Nini sababu ya Matajiri wengi kutokuwa wakweli juu ya utajiri wao?

Nini sababu ya Matajiri wengi kutokuwa wakweli juu ya utajiri wao?

Ni kwasababu mara nyingi utajiri wameupata kwa njia za panya, yaani kihalifu

Mhalifu hawezi kukiri ni mhalifu kirahisi, si ndio?

Lakini nilichogundua ni kwamba kuna patterns flani utazisikia kwa matajiri wengi; kukwepa kodi, kutakatisha fedha, kutumia milango ya siasa nk
Mfano niliwahi kusikia mo alitumia connections zake za kisiasa kununua makampuni kwa bei ndogo kipindi cha mkapa
Au kuna hii taarifa ya rostam kutaka kutawala sekta ya madini kwa kulazimisha makampuni yamuuzie hisa nyingi

Hizo njia za kihalifu pia ni ngumu, kwahiyo kazi kazi usidhani kuna kitonga popote. Ukifanya uhalifu unarisk kunyea ndoo.

Pia nasikia kuna kiwango cha utajiri unaweza pata kwa njia halali, na kuna kiwangi ambacho huwezi kukipata bila kuwa mhuni, ila sijui ni viwango gani.

Na mpaka ufikie hiyo level ya kutakatisha hela, kutumia wanasiasa, maana yake unazungusha hela kubwa kwahiyo hapo nyuma kuna kamsoto ka kuanzia.

Sema asilimia kubwa ya matajiri huwa wametoka kwenye familia zenye uwezo...

Ukifuatilia jinsi wamarekani wanavyowachukulia billionaires nchini kwao utaelewa zaidi
Mkuu samahan IVi ni Kweli, kwenye vituo vya police ya TZ, mahabusu Bado wananyea ndoo AU debe,
 
Ni kwasababu mara nyingi utajiri wameupata kwa njia za panya, yaani kihalifu

Mhalifu hawezi kukiri ni mhalifu kirahisi, si ndio?

Lakini nilichogundua ni kwamba kuna patterns flani utazisikia kwa matajiri wengi; kukwepa kodi, kutakatisha fedha, kutumia milango ya siasa nk
Mfano niliwahi kusikia mo alitumia connections zake za kisiasa kununua makampuni kwa bei ndogo kipindi cha mkapa
Au kuna hii taarifa ya rostam kutaka kutawala sekta ya madini kwa kulazimisha makampuni yamuuzie hisa nyingi

Hizo njia za kihalifu pia ni ngumu, kwahiyo kazi kazi usidhani kuna kitonga popote. Ukifanya uhalifu unarisk kunyea ndoo.

Pia nasikia kuna kiwango cha utajiri unaweza pata kwa njia halali, na kuna kiwangi ambacho huwezi kukipata bila kuwa mhuni, ila sijui ni viwango gani.

Na mpaka ufikie hiyo level ya kutakatisha hela, kutumia wanasiasa, maana yake unazungusha hela kubwa kwahiyo hapo nyuma kuna kamsoto ka kuanzia.

Sema asilimia kubwa ya matajiri huwa wametoka kwenye familia zenye uwezo...

Ukifuatilia jinsi wamarekani wanavyowachukulia billionaires nchini kwao utaelewa zaidi
Umeeleza vema mkuu
 
Hata wewe ukitoboa utasema ulikua unalala njaa. Mo alisema alikua anaenda shuleni peku ila kasoma IST.

Bakhressa alianza kuuza ukwaju Leo ana viwanda. Wewe ukianza kuuza ukwaju Leo hadi unakufa hununui hata vitz.
Na wewe ukifanikiwa utatuambia ulikuwa unatembea kilometres 10 kila siku kuuza mboga za majani leo ni billionea 🤣🤣🤣
 
Wasalam wakuu,

Imekuwa ni jambo la kawaida matajiri wakihojiwa kuhusu utajiri wao utasikia anasema nilianza na baiskeli sasa
namiliki kampuni kubwa ya mabasi. Mwingine atasema nilianza mama ntilie leo namiliki hoteli kadhaa mjini, mwingine anasema nilianza kushona viatu ila sasa na miliki kiwanda cha viatu, mara nilianza na mtaji wa 20,0000 sasa nina billion 5.

Wanaeleza mambo kana kwamba ni mepesi sana na baadhi ya vijana wasio fikirisha akili yao vizuri wana chukua kama ilivyo wana hamasika wana enda kupambana bila mafanikio, matokeo yake wanakata tamaa zaidi. Jamani kama alivyo wahi sema Mh raisi mstaafu Jakaya Kikwete kwamba akili za kuambiwa changanya na za kwako hii ni muhimu sana.

Nyie mna mtizamo gani ndugu wanabodi.
Ambao sio ukweli ni upi hapo?
 
Wasalam wakuu,

Imekuwa ni jambo la kawaida matajiri wakihojiwa kuhusu utajiri wao utasikia anasema nilianza na baiskeli sasa
namiliki kampuni kubwa ya mabasi. Mwingine atasema nilianza mama ntilie leo namiliki hoteli kadhaa mjini, mwingine anasema nilianza kushona viatu ila sasa na miliki kiwanda cha viatu, mara nilianza na mtaji wa 20,0000 sasa nina billion 5.

Wanaeleza mambo kana kwamba ni mepesi sana na baadhi ya vijana wasio fikirisha akili yao vizuri wana chukua kama ilivyo wana hamasika wana enda kupambana bila mafanikio, matokeo yake wanakata tamaa zaidi. Jamani kama alivyo wahi sema Mh raisi mstaafu Jakaya Kikwete kwamba akili za kuambiwa changanya na za kwako hii ni muhimu sana.

Nyie mna mtizamo gani ndugu wanabodi.

1. Niffa alianza na elfu 40
2.Shamim Zeze Alianza na elfu 10
3.Super Feo alianza na ELfu 20
4.Dotto Magari alianza na mtaji wa mia 5 ya bando
5.Issa Tambuu alianza na mtaji wa elfu 50.
6.Bakresa alianza na kushona viatu
7.Mo alianza na mtaji wa usd 1m.
8.Musukuma alianza na mtaji wa afu thalathini.
9.Kishimba alianza na mtaji wa afu 6.
10.Vunja Bei alianza na mkopo wa milioni 3.
 
1. Niffa alianza na elfu 40
2.Shamim Zeze Alianza na elfu 10
3.Super Feo alianza na ELfu 20
4.Dotto Magari alianza na mtaji wa mia 5 ya bando
5.Issa Tambuu alianza na mtaji wa elfu 50.
6.Bakresa alianza na kushona viatu
7.Mo alianza na mtaji wa usd 1m.
8.Musukuma alianza na mtaji wa afu thalathini.
9.Kishimba alianza na mtaji wa afu 6.
10.Vunja Bei alianza na mkopo wa milioni 3.
Alhamduli:Llah Bakhressa nalifahamu mpaka duka lake aliloanza nalo la viatu.

Kishimba nafahamu duka leke Mwanza na Mzee aliekuwa anamkopesha bidhaa za kuweka dukani namfahamu.

Kishimba ni mtu mwaminifu sana. Hilo nalifahamu sana.

Bakhressa ni mtu ambae kawanyanyua kimaisha wale waaminifu wote ambao kaanza nao kazi, wengine na wao ni matajiri sasa, wengine wana hali nzuri, wengine wanalalamika kama kawaida ya binadam, Wengine hawataki hata kumsikia, wanasema hakuna bahili duniani kama yeye.


Ili mradi binadam duniani hatukosi kasoro.
 
Alhamduli:Llah Bakhressa nalifahamu mpaka duka lake aliloanza nalo la viatu.

Kishimba nafahamu duka leke Mwanza na Mzee aliekuwa anamkopesha bidhaa za kuweka dukani namfahamu.

Kishimba ni mtu mwaminifu sana. Hilo nalifahamu sana.

Bakhressa ni mtu ambae kawanyanyua kimaisha wale waaminifu wote ambao kaanza nao kazi, wengine na wao ni matajiri sasa, wengine wana hali nzuri, wengine wanalalamika kama kawaida ya binadam, Wengine hawataki hata kumsikia, wanasema hakuna bahili duniani kama yeye.


Ili mradi binadam duniani hatukosi kasoro.

Ni kweli unayoyasema ila behind the scene na ku-make fortune si viatu wala maduka yao!! SSB anatajwa sana kwenye poaching ,Musukuma udhulumati wa madini ,kishimba anatajwa sana kurun bizness za Vigogo wa serikali kwa kupitia jina lake kwakuwa ni muaminifu hapo hapo na yeye akajiongeza.

Kuna jamaa mmoja maeneo flani alikuwa ana duka tu kubwa la nguo anatoka kanda ya kaskazini ,alikuwa pia ana duka genge ,anauza mkaa ,maji na vitu vingi vingi ,lilijaza balaa akajenga nyumba mbili enzi hizo tulikuwa tunaita "SEFU KONTENA" ,jioni alikuwa anasema anafanya kazi ulinzi kumbe behind the scene alikuwa "MANDONGA MTU KAZI SHOW SHOW aka MZEE WA MJEGEJE" ilikuja kubainika baada ya kushikwa kwa ujambazi....Kwahiyo kuna baadhi ya watu wanafanya biashara front kucover ufirauni wao wa nyuma.
 
NbxHuyo Mungu Alishindwa na Anashindwa kuwapa hata chakula Maelfu ya watoto, waake na wazee wanaokufa kwa njaa wakilia na kumuomba awasaidie,

Halafu ndio unasema huyo Mungu anagawa utajiri?

Utajiri gani
View attachment 30783855
Kwa hiyo kiongozi uamini kuwa dhahabu na kila kitu hata wewe mwenyewe unatoka kwa Bwana.?

Naye Bwana Mungu ndiye mgawaji wa riziki.
 
Wasalam wakuu,

Imekuwa ni jambo la kawaida matajiri wakihojiwa kuhusu utajiri wao utasikia anasema nilianza na baiskeli sasa
namiliki kampuni kubwa ya mabasi. Mwingine atasema nilianza mama ntilie leo namiliki hoteli kadhaa mjini, mwingine anasema nilianza kushona viatu ila sasa na miliki kiwanda cha viatu, mara nilianza na mtaji wa 20,0000 sasa nina billion 5.

Wanaeleza mambo kana kwamba ni mepesi sana na baadhi ya vijana wasio fikirisha akili yao vizuri wana chukua kama ilivyo wana hamasika wana enda kupambana bila mafanikio, matokeo yake wanakata tamaa zaidi. Jamani kama alivyo wahi sema Mh raisi mstaafu Jakaya Kikwete kwamba akili za kuambiwa changanya na za kwako hii ni muhimu sana.

Nyie mna mtizamo gani ndugu wanabodi.
Ilimasikini muendelee kuwepo
 
Kwa hiyo kiongozi uamini kuwa dhahabu na kila kitu hata wewe mwenyewe unatoka kwa bwana.? Naye ndio mgawaji wa ridhiki.
Kwanza siamini kwenye kuamini. Sina imani ya aina yeyote ile.

Huyo Bwana hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Hakuna mtu au kitu chochote kilichotoka kwa huyo Bwana.
 
Mtu anasema alianza kwa mtaji fulani, wewe unabisha! Sasa unataka akuambie nini?

Wafanyabiashara wengi huanzia chini sana, ila character zao ndiyo huwajenga kibiashara mpaka wanakuwa na mafanikio makubwa.

Watu wasio wafanyabiashara hudhani mpaka uwe millionea ni uanze na mamilioni.. hawawezi ku-imagine process nzima ya kutoka chini kwenda juu, so huishia kusema wanadanganywa.
 
Ni kweli unayoyasema ila behind the scene na ku-make fortune si viatu wala maduka yao!! SSB anatajwa sana kwenye poaching ,Musukuma udhulumati wa madini ,kishimba anatajwa sana kurun bizness za Vigogo wa serikali kwa kupitia jina lake kwakuwa ni muaminifu hapo hapo na yeye akajiongeza.

Kuna jamaa mmoja maeneo flani alikuwa ana duka tu kubwa la nguo anatoka kanda ya kaskazini ,alikuwa pia ana duka genge ,anauza mkaa ,maji na vitu vingi vingi ,lilijaza balaa akajenga nyumba mbili enzi hizo tulikuwa tunaita "SEFU KONTENA" ,jioni alikuwa anasema anafanya kazi ulinzi kumbe behind the scene alikuwa "MANDONGA MTU KAZI SHOW SHOW aka MZEE WA MJEGEJE" ilikuja kubainika baada ya kushikwa kwa ujambazi....Kwahiyo kuna baadhi ya watu wanafanya biashara front kucover ufirauni wao wa nyuma.
Ni kweli kabisa kama ulivyo eleza kwa kina kuwa mtu anaweza kuwa alianza na mtaji anao sema ila process hapo

katikati ya kumfanya awe alivyo sasa kimafanikio ndio zinawekwa sirini ndio tuna shauri vijana wapambane kwa uwezo wao wasiamini sana story zao.
 
Ni kwasababu mara nyingi utajiri wameupata kwa njia za panya, yaani kihalifu

Mhalifu hawezi kukiri ni mhalifu kirahisi, si ndio?

Lakini nilichogundua ni kwamba kuna patterns flani utazisikia kwa matajiri wengi; kukwepa kodi, kutakatisha fedha, kutumia milango ya siasa nk
Mfano niliwahi kusikia mo alitumia connections zake za kisiasa kununua makampuni kwa bei ndogo kipindi cha mkapa
Au kuna hii taarifa ya rostam kutaka kutawala sekta ya madini kwa kulazimisha makampuni yamuuzie hisa nyingi

Hizo njia za kihalifu pia ni ngumu, kwahiyo kazi kazi usidhani kuna kitonga popote. Ukifanya uhalifu unarisk kunyea ndoo.

Pia nasikia kuna kiwango cha utajiri unaweza pata kwa njia halali, na kuna kiwangi ambacho huwezi kukipata bila kuwa mhuni, ila sijui ni viwango gani.

Na mpaka ufikie hiyo level ya kutakatisha hela, kutumia wanasiasa, maana yake unazungusha hela kubwa kwahiyo hapo nyuma kuna kamsoto ka kuanzia.

Sema asilimia kubwa ya matajiri huwa wametoka kwenye familia zenye uwezo...

Ukifuatilia jinsi wamarekani wanavyowachukulia billionaires nchini kwao utaelewa zaidi
Hii ya kutakatisha pesa matajiri wanatumia sana ila siamini katika utajiri wa masharti kama ipo ni nafasi ndogo sana
 
Back
Top Bottom