Nina shilingi milioni 64, niwekeze kwenye biashara gani kati ya hizi?

Nina shilingi milioni 64, niwekeze kwenye biashara gani kati ya hizi?

Kuna ndugu yangu alikuja kutoka ulaya akauliza rafiki zake afanye biashara gani. Jamaa kila miezi anabadilisha biashara, mpaka hela imeisha wale washauri nao mbio(wamemkibia). Jamaa kachanganyikiwa sasahivi, fanya utafiti mwenyewe na weka uamuzi mwenyewe hakikisha usitie hela yote kwenye biashara.
Dooooohhhh...!! Balaa.
Asante kwa angalizo mkuu
 
Habarini wakuu. Natumaini mnaendelea vizuri na maandalizi ya sikukuu.

Bila kuwachosha sana, nimeweza ku save jumla ya shilingi milioni 64 hadi sasa, kiasi hiki nimeweza kukisave kuanzia mwezi April mwaka huu kutoka kwenye mshahara wangu. Nipo mkoa wa Dodoma.

So far, nimefikiria kuwekeza katika mojawapo ya mambo yafuatayo:

1. Ninunue eneo la shamba kubwa maeneo ya Dodoma nje ya mji au Dodoma vijijini kisha nianzishe kama ranchi hivi ya ufugaji wa mbuzi.

Nimefikiria mbuzi kwa sababu kwa utafiti wangu wa muda mfupi nimeona kuwa mbuzi hawana complications nyingi kulinganisha na wanyama wengine wa kufuga, na pia kuna fursa zaidi kwa mbuzi nchini, na demand ambayo haijawa satsified.

Lengo la hii ni baadae niweze kuwa na kiwanda kabisa cha kuchinja na kuprocess nyama ya mbuzi, na kuweza hata kuuza ndani na nje ya nchi products za nyama ya mbuzi.

2. Nifungue park kwa ajili ya michezo ya watoto kwa Dodoma. Moja ya gaps ambazo nimeziona Dodoma ni kukosekana kwa eneo zuri la maana kwa ajili ya michezo ya watoto na watu kupumzika pia.

Hapa nafikiria ninunue eneo Dodoma then nilitengeneze vizuri na kuweka michezo ya watoto (indoor na outdoor) ya kutosha, pamoja na kutengeneza garden nzuri ya kuvutia kwa ajili ya watu na familia zao kupumzika na kupigia picha.

Kwa nje kwenye ukuta nawaza pia kuwe na frame kadhaa ambazo nitakodisha kwa watu waweke maduka ya vyakula, vinywaji, na vitu vya watoto.

3. Nifungue kiwanda cha maji ya kunywa yale ya kwenye dispenser kwa ajili ya matumizi ya majumbani na maofisini. Nimeona gap pia hapa kwa sababu makampuni yaliyopo hapa Dodoma kwa hii huduma hayatoshelezi mahitaji kwa kiasi kikubwa, mara nyingi sana unakuta yanapotea sokoni kwa muda fulani (no consistency of supply).

4. Ninunue kiwanja saizi ya kati maeneo ambayo sasa hivi ndo yanajengeka (eg Ilazo, NALA) halafu nipige vyumba vya low-cost (behewa style), niweke hapo vyumba kadhaa, then nipangishe nile kodi kila mwezi hata 50K kwa kila room. Baadae kadri ninavyopata mpunga zaidi, niongeze idadi ya vyumba zaidi na zaidi.

Wenye uzoefu wa biashara na ideas na mnaoifahamu Dodoma, niambieni hapo nianze na ipi kati ya hizo kwa mtaji huu nilionao (milioni 64), au hata idea nyingine ambayo sijaitaja hapo juu.

Mimi maisha yangu yote nimeajiriwa tu hadi sasa (nina umri wa miaka 35). Sijawahi kufanya buashara hata ya kuingiza shs 500. Nimeona ni bora pia niangalie upande huu wa business pia maana siwezi ajiriwa milele, na pia kama mjuavyo hizi ajira zetu, leo ipo kesho haipo hasa huku private sector.

Natanguliza shukrani.
Kwanza nikupe hongera mkuu kwa kuweza kukusanya mtaji, Mimi nitakushauri mambo machache ya kufanya

1. Kwa kuwa hujawahi kufanya biashara yoyote ile , Ili kuepuka kupoteza mtaji fanya biashara ambayo haita risk mtaji wako kwa kipindi Cha miezi isiyopungua 6 Ili kupata uzoefu wa hesabu za mapato na matumizi yatokanayo na biashara, mfano anzisha tu kagoli ka tigopesa au uwakala wa bank ( kuwa makini na eneo utakalochagua) hapa test tu na mtaji wa 4m lengo ni kuzoea biashara na namna hesabu zinavoenda huku mtaji wako ukiwa salama



2. Option nyingine wekeza kwenye real estate ( tafuta maeneo yenye potential kwa baadae mfano maeneo ambayo lami itapita siku za usoni tafuta hata heka kadhaa za karibu na barabara kisha tulia zako ( kuwa makini na road reserve), lami ikipita hayo maeneo yatapanda almost mara 4 au tano ya bei uliyonunulia, Kuna maeneo jamaa alinunua eka kwa 250k saivi wadau wanapataka kwa milion 8 na jamaa hataki kuuza


3. Usiingie kwenye kilimo,ufugaji, uchimbaji, au ujenzi huko utapoteza pesa (kama interest yako Ipo kwenye kilimo, au ufugaji hakikisha unatumia faida itakayopatikana ) hivi vitu hupotezaga pesa ndani ya sekunde

4. Kuna nyuzi zangu mbili niliziandika siku za nyuma nikitaka partner mwenye mtaji wa around 3m to 6m na ni 0 risk ukiwa tayari zipitie tunaweza fanya kitu kwa mtaji wa million 6 tu

Hongera
 
Asante mkuu, nitaingia field kwa utafiti, maana mimi pia sina taarifa za kutosha kuhusiana na biashara ya lodge.
Taratibu za lodge wala si ngumu na unaweza kuzimudu hakika..

Mfano:
1: Ramani ya nyumba yenye vyumba sita au Name kwa mfumo wa apartment hii inaleta muonekano kama motel hivi.

2: Fence kali ya kuvutia na mapambo ya miti natural plants with surrounded cctv cameras hadi hapo reception na lazima uchimbe kisima cha maji au ikiwa supply ya maji ya dawasco ipo sawa unachimba kile kisima cha uhifadhi maji pamoja na tanks kadhaa juu ya Hilo Shimo unajenga kwa mfumo wa kajumba au chumba chenye andaki hipa ndio pataonekana kama sehemu ya mapokezi mtu akiingia getini pia unaweza ukadizaini kama counter flani ya vinywa ukauza kwa wateja.

3: Kuhusu furniture unaweka zile zenye hali tofauti ili ikurahisishie kwenye kupanga bei na kuweza kupanga bajeti yako ya uendeashaji kwa urahisi kwa maana ya matumizi ya kila siku wakati wakazi za wahudumu na mishahara.

3: Jitahidi kuweka paking nzuri na isiyo ya kubana ili kuepusha misongamano ya magari bila kusahau kasehemu kapembeni kwa ajili ya mapunziko na mazungumzo kwa wateja wasafiri na hata watalii pia.

4: Kiwanja hapa kwenye hili nakushauri zingatia vile vilivyopo kwenye mazingira ya watu ili kuvutia wateja kwa wingi na usalama zaidi kwakua haitakuwa na mushikeri za uvamizi kwa wageni ila ujitahidi kuweka ukaribu na askari ili linapotokea tatizo kwako iwerahisi kuliweka sawa na kuendelea na biashara na hii ni msaada hata kwenye matukio mengine kadhaa yanayotokea nyakati za biashara.
 
Tafuta eneo weka guest house hata room chache za kuanzia kwa uko ulpo man utakuwa unaongezea kadiri siku ziendavo. Man hiyo hainaga mlolongo ni fulu fedha. Ila codes za kazi unapaswa kuzijua
Cheki wazo la huyu mdau Naona limo konki pia mno. Ujue biashara Ni eneo, mtaji na msimamizi. Eneo Ni market. Hasahasa msimamizi ndio kila kitu. Sasa wewe upo jobu kaloji kwenye mikoa ambayo Ni municipal like Mpanda. Unakomaa hata na self tano room za Mana. Nadhani kila room unaweka 10-15/20 hukosi milioni kwa mwezi.

Loji iko POA pia uangalizi wake Ni kamera. Chumba Cha show time kuwepo, uza na gandomu ikiwezekana weka dada mzuri mweupe mwenye nyamanyama na sio kimbaumbau, yaani ambaye anafanya mtu anaenda kualalapo.
 
Mkuu mm ni jobless ili jarbu huku

1.biashara ya nafaka hapo Dodoma alizeti (hao unaweza kununua na mashine ya kukamulia ukapata mafuta na Mashudu utatauza kama chakula cha mifugo), karanga,mahindi na ufuta ukiwa na center unayafata mazao hukohuko shambani...

2.nenda sehemu inaitwa Mvumi misheni kule kuna hospitali ya macho kumechangamka sana umeme umefika kafungue phamacy kubwa ya kisasa ifanye kazi 24hrs

3.kaweke mashine ya kusaga na kukoboa hukosi 60k kwa siku kijiji cha Mvumi makulu (kwa kina palamagamba kabudi) na hata Mvumi misheni

4.hii acha nibaki nayo

5.Hii pia acha nibaki nayo
 
Kwanza nikupe hongera mkuu kwa kuweza kukusanya mtaji , Mimi nitakushauri mambo machache ya kufanya

1. Kwa kuwa hujawahi kufanya biashara yoyote ile , Ili kuepuka kupoteza mtaji fanya biashara ambayo haita risk mtaji wako kwa kipindi Cha miezi isiyopungua 6 Ili kupata uzoefu wa hesabu za mapato na matumizi yatokanayo na biashara, mfano anzisha tu kagoli ka tigopesa au uwakala wa bank ( kuwa makini na eneo utakalochagua) hapa test tu na mtaji wa 4m lengo ni kuzoea biashara na namna hesabu zinavoenda huku mtaji wako ukiwa salama



2. Option nyingine wekeza kwenye real estate ( tafuta maeneo yenye potential kwa baadae mfano maeneo ambayo lami itapita siku za usoni tafuta hata heka kadhaa za karibu na barabara kisha tulia zako ( kuwa makini na road reserve), lami ikipita hayo maeneo yatapanda almost mara 4 au tano ya bei uliyonunulia, Kuna maeneo jamaa alinunua eka kwa 250k saivi wadau wanapataka kwa milion 8 na jamaa hataki kuuza


3. Usiingie kwenye kilimo,ufugaji ,uchimbaji,au ujenzi huko utapoteza pesa ( kama interest yako Ipo kwenye kilimo,au ufugaji hakikisha unatumia faida itakayopatikana ) hivi vitu hupotezaga pesa ndani ya sekunde

4. Kuna nyuzi zangu mbili niliziandika siku za nyuma nikitaka partner mwenye mtaji wa around 3m to 6m na ni 0 risk ukiwa tayari zipitie tunaweza fanya kitu kwa mtaji wa million 6 tu


Hongera
Acha utapeli
 
Kwanza nikupe hongera mkuu kwa kuweza kukusanya mtaji , Mimi nitakushauri mambo machache ya kufanya

1. Kwa kuwa hujawahi kufanya biashara yoyote ile , Ili kuepuka kupoteza mtaji fanya biashara ambayo haita risk mtaji wako kwa kipindi Cha miezi isiyopungua 6 Ili kupata uzoefu wa hesabu za mapato na matumizi yatokanayo na biashara, mfano anzisha tu kagoli ka tigopesa au uwakala wa bank ( kuwa makini na eneo utakalochagua) hapa test tu na mtaji wa 4m lengo ni kuzoea biashara na namna hesabu zinavoenda huku mtaji wako ukiwa salama



2. Option nyingine wekeza kwenye real estate ( tafuta maeneo yenye potential kwa baadae mfano maeneo ambayo lami itapita siku za usoni tafuta hata heka kadhaa za karibu na barabara kisha tulia zako ( kuwa makini na road reserve), lami ikipita hayo maeneo yatapanda almost mara 4 au tano ya bei uliyonunulia, Kuna maeneo jamaa alinunua eka kwa 250k saivi wadau wanapataka kwa milion 8 na jamaa hataki kuuza


3. Usiingie kwenye kilimo,ufugaji ,uchimbaji,au ujenzi huko utapoteza pesa ( kama interest yako Ipo kwenye kilimo,au ufugaji hakikisha unatumia faida itakayopatikana ) hivi vitu hupotezaga pesa ndani ya sekunde

4. Kuna nyuzi zangu mbili niliziandika siku za nyuma nikitaka partner mwenye mtaji wa around 3m to 6m na ni 0 risk ukiwa tayari zipitie tunaweza fanya kitu kwa mtaji wa million 6 tu


Hongera
Asante sana kwa mawazo kuntu mkuu. Nimependa sana reasoning ya ushauri no 1. Nazicheki hizo nyuzi zako.
 
Hakuna biashara nnaiamini kama ya real estate. Nyumba ni asset ambayo haitokuja ku depreciate value. So hata ukijenga ukapangisha all is well.

Tatizo la nyumba unazika pesa na faida inakuja kuonekana baada ya miaka mpka 7,8 na kuendelea mbele hapo unadhani kibongobongo hiyo ni hasara chukulia nyumba ya M50 kali unapangisha 500k kwa mwenzi hapo Ela inarudi baada ya miaka 9 hapo ikiwa imepangishwa non stop na kitu ambacho hakiwezekani pia kodi nimechukulia kodi ya 500k ambayo ni kubwa ila kikawaida ni 200k mpka 300k.
 
Back
Top Bottom