Asante sana. NMB siku hizi kila penye tawi lenu CRDB wanakuja kwa kazi na ni kipenzi cha watu wengi wakiwemo wafanyabiashara. mm niko Bunda mkoani Mara ambapo CRDB wanajenga tawi kwa kasi. naomba pale customer care kuna wasichana wawili ukiacha yule dada anayeitwa Agnes. wale wawili ni wapuuzi sana kiasi cha mimi kushindwa kufanya shughuli zangu pale. wanajiona kama miungu watu. hawajui thamani yetu na pesa zetu. walahi msipokuwa makini CRDB ikianza kazi mtatukisa wengi. castomer care ni weledi na si kila mtu anatakiwa kuwa pale. waondoeni wale wasichana au wapewe elimu na Agnes namna ya kusikiliza na kuhudumia wateja. Inauma sana kuweka watu wanaoangalia sura za watu ndo wawahudumie. ni hayo tu na nategemea mabadiliko NMB Bunda mkoani Mara.