Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na Samia, yupi Rais bora kwako?

Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na Samia, yupi Rais bora kwako?

Labda unachanganya neno “relative” na reletivity theory ni vitu viwili tofauti, ninaposema jambo xyz ni relative namaanisha kwamba inategemea na jinsi unavyoona au kwa maana nyingine kila mtu ana mtazamo wake ndiyo maana ya kusema jambo fulani ni relative na hakuna uhusiano wowote ule na Einstein, …
Sasa wewe nawe unatuchosha. Nadharia ya "Relativity" si inatokana na hali ya kuwa "Relative"? Unakataaje ulichokisema kuwa hakihusiani na hiyo nadharia wakati maelezo yako ndiyo yanaonesha ulikuwa unamaanisha hiyo nadharia!!?
 
Wakati wa Nyerere hata walipotea wengi zaidi kuliko kipindi kingine chochote kile wala usitake kwenda huko kufungua makabrasha, …
Fungua hayo makabrasha na uwataje waliouawa na kupotea wakati wa Nyerere. Kuna ubaya gani ukiyafungua!!??
 
Haya nani alimuua Mwangosi pale Iringa kwa risasi na utumbo nje? Nani alihusika ?Nani aliyemteka Kiongozi wa madaktari na kumtesa?
Hukuziona picha za jinsi Mwangosi alivyouawa?? Sema tuna mahakama kibogoyo ndiyo maana haki haikutendeka. Aliyemteka Dr. Ulimboka na kumpeleka Mabwe Pande hukusikia akitajwa wakati ule? Usijaribu kusawazisha uovu kwa kutaja uovu wa watu wengine.

1666513097006.png

Dr.Stephen Ulimboka mara tu baada ya kuokotwa maeneo ya Mabwe Pande!!
 
Wote wabovu tu.

Nasema wote wabovu kwasababu makosa yao ndio yameleta matatizo makubwa na kuletea watu umasikini mpaka leo, kifupi makosa yao ndio yameamua mustakabari mbovu.

JK NYERERE - alishindwa kujenga mfumo imara wa maisha ambao ungetumika kuinua maisha ya watanzania milele, kuukumbatia ujamaa ulioshindwa akiamini angeweza kuutumia na kuleta tija ndio chanzo cha matatizo mengi mpaka leo.

AH MWINYI: aliipokea nchi ikiwa imechoka na kuchakaa na matatizo mengi kutoka kwa JK NYERERE, sera yake ya Ruksa na kukumbatia mabepari bila udhibiti kuliigeuza nchi danguro na kuharibu kabisa mifumo ya maisha.

BWM : Huyu sera yake ya ubinafsishaji wa mashirika ya umma bila udhibiti imara ulileta matatizo makubwa ambayo yataendelea kuitafuna nchi milele milele. Kupitia ubinafsishaji kuna jamii ziliutumia mwanya huo na kuishia kuifirisi nchi na ndio ikawa chanzo cha ufisadi mpaka leo.

JK: Huyi alitaka kuleta modern style of management kwa kuwatawala watanzania kwa kufuata basics za uongozi bila kujua anaongoza majitu majinga na mapumbavu matokeo yake alisababisha matatizo makubwa ya wizi na ufisadi usio na kikomo, makosa haya yanaigharimu nchi mpaka leo.

JPM: Binafsi namuita mwamba, huyu makosa yake makubwa ni kutoijua siasa ya dunia na kuamini kwenye theory, Theory aliyosoma darasani na historia za viongozi wapigania uhuru zilimuharibu ubongo wake. Matokeo yake akajikuta anakwenda kupiga pua chini na kuiacha nchi hohehahe.
Kuwa muumini wa ujamaa ambao ukweli pia hakuujua vizuri zaidi ya theory za shule, kujaribu kupractice ujamaa karne ya 21 kwenye nchi ambayo haina msingi wa chochote.

MWISHO KABISA, KILA KITU KINAANZIA KWENYE BASICS, BASICS KWENYE DUNIA HII NI KUWAPA WATU MAARIFA BORA NA SAHIHI... HAO WOTE HAKUNA ALIYEWEZA KUWEKA MAZINGIRA BORA KWA WATU KUPATA MAARIFA SAHIHI NA KUYATUMIA KUJILETEA NA KUILETEA NCHI MAENDELEO, WOTE NI FAILURE TU.
 
Unataka nini wewe!
Usije ukafanya historia ijirudie bure...
Tuache we endelea kufurahia histori unayoijua wewe nasi tunamjua Nyerere kivyetu kama dhulumati tu
 
Mpaka leo bado unamgwaya??

Ha! Ha! Ha! Ha! Ha!

Siwezi kumgwaya mtu mjinga aliyeharibu mfumo yote ya utawala kuanzia Bunge,Serekali (executive) & Mahakama.

Siwezi kumgwaya mtu aliyeunda kikosi cha kuteka,kutesa,kuuwa wale wote waliokwenda kinyume na mawazo yake mabovu kupindukia.

Siwezi kumgwaya mtu aliyeharibu uchaguzi.

Siwezi kumgwaya mtu aliyekuwa akidanganya WaTanzania miradi yote mikubwa ilijengwa na fedha za ndani kumbe alikuwa mkopaki mzuri.

Siwezi kumgwaya mtu aliyetumia kodi za wananchi kujenga uwanja wa ndege kijijini kwake.

Siwezi kumgwaya mtu aliyetenda na kujenga misingi ya ukabila & ukanda.

Kwa hakika kama Tanganyika ingeanza kuongoza na Mungu wa Chato kungekuwa na ukabila mkubwa kuliko Kenya.
 
Itakua baba yako alikua fisadi.Pole sana kwakutoka povu kulipa machungu ya baba yako.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Na hizi ndizo akili mlizojazwa na Nyerere na Magufuli!
Yaani nyie mliaminishwa kila anayetajirika bas huyo ni fisadi tu.
Ndo mana watu huamua kuhamishia mali nje ya nchi kwa sababu ya akili zenu za kimasikini
 
Hukuziona picha za jinsi Mwangosi alivyouawa?? Sema tuna mahakama kibogoyo ndiyo maana haki haikutendeka. Aliyemteka Dr. Ulimboka na kumpeleka Mabwe Pande hukusikia akitajwa wakati ule? Usijaribu kusawazisha uovu kwa kutaja uovu wa watu wengine.

View attachment 2395306
Dr.Stephen Ulimboka mara tu baada ya kuokotwa maeneo ya Mabwe Pande!!

Huyo Ulimboka alitekwa na kuteswa kipindi cha raisi gani ? Nani alikuwa raisi wa nchi Ulimboka alipofanyiwa huo unyama?
 
Ndio kiongozi wa hovyo kupindukia
Ni maoni yangu,ndio maana nimetanguliza tuliompenda,bado sisahau siku aliyoondoka wiki nzima sikuwa vizuri,machozi tu.

Sikuwahi kuwa tz mpaka ameondoka but kazi na sifa zake nzuri zilisikika kila mahali.
Kiongozi bora hujulikana kwa kazi zake njema na misimamo thabiti kutetea Taifa lake,aliyaishi hayo na kuvutia wengi.
 
Back
Top Bottom