Nina mtaji wa laki nne na nusu, naombeni ushauri nifaye nini?

Nina mtaji wa laki nne na nusu, naombeni ushauri nifaye nini?

Biashara!

Watu wengi humu watakushauri kwa kukuambia fanya hiki ama kile ila mifano yote hiyo ya biashara watakazo kupatia ni kutokana na mafanikio ambayo wamewahi kuyapata au wameyapata kupitia biashara hizo ila walio wengi ni kwamba hizo sio biashara zao za kwanza isipokua ni zile biashara ambazo ziliwafanikisha baada ya msululu wa biashara nyingi ambazo wamewahi kuzifanya na kufeli, na Watu hawa ukiwauliza ni jambo gani la tofauti ambalo wamelifanya hadi kupelekea mafanikio kutoka kwenye hiyo biashara ambalo katika biashara zingine zilizokufa hawakulifanya hawatokua na jibu la uhakika la kukupa.

Na ndio maana huwa sipendi kumshauri mtu kwa mtindo wa moja kwa moja kwa maana haya mambo huwa hayana formula lakini...

Nataka uwe na hakika kwamba kila mtu anao uwezo wa kufanikiwa kibiashara lakini si kila biashara inayo uwezo wa kumfanikisha kila mtu.

Kwani...

Biashara ni neno moja katika jicho la kawaida la walio wengi ila kwa jicho la ndani biashara ni muunganiko wa maneno mawili ambayo ni kusaidia pamoja na fedha na maneno haya huwa hayaendi pamoja kwa hiyo unapoanzisha biashara yoyote lazima uamue neno lipi utaanza nalo na lipi litafuata, uchaguzi wako wa lipi lianze na lipi lifuate ndio ambao utatoa taswira ya muda gani utakaa na hiyo biashara kabla haijawa yakudumu au kukufia mikononi mwako mwenyewe.

Na hii ndio sababu ya kwanini ni ngumu kumpa mtu ushauri wa biashara gani afanye kwa maana haujui ni changamoto za kiasi gani za kifedha zilizomzunguka ambazo zinamuhitaji yeye azitatue na kuanza kwake biashara anategemea kesho aanze kupata faida ili atatue changamoto zake.

Na ndio maana ushauri wa biashara nyingi za kufanya ambao watu wamewahi kupewa walipoamua kuzianzisha biashara hizo zilikufa kwa maana wengi huanzisha biashara huku wakichagua kwenda na neno fedha badala ya kusaidia.

Sasa fedha inakawaida ya kuwazingatia wale watu ambao hawaizingatii, na sababu ya fedha kufanya hivyo ni kwamba watu wengi ambao hawaizingatii fedha huwa sio wabinafsi, na hii inamaanisha kwamba fedha na ubinafsi huwa havikai nyumba moja.

Na kikawaida ni kwamba nyakati nzuri ambazo mtu huwa hawi na mazingatio makubwa kwenye fedha ni zile Nyakati ambazo uhitaji wa fedha kwake ni mdogo au haupo kabisa.

Na nyakati pekee ambazo mtu anakua katika hali hiyo ni zile nyakati ambazo anakua hana cha kupoteza kwa maana ukiachana na yeye mwenyewe hana watu wengine ambao changamoto zao za kifedha zinamtegemea yeye kuzitatua.

Ukishakua na changamoto nyingi za kifedha ambazo unahitaji uzitatue, kwenye biashara utachagua kwenda na neno fedha na utaachana na kusaidia na ukishaachana na kusaidia basi unakua mbinafsi na ukiwa mbinafsi fedha inatengana na wewe na fedha ikishatengana na wewe hautakua na nguvu ya kuendelea na hiyo biashara kwahiyo itafia mikononi mwako mwenyewe.

Ili uweze kupata unafuu kidogo inabidi utumie mbinu ya kujitengenezea kazi mwenyewe badala ya biashara.

Kwa maana biashara na kazi ni mambo ambayo hayana utofauti pindi yanapoanza kwenye lile swala la muda ila kadri siku zinavyokwenda biashara hujitenda kwenye kazi.

Kazi inaweza kuanzishwa na mtu yeyote yule kwa maana huwa wazo lake likimjia mtu kichwani muda huu basi kesho anaweza akalitekeleza na kuingia sokoni moja kwa moja ila biashara ni ngumu kwa maana huwa inahitaji mchakato wa muda mrefu tangu wazo linapomjia mtu kichwani hadi kuingia sokoni kwa maana linahitaji nguvu zote nne za asili ya ulimwengu ziweze kuingia ndani yake.

Kwahiyo sio kila kazi inaweza kuwa biashara ila zipo kazi ambazo zinauwezo wa kuwa biashara kwahiyo kama wewe uko na changamoto nyingi zinazohitaji fedha na unataka uanze kupambana mwenyewe anzia kwenye hiyo hatua ya kazi kabla ya kwenda kwenye biashara.

Biashara huwa tunaipima kwa magnitude and leverage, ila kazi haina hizo sifa ingawa kuna kazi ambazo zinauwezo wakupelekwa kwenye hizo sifa na hizi ndio unatakiwa uanze nazo kwa maana unahitaji uwe mfanya biashara.

Kila la heri.
 
Miss kuna kitu nataka tuwekane sawa....
Mimi mwenyewe mfanya biashara kuna mambo yanafanywa na mtu ila ukifatilia deep unajua undani wa kile anachofanya..

Naposema apambane na vibarua apate kama M1 hivi namaanisha na atanishukuru kuna vitu sio vya kusema ukurupuke tu mkuu
Nitakupa story yangu Kwa ufupi
Nilimaliza chuo 2015
Baada ya kupambana kusaka nikawa na laki 1 tu
Nikaamua nichukue zile t-shirt manga plain, nianze kuuza kimachinga mtaani
Zile t-shirt zilipendwa na watu sana
Nilikuwa nanunua sh 6000 nauza 15000
Hadi nikawa maarufu chinga matishet

Nikipata order nyingi sana
Huu mtaji ndo umenipa kila kitu baada ya miaka 9 saiv Nina maduka mawili ya nguo yenye kila kitu
Naendaga kariakoo naifunga mzigo kuanzia million 10 Kwa mtaji wa laki 1

Hii story ni ya kwangu binafsi na Iko ivo
Usidharau mtaji wowote
Biashara ni timing tu mkuu na ubunifu wako tu
Laki 4 anakomaa na anatoka vizur
 
Nitakupa story yangu Kwa ufupi
Nilimaliza chuo 2015
Baada ya kupambana kusaka nikawa na laki 1 tu
Nikaamua nichukue zile t-shirt manga plain, nianze kuuza kimachinga mtaani
Zile t-shirt zilipendwa na watu sana
Nilikuwa nanunua sh 6000 nauza 15000
Hadi nikawa maarufu chinga matishet

Nikipata order nyingi sana
Huu mtaji ndo umenipa kila kitu baada ya miaka 9 saiv Nina maduka mawili ya nguo yenye kila kitu
Naendaga kariakoo naifunga mzigo kuanzia million 10 Kwa mtaji wa laki 1

Hii story ni ya kwangu binafsi na Iko ivo
Usidharau mtaji wowote
Biashara ni timing tu mkuu na ubunifu wako tu
Laki 4 anakomaa na anatoka vizur
Hongera boss ulikuwa unazungusha au ulitega goli sehemu
 
Madam nipo seriously...
Wee biashara ya laki nne kama unashauri afanye sawa alafu alete mrejesho hapa..

Maana nakumbuka nilikua na pesa zaidi ya hiyo kipindi hicho na ni mfatiliaj sana wa nyuzi kule jukwaa la biashara..

Mkuu ipo hvi ukitaka kufanya biashara ili ujue pesa hiyo inatosha au laa ingia mzigoni ndo utajua ujui mkuu...

Naposema jamaa ajichange basi namaanisha kama anataka kufanya afanye alafy ataleta mrejesho hapa..

Usiingie katika biashara kwa ku test et fulani mbona alifanya hivi na mi ngoja nijaribu...
Biashara hata kama unaanza mdogo mdgo sio kwa laki 4..

Wakuu kuweni serious
Kwahiyo biashara serious inatakiwa aanze na milioni ngapi? 😁
 
t
Madam nipo seriously...
Wee biashara ya laki nne kama unashauri afanye sawa alafu alete mrejesho hapa..

Maana nakumbuka nilikua na pesa zaidi ya hiyo kipindi hicho na ni mfatiliaj sana wa nyuzi kule jukwaa la biashara..

Mkuu ipo hvi ukitaka kufanya biashara ili ujue pesa hiyo inatosha au laa ingia mzigoni ndo utajua ujui mkuu...

Naposema jamaa ajichange basi namaanisha kama anataka kufanya afanye alafy ataleta mrejesho hapa..

Usiingie katika biashara kwa ku test et fulani mbona alifanya hivi na mi ngoja nijaribu...
Biashara hata kama unaanza mdogo mdgo sio kwa laki 4..

Wakuu kuweni serious
Una wazo mkuu, usikilizwe
 
Sawa mkuu nipo hapa
Jibu maswali haya:
1.. je unakipaji chochote
2.. je una utaalamu wowote
3. Je una wazo la biashara
4. Je una majukumu ya kila siku
5. Je ni kijana mwenye nguvu, (are you drive and energy)
6. Je umewahi kufanya biashara yoyote jadili
7. Je uko tayari kukosolewa
8. Unaweza kutunza mahesabu ya kila siku
8. Je unaweza kuwatambua wateja wako taraji
9. Je unaweza kuwatambua wapinzani wako nguvu zao na mapungufu yao, pamoja na wateja wao, hao wateja wao wanakotoka

10. Ainisha nguvu zako na mapungufu yako kwa biashara unayotaka kifanya

11. Zitaje tabia 10 za wajasiriamali waliofanikiwa
12. Je unazijua sababu kwanini biashara zinakufa, zitaje
13. Kama unajua kwamba biashara zinakufa kwanini wewe huogopi kufanya biashara
14. Je unaweza kufanya utafiti wa masoko?
15 zitaje mbinu utakazo zitumia kujua kama wazo lako la biashara linaweza likawa halisia

Baada ya kujibu maswali haya tutaendelea na mpango mwingine
 
Back
Top Bottom