Nimwombe Rais Samia awaondoe haraka wanajeshi wetu kule DRC Congo. Mnapigana na nchi ya EAC

Nimwombe Rais Samia awaondoe haraka wanajeshi wetu kule DRC Congo. Mnapigana na nchi ya EAC

Huo mgogoro huko DRC Mashariki uko kwa karibu miongo mitatu sasa, haujawahi kuwa na wala hauna madhara yoyote ya maana kwa Tanzania.
NHyakati zimebadilika sana sasa. Tunataka manufaa ya kiuchumi katika eneo hili bila ya vurugu za kivita.
Pakuanzia ni hapo panapovuruga amani ya eneo, yaani kwa akina Kagame.
 
Acha story nyingi za vijiweni, ingia mtandaoni usome mwenye kuhusu SAMIDRC.
Kwa hiyo umekwisha nihukumu na kujifanya wewe ndiye mjuaji? Si bora ukae na ujuaji wako mwenyewe badala ya kuuleta hapa kama hutaki kusikia ya wengine?
SAMDRC ni 'peace enforcer', siyo 'peacekeeper'.
 
Huyu Jamaa bado ana roho ya mauaji... Atakuja kinukisha tena...
 
Mbona huwa mnasema jeshi letu ni imara kuliko la Rwanda, sasa inakuwaje wanaingiza ubaridi tena? Au jeshi letu ni dhabiti kwenye kudhibiti rais wasio na silaha ambao hawaikubali ccm?
Ukiingia kwenye mapigano kuna kuua na kuuwawa.
 
Inaonekana askari wetu wanamalizwa sana huko tunafichwa idadi tu
Shida sio kufa au kutokufa; ila loss of lives iwe justified na intended end results. Vinginevyo ivyo vifo vinakuwa unnecessary loss of lives.

Kilichowaondoa US Afghanistan ni kukubali matokeo, baada ya miaka mingi sana ya kutumia billion of US dollars kutoa military training, police training na kuwapa kila zana wenyeji ya kukabiliana na Taliban.

Kasheshe sasa ikawa wakiwapa jeshi la ulinzi na polisi wa Afghanistan eneo la kusimamia wenyewe ndani ya week Taliban inaondoa local forces. after many years of trying huku US ikipoteza askari wake ikabidi wakubali matokeo aiwezekani.

Ndio scenario yetu Tanzania kwenye mgogoro wa East Congo, unakwenda unawaondoa waasi mkitoka tu wanarudi pale palę; mmaenda tena mkitoka yale yale till when.

Ujinga ni kufanya kitu kiłę kiłę na kutegemea matokeo tofauti. Ifike wakati wa kuongea na serikali ya Congo either wa commit kuwa na control ya hilo eneo au tuache liwalo na liwe.
 
Mtoa mada ni mnyarwanda siyo bure. Huwezi kuw mtz usielewe presence ya jwtz congo ina impact gani kwa taifa.
 
Na Kagame siyo wa mchezo mchezo. Ni Putin wa Afrika huyu, akiamua kumung'oa mama jua halizami.

PK aliwahi kumwambia JK, I will hit you!. JK hakutia neno.
Storybza vijiwe vya kahawa , kagame ni mtu mdogo sana tanzania hii hana jeuri yeyote
 
Rwanda ni sehemu tu ya mzozo ila matatizo ya Drc ni zaidi ya Rwanda.

zitto junior JokaKuu imhotep Richard
Uko sahihi 100%

Na kibaya zaidi na ambacho hakisemwi ni kwamba makabaila ndo wanokoleza mgogoro kwa manufaa yao.

Angalia msaada wanopewa M23 ambao wajumuisha vifaa cya kisasa kabisa.

Nimeongelea jambo hili lakini nahisi Goma na Kivu yote vitakuwa chini ya M23 na Rwanda bado watuhumiwa kuwa wapo nyuma yao.

Jiulize inakuwaje watu wązito wamehudhuria juzi maadhimisho ya mauaji ya Kimbari?

Bill Clinton, mwakilishi wa Israeli, majasusi waandamizi wa barani Ulaya na Marekani, makampuni ya kigeni na hata wawakilshi wa Ukrainę walikuwapo.

Hivyo mgogoro huu si wa kuhusu mipaka tu bali pia wahusisha wenye dunia na suala zima la siasa za kijiografia.
 
Na Kagame siyo wa mchezo mchezo. Ni Putin wa Afrika huyu, akiamua kumung'oa mama jua halizami.

PK aliwahi kumwambia JK, I will hit you!. JK hakutia neno.
bora ubaakie tu hivyohivyo ukiwa haujui lolote kuhusu Nchi yetu! we kula lala kwa amani
 
Na Kagame siyo wa mchezo mchezo. Ni Putin wa Afrika huyu, akiamua kumung'oa mama jua halizami.

PK aliwahi kumwambia JK, I will hit you!. JK hakutia neno.
Labda kuhit masikio yake kama madish ya ungo..
 
Uko sahihi 100%

Na kibaya zaidi na ambacho hakisemwi ni kwamba makabaila ndo wanokoleza mgogoro kwa manufaa yao.

Angalia msaada wanopewa M23 ambao wajumuisha vifaa cya kisasa kabisa.

Nimeongelea jambo hili lakini nahisi Goma na Kivu yote vitakuwa chini ya M23 na Rwanda bado watuhumiwa kuwa wapo nyuma yao.

Jiulize inakuwaje watu wązito wamehudhuria juzi maadhimisho ya mauaji ya Kimbari?

Bill Clinton, mwakilishi wa Israeli, majasusi waandamizi wa barani Ulaya na Marekani, makampuni ya kigeni na hata wawakilshi wa Ukrainę walikuwapo.

Hivyo mgogoro huu si wa kuhusu mipaka tu bali pia wahusisha wenye dunia na suala zima la siasa za kijiografia.
Genocide ilitokea Bill Clinton akiwa Rais wa USA na ni mojawapo ya mambo aliyolaumiwa sana kwa US kutofanya jambo lolote wakati huo
Rwanda ni mojawapo ya mataifa machache ya Africa yanayoisapoti Ukraine dhidi ya uvamizi wa Urusi.
Makampuni makubwa ya teknolojia yamawekeza Rwanda na Kagame ana mahusiano mazuri sana na nchi za Magharibi na Israel.
 
Back
Top Bottom