Nimesikitika baada ya kuona Nigeria ina GDP karibu mara tano ya Tanzania

Nimesikitika baada ya kuona Nigeria ina GDP karibu mara tano ya Tanzania

Kinachokusikitisha ni nini? 60% ya Uchumi wao unategemea Mafuta na hao ndio Wanaongoza Kwa mafuta Afrika unategemea nini?

Unadhani wangekuwa wanategemea mahindi na migomba na Madini ya kubahatisha bahatisha Kwa idadi Ile ya watu wangekuaje?

Mwisho mlaumuni Baba yenu wa Taifa Kwa ujamaa wake wa miaka 25 ambao hakuna Cha maana ulisaidia as far as economy is concerned.
Singapore,Israel, Switzerland, Taiwan, Luxembourg, Korea Kusini na Japan wametuzidi.
 
Wapo milioni 220 Nigeria, kumbuka kuwa wingi wa watu ni mtaji tosha.
Canada wako milioni 40, Korea Kusini million 50, Finland milioni 5 na yote haya ni mataifa bora sana

Pakistan wako milioni 230, Bangladesh millioni 170, Ethiopia milioni 120, DRC milioni 100 na yote haya ni mataifa ya hovyo tu.
 
Unabisha nini Sasa Mzee? Kulisha population kubwa kama hiyo unadhani wanahitaji uzalishaji kiasi gani? Automatically tuu GDP itakuwa kubwa.

Pili idadi hiyo ya watu inakuhakikiahia soko ambalo ndio kitu Cha muhimu kabisa
Haijawa automatically kubwa kwa DRC na Ethiopia.
 
Swala hapa sio ku reflect uhalisia wa Maisha Bali size ya uchumi ambayo inapimwa Kwa GDP.
South Korea, Ujerumani, Finland, Netherlands, Norway, Denmark na Canada zina uchumi mkubwa hadi kuwa donor countries zikiwa na population ndogo.
 
Singapore, Canada na Korea Kusini waliotuzidi kwa mbali sana walimuibia nani??
Canada unauliza tena? Huelewi kuwa Canada mpaka leo hii ni nchi ya wahamiaji? Kama ilivyo USA na Australia. Hata Singapore ni nchi ya wahamiaji.

Korea Kusini ni vibaraka wa USA, makampuni makubwa yote huko yanamilikiwa kwa asilimia kubwa na USA.
 
Singapore,Israel, Switzerland, Taiwan, Luxembourg, Korea Kusini na Japan wametuzidi.
Hao Wametuzidi eneo la Teknolojia na ujuzi na maarifa Kwa rasilimali watu.

Nigeria inategemea rasilimali za Asili ambazo ni mafuta ndio Wametuzidi.
 
South Korea, Ujerumani, Finland, Netherlands, Norway, Denmark na Canada zina uchumi mkubwa hadi kuwa donor countries zikiwa na population ndogo.
Acha kukurupuka.

Germany & South Korea wana popn kubwa kuzidi Tanzania na Wametuzidi Uchumi.

Ukitoa Finland Nchi zilizosalia hapo ni Tajiri mkubwa wa gas na mafuta plus teknolojia na Skilled Labor

Harafu acha kulinganisha Nchi za Wazungu na Africa
 
Ukubwa wa DRC na population yake ni very sparsely populated

Ethiopia imetuzidi GDP na push Yao kubwa na population
Urusi wako milioni 144 na ndio nchi kubwa zaidi duniani, Canada wako milioni 40 na nchi kubwa karibia mara 5 ya DRC.
 
Canada unauliza tena? Huelewi kuwa Canada mpaka leo hii ni nchi ya wahamiaji? Kama ilivyo USA na Australia. Hata Singapore ni nchi ya wahamiaji.

Korea Kusini ni vibaraka wa USA, makampuni makubwa yote huko yanamilikiwa kwa asilimia kubwa na USA.
Hata Haiti, Jamaica, Honduras, Bolivia , El Salvador na Nicaragua ni nchi za wahamiaji.
 
Wala usisikitike mkuu, wizi na upumbavu ndio unatuweka kwenye kundi la masikini yaani hata wanyama wana milo mitatu

Nigeria wana export bidhaa nyingi sana na wana crude oil, wana mafuta na gas wanauza nje pia wana vyakula kibao wanauza nje mpaka cocoa
Sasa sisi wanaona bora mkulima wa machungwa wa Muheza aweke barabarani kama mlima na kusubiri mabasi yapite auze na mengine kuozea hapo ila hamuwezi kuleta hata Ulaya au Uarabuni

Halafu kuna watu wanauliza eti nani katuroga
Nani awaroge wakati kuna viongozi wanaona umasikini wenu ndio mtaji wao
 
Shida yetu ni zaidi ya uongozi, tuache kulaumu uongozi tu.

Nakubaliana nawe. Naelewa "Noblesse Oblige". Waliopewa talanta nyingi zaidi watadaiwa marejesho mengi zaidi, hata mwanafalsafa Yesu alituambia hili katika mfano wake.

Uongozi una lawama kubwa kabisa na za awali kabisa. Hilo halina ubishi. Lakini, uongozi haujiweki wenyewe. Watu wanaoongozwa pia wana sehemu ya lawama kwa kujiruhusu kuwa na uongozi huu. People get the leadership they deserve. Else they remove that leadership and put one that they deserve.

Kwa kila rais mmoja anayeiba kura, kuna maelfu na maelfu ya wasimamizi wa uchaguzi mpaka majaji walio katika tume ya uchaguzi wanaoshiriki wizi huu.

Kuna wananchi mamilioni wanaoona wanaibiwa kura lakini wanakubali kikondoo na kusema hewala heeala tu.

Kuhusu wingi wa watu;

Wingi wa watu kama hujajipanga kuwatumia hao watu kuzalisha ni tatizo.

Kwa maana utakuwa na watu wengi wa kuwalisha nankuwahudumia wakati hawazalishi.

Bongo watu wanamaliza chuo na kukaa miaka mitano mpaka kumi wanatafuta kazi. Yani hapo hata mtu akipata kazi, usomi ushapotea anabaki kuwa Mmachinga tu.

Sasa hapo wingi wa watu utasaidia nini?

Pia, kusema Tanzania tunawazidi Kenya kwa wingi wa watu , obviously Tanzania ni nchi kubwa, so kuongelea wingi wa watu tu unarudi kule kule kwenye kuongelea GDP.

What is the population density? What about arable land? How many people are employed? How many are in disguised unemployment? How many are productive (population minus children, the eledery, the infirm)

Unaweza kuwa na nchi ina watu wachache, lakini ina wazalishaji wengi na watoto/wazee/wagonjwa wachache, na unaweza kuwa na nchi ina watu wengi, lakini wqzalishaji wachache, wengi ni watoto/wazee/ wagonjwa.

So, wingi wa watu tu hautuoneshi kitu specifically hata kama unaweza kuwa indicator in similar countries under ceteris paribus.
Umenena vzr mkuu
 
Utajiri wa kweli sio rasilimali bali ni akili. Uingereza haina rasilimali yoyote lakini ilitawala dunia. Leo hii pale Israel kuna rasilimali gani?

Kule Bahamas wanategemea fukwe ambazo ni kilomita chache sana ukifananisha na tulizo nazo na wanaingiza mapato mara tano zaidi yetu.
Tatizo kwetu mpaka mwizi wa mabilioni amuombe tajiri mmoja awekeze kwenye fukwe au ajenge mahoteli ya kifahari nae akiwa mfadhili wa kujificha maana ni mwizi

Sasa unategemea nani atakubali kuzipokea hizo hela huku akijua kesho anaweza kugeukwa na huyo huyo mwizi atapofukuzwa kazi

Africa nchi nyingi ni magumashi hatutaki kufuata utaratibu wa haki
Ukiomba wewe hupati na utaambiwa una hela wewe

Ila roho mbaya wameona wale waliojenga vibanda kama mazizi ya mbuzi kwa miaka 30 wawaondoe leo na utakuta kuna jizi linawekeza
 
Back
Top Bottom