Nina mashaka Luteni Urio anaenda kuharibu ushahidi dhidi ya Mbowe na wenzake 3. Fact hizi hapa
Na kwanini Mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi wake akiwa na Bilicanas?

Je, hao makomandoo wangefanya kazi zipi kwake ambazo zingekuwa mpya tofauti na maisha yake ya siasa zaidi ya miaka ishirini?

Je, wajua komandoo mmoja anaweza kuwa na athali kubwa kwa nchi ambayo raia wengi hawana uelewa wowote wa kivita?

Kama makomandoo Wana athali kama unavyosema then why walifukuzwa kazi na wakawa Tu mtaani ?
 
A shahidi ambaye alisubiriwa kwa hamu kubwa ili kuujua ukweli ni huyu Lut Denis Urio. Sasa Shahidi wake wote mpaka sasa unathibitisha kuwa hakuna mahali popote Mbowe na walinzi wake walipanga ugaidi. Hakuna picha, hakuna video, hakuna voice notes na hakuna hata sms kuthibitisha kuwa kweli walikutana na Mbowe kupanga ugaidi.

Amekiri kwa kinywa chake kuwa aliwatafuta wale makomandoo waliofukuzwa kazi wakafanye kazi ya Ulinzi na siyo uhalifu na kuwaomba kuwa kukiwa na uhalifu wamwambie kitu ambacho hakikutokea, amethibitisha kuwa walitumiwa nauli kwenda kufanya ulinzi na siyo uhalifu, akasema kua angewaambia kua wanaenda kufanya uhalifu wangekataa kwa sababu wana viapo, maana yake walipofika kwa Mbowe wakaacha viapo vyao wakakubali kufanya uhalifu bila kumjuza[emoji1787][emoji1787].

Kwa maana hiyo mpaka sasa kina Adamoo na wenzake ni innocent maana hawakufanya uhalifu na wangekataa ikiwa kungekuwa na uhalifu, maana hata Lut Urio amekiri kwa mdomo wake kuwa wasingekuwa tayari kufanya uhalifu kwa sababu ya viapo vyao. Iweje leo waitwe magaidi? Asante sana Lut Urio imerahisisha kazi.

Hivi kweli DCI na timu yake wameambiwa kuna mipango ya ugaidi badala ya kumtuma Urio amrekodi Mbowe akimpa maelekezo ya kutekeleza ugaidi au ampige hata picha basi, yaani hadi wamtume akawashawishi kina Adamoo waende kwa Mbowe akiwadanganya ni ni kazi ya ulinzi kumbe ni ugaidi? Sasa kwa mantiki hii Polisi walizuia uhalifu au walichochea? Walishindwa nini kumkamata Mbowe kabla hata ya makomandoo hao kwenda Moshi?

Nasema asante sana Lut Urio kwa kuwasafisha Mbowe na wenzake. Sasa tumepata uelekeo wa kesi.


Eti Mama aombwe msamaha Gaidi Mbowe asamehewe, kwa lipi?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Unafki wa ACT Wazalendo wabaki nao majumbani mwao.CHADEMA si wanafki kama wao. Siyo waoga kama ACT.
bila Shaka haya Ni maoni yako sio ya jaji
 
Mabaunsa unazani diamond huyo? Je wanaweza kuzuia au kupambana kwa kutumia silaha za Moto Kama zile zilizomkuta lisu. Je hujifunza kutumia silaha?

Baunsa ilikuwa sawa kabla ya lisu
Umemjibu vizuri sana; ukweli hi nchi ina watu wana uelewa wa chini sana hadi aibu; imagine mtu mwenye uwezo wa kutumia computer ameuliza maswali ambayo hata mtoto wa darasa la saba hawezi kuuliza swali la KIJINGA kama hilo. Tatizo elimu yetu imetufanya tushindwe kufikiri na kuamua kukariri tu au UJINGA unaongezeka miongoni mwetu?? I am still thinking about it.
 
Umemjibu vizuri sana; ukweli hi nchi ina watu wana uelewa wa chini sana hadi aibu; imagine mtu mwenye uwezo wa kutumia computer ameuliza maswali ambayo hata mtoto wa darasa la saba hawezi kuuliza swali la KIJINGA kama hilo. Tatizo elimu yetu imetufanya tushindwe kufikiri na kuamua kukariri tu au UJINGA unaongezeka miongoni mwetu?? I am still thinking about it.
Mijitu iko bize na ligi za mipira tu unategemea nini?

Ni stories za matukio tu asubuhi hadi jioni...huyo mtu lazima awe mjinga kupitiliza
 
According to you. Boss wao mpya (FM) probably aliwapa maelekezo.
According to Urio...na Urio anasema wale ni askari na wana viapo, na walimuambia nchi kwanza kabla ya maslahi binafsi. Inaonekana hata hayo mahojiano hukuyasoma
 
According to Urio...na Urio anasema wale ni askari na wana viapo, na walimuambia nchi kwanza kabla ya maslahi binafsi. Inaonekana hata hayo mahojiano hukuyasoma
Wewe ndiye hukusoma ama hukuelewa. Alisema pia: ^Kazi kwa bosi (FM) imebadilika, tofauti na ile uliyotuambia!^

Meaning?
 
Key witness ameharibu kesi kwenye examination in chief, ukifika wakati wa cross sijui ndio itakuwaje sasa. Na nasubiri kwa hamu huyu shahidi analeta vidhibiti gani kusupport ushahidi wake
 
''Hivi kweli DCI na timu yake wameambiwa kuna mipango ya ugaidi badala ya kumtuma Urio amrekodi Mbowe akimpa maelekezo ya kutekeleza ugaidi au ampige hata picha basi, yaani hadi wamtume akawashawishi kina Adamoo waende kwa Mbowe akiwadanganya ni ni kazi ya ulinzi kumbe ni ugaidi? Sasa kwa mantiki hii Polisi walizuia uhalifu au walichochea? Walishindwa nini kumkamata Mbowe kabla hata ya makomandoo hao kwenda Moshi?''

Hapa ndipo nawashangaa hawa watengeneza kesi mchongo.Wawe smart kwenye kupika hivi vitu,aibu sana kwa kweli.
 
Wewe ndiye hukusoma ama hukuelewa. Alisema pia: ^Kazi kwa bosi (FM) imebadilika, tofauti na ile uliyotuambia!^

Meaning?
Hiyo meaning unataka kuitengeneza wewe hatuishi kwa hisia Bali uhalisia na lazima uthibitishe bila chembe ya shaka
 
Ukomandoo ni Kada muhimu Sana katika Jeshi na Ulinzi wa nchi. Ni Kada ambayo katika nchi za wenzetu mafunzo yake ni kitu cha Siri na cha kutukuka. Ni mafunzo ambayo Askari anayehitimu anakuwa amepita vipimo vyote na kufaulu Ikiwemo utimamu wa akili na mwili. Lakini pia mwenendo wake na historia ya maishà yake hutazamwa kama kipimo cha kumpa nafasi ya kupata mafunzo haya ya juu katika medani ya kimapigano. Huwezi kumpa Ukomando Mtu ambaye hujui mwenendo wake, tabia zake wala uwezo wake wa kuhimili mitikisiko Ikiwemo kuishi bila kipato rasmi, mateso ya kimwili, kiakili au kupoteza wapendwa wake.

Chukulia Mwalimu anayetegemewa kufundisha na kuivisha watu muhimu wa aina hiyo eti ni kama alivyo Lt Denis Urio wa 92KJ. Mwalimu aliyefundisha wanafunzi àmbao aailimia kubwa wamefukuzwa kazi Kwa utovu wa nidhamu halafu anapata deal la kuliokoa Taifa na Ugaidi anatumia hao hao watovu wa nidhamu?

Tusicheke na kudharau Makomandoo wetu wanapopita kwenye show off wamebeba magogo ya kilo 30 tukahadithiwa ni zana muhimu vitani. Tumesaidiwa Sasa kujua Aina ya wapishi (Walimu) wanaotumika kuwapika vijana hawa muhimu jeshini. Tumeoneshwa Walimu walivyo weupe kichwani kiasi cha kufikia kuuza maisha ya wanafunzi wao Kwa ahadi ya cheo cha kufikirika.

Komandoo anatakiwa kuwa na uwezo mkubwa wa kubalance nguvu na akili, lakini Urio ametutjibitishia amekuwa akifundisha matumizi ya nguvu asilimia 85 na akili asilimia 15. Mbowe ni raia Kwa asilimia [emoji817] Urio kama Komando tena Mwalimu wa Walimu Hakuna mahali popote anapoonesha kuchangia chochote katika kuendesha Mpango hatari wa Mbowe wa kufanya ugaidi.

Askari aliyeiva hawezi kupokea mpangokazi wa Mhalifu na kuuacha hivyo hivyo bila kushauri chochote ambacho kingemtia hatiani mhusika bila kuathiri wengine wasio na hatia. Ni wapi Urio baada ya kupeleka taarifa kwa DCI na Kingai alipoonesha kumwingiza Mbowe mtegoni zaidi ya kumwacha aendelee na mipango yake na yeye kutegemea huruma ya Mbowe kumpigia simu? Komando huyu anayehusudu nguvu pipa na akili Kisoda anamwachia Mhalifu aendelee na uhalifu bila followup wala tailing?

Achà Makomandoo waendelee kutuonesha aina ya mitembeo uwanja wa Taifa kumbe siyo kosa lao maana Taifa limeshindwa kuwapa Walimu sahihi.
 
00
Homeboy Urio katika ushahidi kakiri pesa zilizotumwa kwake zilikuwa ni nauli ili kufanikisha watu wanne wakapate kazi ya upambe/ulinzi...

Nyuma kidogo, kutoka mashahidi wale waliokuwa na simu, waliweka bayana kuwa hakuna mahali katika maandishi yaliyokaguliwa kama kulionesha kiashiria cha ugaidi...
P
 
Tanzania kuna kazi sana, hao makomandoo wamehisiwa kufanya uhalifu na wamekaa ndani hadi leo, kaa hisia tu!
Inasikitisha. Yaani makomandoo wanakamatwa na kusoteshwa kama vibaka! Yaani ili Kumfix Mbowe tu inabidi hadi jeshi lidhalilishwe na polisi! Polisi wenyewe hawa wa modeli ya wale wa Mtwara. Hiyo ni gharama iliyopitiliza. Ni bora itafutwe “bei” ya Mbowe anunuliwe kabisa. Iliwezekana kwa Slaa; bila shaka dau la Mbowe linaweza fikiwa tukapata ahueni! Ni sisi ndio tunaona aibu kwa haya mambo.
 
Back
Top Bottom