Ningekutana na Rais leo, Nimgemwuliza kwanini amemtoa Mchengerwa Utawala Bora

Watumishi wa uma ni zaidi ya laki nne,wewe umeongea nao wote,acha uhuni wewe.
Cochran's sampling formula inakupa sample size ya kuweza ku-generalize results for the population. Inawezakana johnthebaptist katumia methodology hiyo (sampling). Sio lazima ahoji watumishi wote. Sawa?
 
Mchengerwa yule aliyesema 21% ya ajira ziende Zanzibar ?

Watanganyika ni mazezeta kupindukia
 
Kwahiyo polisi wapo chini ya utumishi sio?!

Na hao polisi waliopanda vyeo mwezi mmoja baada ya kuwa wamemaliza kozi ni wa level ipi?! Hawa hawa wanaotokea CCP wakiwa kama Private, ndo unataka kusema mwezi mmoja baadae wakawa Makoplo?
 
Kura ya maoni imechukukiwa lini na taasisi gani, hao ni watumishi wa taasisi gani, naona Kama ni kikundi Cha mchengerwa kumpa promo kupitia JF, hii ndio michezo ya kina JK

Huko kwenye utumishi amekaa miezi mingapi, ametatua kero gani,
Ndugu hakuna kitu km hicho, mimi kama mtumishi wa umma bila ubaguzi wala upendeleo huyo Jenista Mhagama ametuminya sana,hana la maana amefanya kwa watumishi ila huyu kijana Mchengerwa kwa muda mfupi amekuwa nuru na suluhu ya mambo mengi yalikuwa yanawakabili watumishi. Hivyo si kwamba watu wanampa promo bila sababu, jiulize kwanini wamezungumza sana kuliko wengine? Kwanini hawajamlilia Ndalichako? Wakati mwingine hata km anayo mapungufu yake lakini watumishi walimkubali sana kuliko Jenista Mhagama
 
Raha Sana kazi yako ukiifanya vizuri hadi watu wanakulilia. Lakini huyu jamaa binafsi sikuwahi kusikia sifa zake zaidi ya kipindi kile Cha kupandisha madaraja watumishi. Alikuwa kimya Sana.
Aliyekutana nae kiutendaji atuambie ni mtu wa namna gani
 
MAMA NAKUOMBA TOA HUYO MDHULUMATI WA HAKI ZA WATUMISHI. HISTORIA YAKE INAMHUKUMU. MDHULUMATI MKUBWA WW.
 
Kweli watumishi mmeumizwa sana Poleni.
naamini Mhe. Rais Mama yetu atalifanyia kazi suala hilo.

Lakini pia kama Jeni ujumbe umemfikia basi ni bora akajiengua mapema kuliko kuja kuenguliwa kwa fedheha, upepo unao vuma dhidi yake sio mzuri hivyo ajitafakari mapema kabla ya hatari.
 
Kweli watumishi mmeumizwa sana Poleni.
naamini Mhe. Rais Mama yetu atalifanyia kazi suala hilo.

Lakini pia kama Jeni ujumbe umemfikia basi ni bora akajiengua mapema kuliko kuja kuenguliwa kwa fedheha, upepo unao vuma dhidi yake sio mzuri hivyo ajitafakari mapema kabla ya hatari.
 
Zanzibar ni Nchi Hilo moja pili hiyo 21% ni takwa la mama au NI takwa la kisheria??
 
Ficha ujinga wako
Huu sio ujinga,ni ukweli mchungu.Kati ya hao mabosi mnaoita wenye roho mbaya na wenye roho nzuri wapi huwa wanatumbuliwa?

Yaani siku ukija kuajiriwa sekta binafsi ukawa boss afu ukawa vizuri kwa watumishi wa chini huchukui round.

Ni aidha uwe mnafiki kujifanya unajali watumishi wa chini huku unawafanyia mnayoita roho mbaya wasimamizi wao,ukirogwa tuu ukawa fresh kwa wote ujue uongozi umekushinda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…