Nyerere, Mwinyi, Mkapa, na Kikwete waliwahi kuvaa Magwanda ya JWTZ walipokuwa Marais?

Huo uvaaji ulianzishwa na Magufuli. Sijui sababu ilikuwa nini. Kagame na Museven ndio wavaaji wakubwa wa sare hizo na wao wanajulikana walitawala mwanzo kwa mapinduzi.
Putin na xi Jin ping huvaa
 
Asipoelewa nahapa tena tumpopoe namawe hakika
Marekani ni nchi ya kidemokrasia,jeshi lake huitwa jeshi la wananchi?..jeshi la china haliitwi jeshi la wananchi,rais wao hakuwahi vaa sare za jeshi?..hizo Sheria zake/elimu ya uraia ni universal, kwa maana ni kwa kila nchi duniani?
 

Zile nguo zimetoka jeshini
So kama wao ndio wamempa then wanajua hakuna shida ya Rais kuvaa

Otherwise wasingekubali avae kama kungekuwa na shida
 
Rais anapata wapi ushauri wa mambo ya jeshi? And why anapata ushauri why asiamue tu
Katiba ya JMT inasema wazi Rais halazimiki kuchukua ushauri wa mtu yeyote.

Maana ya kutii unaelewa? Unaposema Rais amtii Jenerali unaelewa unamaanisha nini?

Jenerali amekula kiapo cha utii Kwa Rais ila Rais hawezi kumtii Jenerali. Haya mambo yapo wazi Sana nashangaa unarefusha hoja.
 
Huna akili,wakivaa kina Samia wanavunja sheria gani kwenye katiba? Kwan amir jeshi mkuu ina maana gani? au unahisi maana yake ni mkuu wa vyama vya siasa
 
Japo sio muhimu na wala haina maana yoyote, sijawahi kumuona hayati J.K.Nyerere katika gwanda za kijani za CCM na ndie alikua mwenyekiti wa CCM taifa 🐒
 
Umesema kitu cha kufikirisha sana. Inawezekana huu ndio MSIBA mkuu wa kihistoria wa Waafrika (historical tragedy of this continent).

Maelezo mengi ya kihistoria niliyosoma yanaonyesha wababe walipokuwa wakija Afrika kusaka watumwa, rasilimali na makoloni, waafrika badala ya kuungana kupambana kuwaondoa, walikuwa wakizungukana na kujikomba kwa wababe hao na kuwasaidia kuchukua ndugu zao utumwani pamoja na kuwabebea yote waliyotaka hadi kwenye merikebu zao.

Wakoloni waliwezeshwa sana na baadhi ya machifu na watu wao kujitwalia makoloni na kuwatumikisha maelfu ya Waafrika kitumwa katika shughuli za ujenzi, kilimo, uaskari, n.k. Bila machawa hao wa Kiafrika, wakoloni na wafanya biashara ya watumwa wangekwama sana katika harakati zao.

Hadi leo hii somo la demokrasia na haki za binadamu linashindikana kabisa Afrika. Wengi wanadai ni utamaduni wa Magharibi, kwamba ni janja ya kutaka kuiba rasilimali za Afrika! HAWAUTAKI. Wanachotaka ni kiongozi imara, mwenye maono na mwenye kujali wanyonge! Atapatikanaje? (kwa maombi na deep state!) Na uchawa kwa viongozi wababe ndio mtindo mkuu wa maisha na mafanikio kwa Waafrika wengi chini ya jangwa la Sahara. Sad.
 
lipandishe tena mkuu
 
Zile nguo zimetoka jeshini
So kama wao ndio wamempa then wanajua hakuna shida ya Rais kuvaa

Otherwise wasingekubali avae kama kungekuwa na shida
Bado hujaelewa somo na at this point nafikiri labda si tu hujaelews somo, labda huna uwezo wa kuelewa somo.

Nguo kutoka jeshini si hoja.

Kwa sababu kinachofanya rais wa kidemokrasia kuvaa nguo za jeshi kuwa jambo baya si nguo zinatoka wapi.

Kinachofanya rais wa kidemokrasia kuvaa nguo za jeshi kuwa kitu kibaya ni kwamba rais analeta muonekano wa nchi kuongozwa kijeshi wakati nchi inatakiwa kuonekana inaongozwa kiraia.

Civilian control of the military, amiri jeshi mkuu anatakiwa kuvaa nguo za kiraia ili ionekane nchi inaongozwa kiraia, jeshi linapewa amri na raia.

Rais akivaa magwanda ya jeshi inaonekana kuwa wanajeshi ndio wanaongoza nchi. Nchi haipo katika uongozi wa kiraia, ipo katika uongozi wa kijeshi.

Nina shaka kama unaweza kuelewa.

 

Brother, amevaa mara ngapi?

Amevaa kwenye matukio gani?

Mbona mnatake Jambo la kawaida kuwa big ishu?

Possibly Sheria zimechange bila ww kujua so ulizia zaidi Kwa wahusika

Hii ishu ingekuwa ni hivyo unavyosema sidhani kama Rais angevaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…