Nina Mgogoro kwenye ndoa, kila pesa anayopata Mke wangu anaenda kujenga kwao. Naomba msaada

Nina Mgogoro kwenye ndoa, kila pesa anayopata Mke wangu anaenda kujenga kwao. Naomba msaada

Nipo kwenye ndoa nimekuwa nikisoma tu lakini naona na mimi limenikuta.

Iko hivi wife na mimi tulifahamiana kijijini. Nilikuwa f6 yeye akiwa f4 leaver. Nilimsaidia akapata chuo cha takwimu akaenda akafanya akapata cheti. Wakati akiwa chuo nliamua kudate nae tukaoana (marriage) nikiwa nafanya kazi na yeye akiwa chuo.

Miaka mitatu baadae tulijaaliwa watoto wazuri. Maisha yaliendelea nikiwa kazini na yeye akiwa ofisi moja masuala ya takwimu nchini.

Mambo ya ndoa yalikuwa safi sana nilii injoi ndoa labda kwa sababu ilikuwa ya kusafiria. Maana yeye mkoa mimi mkoani.

Nilifanikiwa kumuhamishia mkoani kwangu yeye na watoto. Tuliishi vizuri kwa wastani wa miaka 5. Baadae mzazi wake yaani mkwe aka experience wakati mgumu (code). Tukashauriana tumjengee kibanda. Kwa kuwa wapo watoto wakubwa wakaona washirikiane wote. Kwa kuwa wife nde mwenye kipato kizuri akakopa banki 27M lakini nyumba haijaisha.

Kero ikaanza sasa. Kila wakati anataka pesa ya ujenzi kwa mama mkwe. Kumbuka yule ni mzee ile nyumba watakuja kugombana watoto nikamwambia ujenzi hauishi siku moja. Buy time.

Majuzi alipata bingo ofisini kwao 20 Mil ni pesa ya offer ya Serikali yenye riba kidogo.

Lahaulaaa si akaipeleka yote kwenye ule ujenzi.

Wana JF wenzangu, kumbuka si kwamba sisi na watoto wetu hatuna mahitaji, hapa ada, nyumba haijaisha asilimia Mia. Why apeleke 20 kwao? Mwanamke kiumbe wa ajabu sana.

Hivi? Hajui ile nyumba hawataishi watoto wake? Hivi hajui ile nyumba watagombea vidume?

Ndani ni kuchuniana. Najuta sana kuoa mwanamke huyu.

Niko puzzled. Epuka kusomesha mchumba.
Kwenye swala la pesa siyo mke wakp tu ila binadamu akipata pesa hubadalika, Why do people change when they have money?
 
Nipo kwenye ndoa nimekuwa nikisoma tu lakini naona na mimi limenikuta.

Iko hivi wife na mimi tulifahamiana kijijini. Nilikuwa f6 yeye akiwa f4 leaver. Nilimsaidia akapata chuo cha takwimu akaenda akafanya akapata cheti. Wakati akiwa chuo nliamua kudate nae tukaoana (marriage) nikiwa nafanya kazi na yeye akiwa chuo.

Miaka mitatu baadae tulijaaliwa watoto wazuri. Maisha yaliendelea nikiwa kazini na yeye akiwa ofisi moja masuala ya takwimu nchini.

Mambo ya ndoa yalikuwa safi sana nilii injoi ndoa labda kwa sababu ilikuwa ya kusafiria. Maana yeye mkoa mimi mkoani.

Nilifanikiwa kumuhamishia mkoani kwangu yeye na watoto. Tuliishi vizuri kwa wastani wa miaka 5. Baadae mzazi wake yaani mkwe aka experience wakati mgumu (code). Tukashauriana tumjengee kibanda. Kwa kuwa wapo watoto wakubwa wakaona washirikiane wote. Kwa kuwa wife nde mwenye kipato kizuri akakopa banki 27M lakini nyumba haijaisha.

Kero ikaanza sasa. Kila wakati anataka pesa ya ujenzi kwa mama mkwe. Kumbuka yule ni mzee ile nyumba watakuja kugombana watoto nikamwambia ujenzi hauishi siku moja. Buy time.

Majuzi alipata bingo ofisini kwao 20 Mil ni pesa ya offer ya Serikali yenye riba kidogo.

Lahaulaaa si akaipeleka yote kwenye ule ujenzi.

Wana JF wenzangu, kumbuka si kwamba sisi na watoto wetu hatuna mahitaji, hapa ada, nyumba haijaisha asilimia Mia. Why apeleke 20 kwao? Mwanamke kiumbe wa ajabu sana.

Hivi? Hajui ile nyumba hawataishi watoto wake? Hivi hajui ile nyumba watagombea vidume?

Ndani ni kuchuniana. Najuta sana kuoa mwanamke huyu.

Niko puzzled. Epuka kusomesha mchumba.

Chai

"akakopa banki 27M lakini nyumba haijaisha"
 
sijaona unacho lalamika, kwanza mkeo anakupenda ndiyo mana amekushirikisha kuna wengine wanakopa kimya kimya na wanawapa wanawowafanyia masagi kimya kimya!
 
Kama anajenga kwa pesa yake ni sawa,huo mkopo atalipa yeye..wewe pesa yako jenga hiyo yako,ingekua ni mimi ningemwacha ajenge kiroho safi
Ni kweli mkuu yeye amuache cha muhimu aombwi pesa ya ujenzi wala pesa ya kulipa deni. kingine na yeye akope pesa ajenge nyumba yake au na yeye awajengee wazazi wake nyumba.
 
Wewe unaGombana na mkeo kwa jambo la kijinga sana,unataka asijenge kwao!? Ishini na wake zenu kwa akili,mimi mke wangu juzi kakopa milioni 10 akaenda kukarabati nyumbani kwao ilikhali sisi tuko katika nyumba ya kupanga.
Pigia mstari neno ishini nao kwa akili.
Mkuu wanawake nao wana haki ya kujenga makwao kama wanaume wanavyo waboreshea wazazi wao kijijini, lakini inategemea na mira na tamaduni, mfano kwa sisi Mwanamke akishaolewa ana kuwa sehemu ya familia ya Mwanaume na kujenga au kuwajengea wazazi nyumbani kiijin ni vigumu, kwasababu mtoto wa kike hapati mirathi, mfano kwenye kugawana aridhi mtoto wakike hapati.
 
Mlikuwa mkoani,je mkeo ni mkimya? Nadhani mpaka inafika hii hatua kuna sehemu uligusa na hajaongea.

Binadamu akichoka kabisa huwa haongei na hilo ni jambo linapikwa kuhusu madhara sijui maana itategemea na mienendo yenu huko nyuma ulimjali vipi na ulifanya nini wakati hana
 
Kaka pesa ya mke huwa sio ya familia .hongera umejua unaishi na shetan nakushauri Anza ujenzi wa nyumba na ww kisirisiri ambayo hata mkiachana asiijue kabisa .pia nasisitiza PIMA WATOTO WOTE DNA .Utanishukuru
 
Ndoa nyingine ni utapeli ,nakushauri mkae chini muwajengee watoto wenu ,kujenga nyumba ya ndugu sijui mzazi kma mnataka ya kifahari utaumia na usitegemee pesa ya mke.

Maisha gani kama majambazi mnaviziana..

Fanyeni muwajengee watoto wenu mapema msije kuwapa mitihani baadae waje kuwajengea nyie ,mwanamke akishajenga kwao hapo atakuletea nyodo maana kashapata pa kukaa.
Sasa mkuu huyo Mwanamke siku wazazi wake walifariki na mirathi ikigawanywa unazani hiyo nyumba ataimiliki yeye Mwanamke, na kama kajenga kwenye kiwanja cha familia , wazazi waki Afrika ukiwajengea nyumba kwenye maeneo yao elewa kwamba kama mpo watoto kumi kwenye mirathi mnagawana sawa, na Wazazi wetu kuandika wosia ni ngumu, wanajua wakiandika wosia utaleta chuki kwa watoto.
 
Jambo ambalo unatakiwa kufahamu siku zote, mshahara wa mke siyo mshahara wako!
Ila mshahara wako ni mshahara wa mkeo!
Kwa mantiki hiyo siku zote Mwanaume ishi kana kwamba ni wajibu wako kumtunza mkeo na watoto wako! Familia ni ya Mwanamme siyo ya Mwanamke.
Hata hivyo kwa hili la kumjengea Mzazi wake nyumba siyo kosa la kukufanya ujute kuoa!
 
Msimamo wa kijinga sana huu...
Mimi kama mwanamke nasema pesa ya baba na mama ni ya familia
Kila amount inayopatikana kipaumbele ni familia ndo wengine wanafata.
Ndoa ni taasisi.. kuna hela zinatoka tu kimya kimya,
Ila kuna kiwango kulingana na kipato cha wahusika lazima mshauriane
47M kwenye nyumba ya familia na hela inakatwa kwenye mshahara na nyumba haijaisha ni KUKOSA MAARIFA unless hiyo ni nyumba yake anazuga tu
Afadhari wanawake muongee maana kuna wanaume ni wanawake hadi kuwazidi wanawake
 
Back
Top Bottom