NMB Tanzania Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri

NMB Tanzania Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri

Sikufikiria kama benk yetu inafika mpaka huku hongereni benk inayowafuata wateja wake popote walipo.

Mpaka sasa sijawahi kupata tatizo lolote katika huduma zenu kupitia matawi ninayoyatumia
 
Naomba kujua juu ya BONUS ACCOUNT
Faida yake
Unaweza jua salio
Unaweza toa pesa kabla ya mwaka
Mwaka utaisabiwa vp toka mwez uliojiunga kwa miez 12
 
Asante sana. NMB siku hizi kila penye tawi lenu CRDB wanakuja kwa kazi na ni kipenzi cha watu wengi wakiwemo wafanyabiashara. mm niko Bunda mkoani Mara ambapo CRDB wanajenga tawi kwa kasi. naomba pale customer care kuna wasichana wawili ukiacha yule dada anayeitwa Agnes. wale wawili ni wapuuzi sana kiasi cha mimi kushindwa kufanya shughuli zangu pale. wanajiona kama miungu watu. hawajui thamani yetu na pesa zetu. walahi msipokuwa makini CRDB ikianza kazi mtatukisa wengi. castomer care ni weledi na si kila mtu anatakiwa kuwa pale. waondoeni wale wasichana au wapewe elimu na Agnes namna ya kusikiliza na kuhudumia wateja. Inauma sana kuweka watu wanaoangalia sura za watu ndo wawahudumie. ni hayo tu na nategemea mabadiliko NMB Bunda mkoani Mara.

Mromboo, NMB Bunda inakera sana kama akina dada wengine wanajiona mno.
Biashara nzuri ni customer care. Dada anna alinihudumia vizuri sana she knows why she's there.
Hapa Bunda CRDB wanajenga tawi karibu na kituo cha polisi Bunda mjini.
 
Last edited by a moderator:
Mkoa mzima wa Rukwa ATM 3 ambazo zimetegwa manispaa ya sumbawanga, na huwezi ukakuta zote zinafanya kazi lazima moja iwe imecease, hii ni kero kubwa kwa wakazi wa rukwa. Tazameni hilo
 
Songea mkoani ruvuma kuna mashine za ATM zaidi ya tatu lakini muda mwingi utakuta zinafanya kazi mbili au moja munakera sana NMB ukifika Ruangwa lindi utakuta madirisha ya huduma yako mawili lakini utakuta kila siku linafanya kazi dirisha moja hata iwe foleni namna gani
 
Asante NMB, mie ni mteja wenu, ningependa kujuwa kwa kiini, mikopo kwa wafanyabiashara kama "Mortgage", uzuri mimi na mwenzangu tunayo security ya kutosha kuweka kwa ajili ya huu mkopo, naomba nijuwe riba, grace days, kama inawezekana kukopa na kurudisha baada ya miaka 10, documents mzitakazo, na malipo ya kila mwezi kwa mioaka yote kumi..
Asante
 
Tatizo langu NMB kuna tawi lenu moja mnalisahau sana kila siku halina pesa yani toka nimeanza kupita ile njia nimewahi bahatika pesa mara moja tuuu siku zote hakuna pesa nashindwa kuelewa ni kwa nn NMB ATM YA UHASIBU (T.I.A)

kwa kawaida najua mliweka pale kupunguza foleni ya watu kwenda uhamiaji kule na temeke pale JIRAF HOTEL ambapo bado huwa na foleni kubwa sana kutokana na kukosa pesa pale uhasibu.

Eneo lile na ATM ile ingepaswa kuwa na pesa wakat mwing na kukumbukwa mara kwa mara kutokana eneo lile lina watu weng sana na wengiwao ndo benki yao ya matumizi pembeni pale kuna kambi ya jeshi TWALIPO ambayo wafanyakazi hawa hulipwa kupitia NMB ni wengi sana haya hapo hapo kuna wanafunzi wa chuo cha uhasibu hapo weng tu pia wote hutegemea kupata huduma apo apo bado kyna watu mbali mbali ambao huingia kwenye maduka ya jeshi wote hutaka pesa pale kuna wapita njia pia hupenda kupata pesa pale lakin nasikitika kuona waka hamna muda kabisa na benki hii kwa nn????

Nawasilisha kwenu
 
...nmb sometims unabore saaana...nlifunguaga akaunt moshi..nelson mandela branch yr 2008...den after shule nlihamia dsm as kikaz zaid...atm yangu ili x pire....nlifuatilia nipewe ingine via ilala branch ila mnazingua miez mitatu ikaisha et atm mpya ipo moshi....kuileta imekuwa issue.....badiliken maana mpaka leo kimnya...mnaringa mtadhan bank n yenu pekeenu...nlishahama na nahamasisha wengine wahame hamna msaada kwa sisi jamii ya kawaida.......
 
...nmb sometims unabore saaana...nlifunguaga akaunt moshi..nelson mandela branch yr 2008...den after shule nlihamia dsm as kikaz zaid...atm yangu ili x pire....nlifuatilia nipewe ingine via ilala branch ila mnazingua miez mitatu ikaisha et atm mpya ipo moshi....kuileta imekuwa issue.....badiliken maana mpaka leo kimnya...mnaringa mtadhan bank n yenu pekeenu...nlishahama na nahamasisha wengine wahame hamna msaada kwa sisi jamii ya kawaida.......

Daaah afu swala la kusafirisha kadi kwa nmb ni big problem duu.

Nakumbuka tulikuwa arusha tulifungua account zetu pale na jamaa yangu mmoja iv asa tulipokuja mjini kikaz kadi ya mwenzangu ikawa haisomi pesa hadi achukulie dirishani alipowaambia atengenezewe kadi nyingne wakasema wameituma arusha jamaa yangu alikuwa kapata potya kwenda nje alitaka apate kadi awaachie wazazi wake waendelee kutumia lakin tumefuatilia kwa miez kama minne iv bila mafanikio....na hadi sasa hajaipata iyo kadi ye yupo russia..

Kuweni makini bwana
 
Nina swali la kuwauliza wahusika ni hivi?

Kama nimerejesha marejesho yote tena kwa muda kabla ya tarehe siku mbili nyuma, nimemaliza mkopo wangu salama je ni kwanini Ofisa wangu wa benki amekataa kunipa mkopo mwengine na sababu za msingi ansema nilikua sizungushi akaunti?

Je hili suala la kuzungusha akaunti limo katika mkataba wa mkopo wa awali ambalo mteja anatarifiwa kabla ili ajiandae? Na kama halimo inakuaje kwa ofisa kama huyu hatua gani achukuliwe?

Hili limemkuta mteja wenu ambae ni rafiki yangu

Ahsante

Kwa upande wangu nina masikitiko makubwa sana nimeanza kukopa NMB miaka kumi iliyopita tangu niko kijijini mpaka sasa nimehamia mjini sijawahi kuchelewesha hata marejesho ya mwezi mmoja lakini inasikitisha bado benki haijaweza kunisaidia kupata mkopo wa kuniwezesha nikaweza kuendeleza biashara zangu kwa kujali kuwa mimi ni mteja wa muda mrefu na wa kuamini mpka leo bado sijajiweza kimaisha.

Ahsante
 
Admins Fungeni hii thread haina maana, kama wamefngua humu dawati la huduma kwa mteja halafu wanashndwa kufuatlia na kutoa majibu kwa maswali wanayouliza inaonesha huduma zao ni mbovu tu!
 
Admins Fungeni hii thread haina maana, kama wamefngua humu dawati la huduma kwa mteja halafu wanashndwa kufuatlia na kutoa majibu kwa maswali wanayouliza inaonesha huduma zao ni mbovu tu!

Kweli kabisa tunaandika apa afu no majibu kwaiyo wanatuona sie waoimbavu tuuu
 
Tar 15.12.2014 nilienda kufungua account kwa ajiri ya mshahara wangu makambako njombe mimi ni mgeni nilikuwa nimetoka bukoba na kule sina ndugu nilifikia guest nisiende mbali uko cha ajabu nimepewa barua ya utambulisho kutoka kwa mkurugenzi ya almashauri ikinitambulisha kuwa mimi ni mfanyakazi mpya na wanisaidie kufungua accoount NMB ila bahati mbaya sikufanikiwa sababu nilizoambiwa siwezi kufungia account ni kwamba niwe na kitambulisho cha kazi au barua ya mtendaji kwamba iyo barua ya mkurugenzi wao hawaitambui.

nikajaribu kuwaambia mimi ndio naanza kazi kama barua yangu inavyosema na kitambulisho ntapata baadaye ila nikakataliwa nikaambiwa niende kwa mtendaji, sasa nikawauliza mtendaji atanipaje barua wakati mimi si mkazi wa makambako?

Mana nilazima nitoke na barua kwa mjumbe inayonitambulisha kuwa mimi ni mkazi wake, ila wakanikatalia kabisa, swali langu ni kwamba kwanini mnafanya kazi kizamani sana?

Nilitoa kitambulisho cha kupiga kura nacho akikutosha mpaka barua ya mtendaji ili hali nina barua ya mkurugenzi wa manispaa akinitambua, nilikasirika nikaenda CRDB nimefika sijachujua hata dk 5 nimemaliza kufungua account.

kitu kingine kwenye mshahara mnafanya maksudi kuamisha pesa kwenda CRDB ili tuame CRDB tuje NMB wakati uko mna masharti mengi kama vile unaomba uraia , acheni izo na mbadilike
 
hawa jamaa wa nmb wameingia mitini! mbona hawajibu maswali yetu?
 
Two times cheque zangu zinabounce, nikipiga simu makao makuu mnasema nenda kwenye branch yako wakati mtu wakati huo yuko Mkoa na branch liko Dar. This is disgusting.

Inabidi mtu anapopiga HQ nyinyi ndo muwasiliane na mteja na mumwambie tatizo. Hii ni karne ya 21, communication is very simple and you make it complex. You make me sick.
 
Nimepotelewa na ATM CARD yangu mwezi wa2 sasa na taarifa nilishatoa na form nimejaza zote nilimfungulia acc NMB MSASANI BRANCH but kwa sasa nipo dodoma kikaz nahuku ndipo card ilipo potelea kila nikifuatilia naambiwa wametuma e mail mara nyingi huko msasani branch lakin hazijibiwi zinapuuzwa, na nikuenda dirishan kuchukua pesa naambiwa hawaoni picha!!

Mbona utaratibu ni mbovu saana cjapenda huduma za namna hii
 
Haina haja ya kupost kitu hapa... tangu wamefungua had leo kimya....nn maana yake..?
Mods fungeni nii thread
 
Ndugu wana JamiiForums,

Tunashukuru kwa maoni yenu mliyoweka hapa juu ya huduma mnazo pata kwenye matawi yetu nchini kote, NMB inafanyia uchunguzi maoni na malalamiko yenu na tuna wahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki dhidi ya wafanyakazi waliotajwa na wengine wenye tabia kama hizo.

Ndugu wana jukwaa, NMB inajipambanua kwa kusimamia maadili moja wapo ikiwa ni uaminifu kwa wafanyakazi wake.
NMB pia inapenda kuwa hakikishia wateja na jamii kwa ujumla kwamba itaendelea kusimamia sera zote za benki ikiwa ni pamoja na kutovumilia wafanyakazi wasio waadilifu.

Kama kutatokea umepata huduma isiyo ridhisha au ufanyaji kazi usiofuata maadili, uaminifu na uadilifu, tafadhali toa taarifa kupitia njia zifuatazo:

1. Kupitia tovuti: http://www.nmbtz.com
2. Kupitia e-mail maalumu: whistleblower@nmbtz.com
3. Kwa posta – Unaweza kutuma barua kwa Afisa Mtendaji kama ifuatavyo:

Afisa Mtendaji Mkuu (Bahasha iandikwe "Siri")
Makao Makuu ya NMB,
P. O. Box 9213,
Azikiwe/Jamhuri Street,
Dar es Salaam, Tanzania.

4. Au kwa kupiga simu zifuatazo:
0658 751 000 Tigo
0779 751 000 Zantel
0685 751 000 Airtel
0800 751 000 Vodacom
Ninaweza kupata salary loan topup,mar ya mwisho nilikopa february mwaka jana?Kwenye web yenu inaonyesha unaweza fanya topup baada ya miezi sita,but hapa singida nmb wakasema hadi mwaka.

Huu mkanganyiko unatuchanganya wateja
 
Back
Top Bottom