Nipo Zambia, kila Mzambia ananiulizia habari za Rais Magufuli

Nipo Zambia, kila Mzambia ananiulizia habari za Rais Magufuli

Tueleze vizuri na soko la soya liko reliable kiasi gani na margin yake ikoje ukizingatia unafanya mzunguko mkubwa sana kuanzia kuikusanya, kusafirisha mpaka imfikie mnunuzi wa mwisho ambae ni exporter
 
JPM lilikuwa jembe!
Wao wanaamini waliibiwa votes, 2020 ni mwendawazimu tu ndo ulikuwa huwezi mpigia kura JPM, na tulipiga sababu tulitaka Rais "mnyooshaji".

wamekesha wakimtukana na mama akaingia mkenge akawafata wakati wao walikuwa wanajua wanachokifanya, wanajua JPM yuko na wapiga kura wengi na kudhihakiwa kwake bila serikali kuchukua hatua wapiga kura watapiga kura za hasira, sasa, mama kastuka, na asipowashughulikia hao walohusika na hiyo saga ilotubadirishia uongozi bila aibu tutaelewana mbele...WANAJULIKANA.
 
Waambie alikufa, alishaoza, alishasahauliwa na sasa tunarekebisha uchumi, tunarudisha mahusiano kimataifa, umoja wa taifa na tunapambana na covid-19 kisayansi kulingana na protocol zaWHO.
 
JPM ni gumzo kwa wenzetu kuanzia Nakonde Region, Kitwe, Ndola, Kapimposhi, Mkushi, mpaka Lusaka JPM ni gumzo
Aiseee,

Wewe bado unamkumbuka JPM, habari ya mjini sasa hivi ni SSH.

Anza kujifunza kuimba wimbo huo.

Watu wengine bwanah, sijui wanaishi dunia ya wapi!
 
NIPO ZAMBIA,KILA MZAMBIA ANANIULIZIA HABARI ZA RAIS MAGUFULI.

Nipo Zambia now kununua Soyabeans,JPM anakubalika vibaya mno (kumbuka tenda ya kuuza Soyabeans alituombea JPM mwezi Wa 12 mwaka Jana kwa Waziri Wa mambo ya nje Wa China alipozuru Tanzania- ambapo China ilikubali kuijumuisha Tanzania kama muuzaji Wa Soya bean kwao na kwa Africa zimepewa tenda hiyo nchi tatu tu Tanzania, Ethiopia na Benin na kwa mwaka inatakiwa kuiuzia China tani milioni tatu hivyo sababu sisi hatulimi soya kwa sana JPM alituombea kwa Zambia na Malawi waturuhusu watz kufata soya huko,Pia JPM alituombea soko la kuiuzia Soya na Ufuta nchi ya India lakini sababu watanzania ni wazembe fursa hizo zimechangamkiwa na wakenya,wakenya ndo wamejaa huku).

..last week nilikosea mpaka-sheria ya Zambia mwisho kwa Watanzania kufanya biashara na shughuli zao pale Zambia ni SAA tatu usiku vinginevyo uwe na vibali,so sikujua makazi tumeweka Tunduma boda majuzi nikatoka kwenda kutembea nikakamatwa nilipofikishwa kituo kidogo cha police pale nakonde nikahojiwa kisha nikapelekwa kituo kikubwa Nakonde Police Central ni kama Oysterbay police au central police watuhumiwa walikuwa wengi mno waethiopia,wasomali,wanyarwanda na wengine cha kushangaza Police walipokuwa wanachukua Maelezo yangu wakagundua kuwa kuwa Mimi ni MTz wenyewe wanatuita "waswahili"(waliniachia baada ya kunipa kosa la Shishita nasio migration case)

Wakaanza kuniuliza habari za JPM huku wakimponda President wao Mr Edgar Lungu wenyewe wanamfananisha JPM na marais wao wazamani Marehemu Sata na Mwanawasa wengine Kaunda,rupia banda,chiluba wanadai walikuwa wezi na walijenga kwenye nchi zao "kumbuka Zambia inadaiwa haijawahi kuongozwa na mzawa"wazambia hata ukikakaaa nao mitaani wakigundua wewe ni mtanzania story zao ni kumsifia JPM hata boda ya Tunduma upande Wa Tanzania na Zambia aliijenga kisasa yeye na mpaka lami akaweka Hadi Zambia ila lungu akashindwa kumalizia, wenzetu Hadi mahabusu,saloon,machinga,mamalishe wanafatilia siasa huwaambii kitu kuhusu JPM na hii nimeikuta pia Malawi pia kwenye Soya kuanzia Kasumulo boda Hadi Malawi.

Wamalawi wanamkubali rais wao mmoja tu Marehemu Bingu Wa Mutharika wao wanaamini aliuawa kwa sumu na wazambia pia wanaamini Dr.Levy Mwanawasa na Michael Sata waliuawa kutokana na misimamo yao.

JPM ni gumzo kwa wenzetu kuanzia Nakonde Region, Kitwe, Ndola, Kapimposhi, Mkushi, mpaka Lusaka JPM ni gumzo
Kwamba hawajui habari zake au wanatukebehi tu
 
Mkuu unasema kweli kwamba uko Zambia ..vip hyo soya inapatikana kweli je vip mtaji unoitajika ili kutrase na hyo biashara ..na mteja gani anaiitaji mizigo
 
Kuna watu wataumia kusikia hili

Aendelee kupumzika kwa amani Shujaa, Mwamba na Rais wa karne[emoji120]
Mtendee haki huyo mama uliyemueka profile anaheshimika sana kwenye ulimwengu wa hiphop na rnb
 
Hao watumishi wa Mungu walikuwa na miguu minne nini! Eti kufufuka, Kufufuka? Labda njozini, kifo hakina breki budah, endelea kukariri.
walikuwa na miguu miwili.. but hawakuteulwia kwa miguu.. Mungu aliwaweka special.. but not Magufuli.

kama angekuwa immortal angekuwa hai, probably angekuwa na direct line na Mungu.. but nooooo all that didnt happen.
why?

because he is not ,stop overrating dead man... he is not coming back
 
Yesu alisema hata nyote mkikaaa kimya mawe yatapaza sauti [emoji4] falsafa nzito sana hii
 
Waambie alishakuwa mwendazake.

Kumbuka hata hapa bongo miaka hadi ya 2000 kuna watanzania wengi wa vijijini walikuwa wanajua nyerere yupo hai wakati alishafariki
Itakuwa wapo Kama hao watanzania wa kipindi hicho.

Watakuwa hawafatilii mambo ya siasa Kama ulivyowasifia ,au utakuwa unatudanganya

kama ni ivo basi ujue anakaa ndan ya watu sana na ni kitu kizuri
 
kama ni ivo basi ujue anakaa ndan ya watu sana na ni kitu kizuri
Hakuna uzuri wowote sanasana inaonekana hiyo jamii ni ya watu duni sana ambao hawana hata access ya mawasiliano kujua dunia inaendaje kitu ambacho sio kizuri.
Yaani mtu kafa halafu watu hawana taarifa wanaendelea kumuongelea as if hajafa.
Kwenye kabila letu ikitokea mtu amekufa halafu mtu akamuulizia kwa sababu kwa bahati mbaya alikuwa hafahamu Kama alishakufa inaonekana Kama ni uchuro flani hivi
 
Duu mkuu m tz ulikuwa wewe peke yako Ila mataifa mengine kibao kwenye utafutaji.
Mie nachoaamini hatuna shida bado Mana uhakika wa kula upo
 
Wengi wanamkubali kwasababu ya msimamo wake dhidi ya korona. Walakini hawajui kama alikuwa mwonevu, mtesaji na mwovu kuliko yeyote aliyemtangulia.

Haya tunayajua sisi humu Tanzania.
Huko nje wanasikiliza tu lakini hawaishi Tanzania. Ndiyo maana nawaambia wanaomsifia Gadafi kuwa walipaswa kuishi kama raia wa Libya ili kumfahamu Gadafi vizuri.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Ni kama ambavyo kuna watu wanammiss Idi amini.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Wewe ni kinda, usifananishe Idd Amini na JPM. JPM alikuwa mjenga nchi na idd Amini alikuwa ni laghai tu. Mfano mmoja ni jinsi alivyorejesha fedha kutoka kwa elite na kuzitumia kuendeleza infrastructure bila kuongeza kodi kwa walalahoi. Huwezi kuona sasa hadi mwaka upite ndipo tutakuwa tunaongea lugha moja nchi itakavyokuwa hohehae
 
Back
Top Bottom