maana sekta nyingi zinazolisha Pato kwa wingi hazitokani na wananchi walio wengi Mfano madini etc...so unapojumlisha mapato yote then ukagawa Kwa popoluation haileflect uhalisia..ndio nachomaanisha.
Swala hapa sio ku reflect uhalisia wa Maisha Bali size ya uchumi ambayo inapimwa Kwa GDP.
 
Sisi huwa ni makelele tu kila kukicha ila hamna kitu.
Wewe na mtoa mada mna matatizo makubwa sana.

Uache kushangaa Kenya,Angola na Ethiopia kutuzidi uje kushangaa Nchi yenye Uchumi mkubwa Afrika kutuzidi?

On top of that Nigeria ndio inaongoza Afrika Kwa mafuta Sasa hapo kipi Cha kushangaza maana wanatuzidi Kwa Kila kitu kuanzia Utajiri wa rasilimali Hadi idadi ya watu na Ukubwa wa Nchi.
 
Msingi mbovu unaleta ugumu kwenye muendelezo maana hakuna kazi ngumu kama ya kubadili fikra za watu waliozoea rojo.mfano mzuri ni sera za Mwendazake Bado watu wanahusudu ujamaa.

Kwa hiyo kama Nchi tutakuwa tunaenda mbele na kurudi nyuma kulingana na milengo ya siasa.

Hata hivyo tukijitahidi kufikia growth rate ya 7% Kwa miaka 10 mfululizo tunaweza mshusha Kenya na Angola ila kuizidi South Africa haitakuja kutokea kamwe.
Wewe uko tayari kumlaumu baba yako mzazi kwa failures zako mwenyewe, kwamba Mzee hakukuandaa vyema kwa changamoto za maisha.

Yafaa sisi kama taifa kuangalia hali ya sasa na kuweka bidii badala ya kumlaumu sijui Nyerere alifanya nini nini. Mbona China walipoona Mao Tse-Tung economic policies zake hazikufanya vyema, waliochukua kijiti kwake (Deng Xiaoping na wenzake) warekebisha dosari na kusonga mbele? Nyinyi mnafeli wapi? Kila siku kuzunguka mbuyu tu.
 
Kumbe nchi yetu imezidiwa kiasi hiki na nchi yenye boko haram? Yaani kweli wao wanakaribia gdp ya bilioni 400 usd wakati sisi tupo kwenye bilioni 80s usd?
Kanuni muhimu ya kulinganisha ni kulinganisha vinavyolinganishika.

Yani, linganisha machungwa na machungwa, matufaa na matufaa.

Usilinganishe machungwa na matufaa.

GDP ni hesabu inayoweza kukupotosha.

Kwa sababu, haiangalii mgawanyo wa watu.

Ni hivi, ukiwa na nyumba A yenye watu 10, na kipato cha shilingi milioni 10, halafu ukawa na nyumba B ya mtu mmoja, mwenye kipato cha shilingi milioni tano, utasema hiyo nyumba A yenye watu kumi na kipato cha shilingi milioni 10 imeizidi uchumi nyumba yenye mtu mmoja na kipato cha shilingi milioni tano?

Huoni kwamba ukifanya hesabu hapo ukagawanya utapata nyumba A kwa wastani kila mtu ana kipato cha shilingi milioni moja, wakati nyumba B mtu mmoja ana kipato cha wastani cha shilingi milioni tano?

Ni bora uongelee GDP per capita, ambayo inachukua GDP na kuigawanya kwa idadi ya watu, ukapata kila mtu ana GDP per capita gani.

Nigeria ina watu zaidi ya milioni 215, Tanzania haijafikisha hata watu milioni 65. Maana yake unaweza kuzijumlisha Tanzania tatu kwa idadi ya watu, na bado usiifikie idadi ya watu wa Nigeria.

Unaweza kujumlisha idadi za watu wa Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia na Sudani ya Kusini, na bado usiifikie idadi ya watu ya Nigeria.

Sasa hapo unaona kuzilinganisha nchi mbili hizi kwa GDP tu ni sawa?
 
Kumbe nchi yetu imezidiwa kiasi hiki na nchi yenye boko haram? Yaani kweli wao wanakaribia gdp ya bilioni 400 usd wakati sisi tupo kwenye bilioni 80s usd?
Hujajua uchumi bado, Nigeria wnatuzidi kwa GDP kwa sababu wana idadi kubwa ya watu karibia milioni 300, ila kwa maendeleo ni shithole country kama TZ tu,
 
Nigerians wanapotoka kwenda kuishi mataifa ya nje wanakuwa bado wanatambulika kama raia wa Nigeria na mapato wanayopata huko nje (remittance)inakuwa ni sehemu ya pato la ndani. Sababu kuna uwekezaji mkubwa sana kupitia pesa nje.

Nigerians wanapambana sana kama taifa hawana giliba za roho za korosho kama sisi. Tunapenda sana kurudishana nyuma.

Mtu akiona una hela anataka mgao hajui zimetoka wapi, zinakwenda wapi, hazimhusu yeye anachojua ni anataka fungu la sehemu ya hizo pesa. Takataka kabisa.
 
Sisi tuna population kubwa kuzidi Kenya,Rwanda na Zambia,vipi umuhimu wa population hapo?
Shida uongozi,watu wanaiba hadi wanaanza kuzozana bungeni.
Kwenye uchumi huwa wanalingaisha nchi zinazoendana...huwezi lingaisha Tanzania na marekani au nakuwait....popoluation it's matter kwenye GDP ndio maana mwisho wa siku Kuna kitu kinaitwa GDP PER CAPITA yaani wanagawa hiyo GDP Kwa popoluation. ..
 
Back
Top Bottom