Uchaguzi 2020 Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa: Vyama vya Siasa vinavyotaka kushirikiana Uchaguzi Mkuu vimeshachelewa kwa mujibu wa Sheria

Uchaguzi 2020 Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa: Vyama vya Siasa vinavyotaka kushirikiana Uchaguzi Mkuu vimeshachelewa kwa mujibu wa Sheria

vyama vya hovyo utaviona tu
mchakato unafanyika,uteuzi mnafanya halafu angani mnamtosa mgombea wenu,yale yale ya ukawa na Dr slaa
 
ma CCM maoga kuliko kunguru, mbona yenyewe wanaungwa mkono na chama cha TLP?
 
Hawa wapinzani wanafanya mambo yao mengi bila ya kufata sheria na ndo maana wanaona kama wanaonewa kumbe uzembe wao kila siku kulalamika hadi tumewachoka. Chama cha Mapinduzi Jambo lolote ambalo wanalotaka kufanya lazima wafate sheria na ndo maana wanafanikiwa na wananchi tunaona.
 
Amecherewa yeye. tunaoungana ni sisi wapiga kura sio vyama.
 
Sijaona mtu anaeweka arguments kama Tume imekiuka sheria iliyonukuliwa hapo juu mngegundua TLP na UDP imetimiza matakwa kwa kushirikisha vikao vya chama na kwa muda unaotakiwa. Na wala hawakupendekeza mgombea wao akateuliwa na tume na kufanyiwa maandalizi yote ya uogombea. Kiukweli vyama hivi havishirikiani na CCM Bali vime Endorse mgombea wa CCM Nami naiweka.


llA.
(2) The decision to form a coalition shall be made by
a national general meeting of each political party intending to
form coalition and shall be in writing and duly executed by
persons authorized by pol itical parties to execute such
agreements on behalf of each political party intending to
form a coalition.
(3) A coalition agreement entered into before a
general election shall be submitted to the Registrar at least
three months before that election.
(4) A coal ition agreement entered into after the
general election shall be submitted to the Registrar within
fourteen days after the signing of the coalition agreement.
(5) A coalition agreement shall set out the matters
specified in the Second Schedule to this Act.
(6) Political parties to coalition under this section
shall maintain their status as individual registered political
parties, and shall continue to comply with all the
requirements governing political parties under this Act and
any other relevant laws.
 
Ilikuwa ndani ya muda wa kisheria!
Makubaliano yao waliyapeleka kwa msajili? Je yalipitishwa na mikutano mikuu ya vyama husika?
Suala si tu kuanza kushirikiana miezi mitatu kabla ya uchaguzi, bali pia kufuata taratibu zote. Kama mkutano mkuu wa ccm haukupitisha azimio la kuwa watashirikiana na TLP na UDP, then wote wana makosa. Nilisikia mahali mgombea wa CCM akisema tayari ameungwa mkono na TLP - ni hayo hayo ya ACT Wazalendo na CHADEMA.
kwa maoni yangu wote waachwe waendelee halafu tuamue kwenye box la kura.
 
Mtahangaika sana CCM , kijani kibichi , mbinu zenu zote zinajulikana zitabuma tu mwaka huu , watu hata aibu hamna
Screenshot_20200923-113223.png
 
Hawa watu wa tume hawana akili timamu kwa sababu muda wote wanafikiria kuisaidia ccm..... Waache kuhadaa watz wanaotaka mabadiriko....
 

Attachments

  • Screenshot_20200923_122517_com.facebook.katana.jpg
    Screenshot_20200923_122517_com.facebook.katana.jpg
    147.3 KB · Views: 1
Naibu wa msajili wa vyama vya siasa Dkt. Nyahoza amesema vyama vya siasa vinavyojipanga kushirikiana vimeshachelewa.

Nyahoza amesema muda uliowekwa kisheria kwa vyama vyenye nia ya kushirikiana kuingia mkataba wa kisheria umeshapita hivyo hakuna ushirikiano utakaoruhusiwa kwa sasa.

======

MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA: VYAMA VINAVYOTAKA KUUNGANA, VIMESHACHEWA

Vyama vya Siasa ambavyo vinatarajia kushirikiana wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu bila kufuata Sheria ya Vyama vya Siasa kama ilivyoainishwa kwenye Kifungu Na.11 (a) cha Sheria hiyo vitakuwa vimevunja sheria.

Onyo hilo limetolewa jijini Dodoma na Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza, wakati alipofanya mahojiano kuhusu msimamo wa ofisi yake kwenye suala la ushirikiano wa vyama vya siasa wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Nyahoza amesema kuwa ushirikiano wa vyama hivyo umeratibiwa vizuri kisheria ambapo vyama vinapohitaji kushirikiana vinapaswa kutumia vikao halali vya chama badala ya utashi wa mtu binafsi. Msajili Msaidizi Nyahoza ameongeza kuwa baada ya vikao halali kupitisha azimio la kufanya ushirikiano vyama husika vinapaswa kuwasilisha mkataba wa ushirikiano Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa miezi mitatu kabla ya mchakato wa uchaguzi kuanza.

“Vyama havijakatazwa kushirikiana bali vimewekewa utaratibu ili Tume ya Uchaguzi pamoja na taasisi zote zinazohusika na uchaguzi ziweze kujiandaa vizuri na kuimarisha ulinzi hasa wakati wa kampeni pamoja na kuvisaidia vyama vingine kuelewa wanashindana na vyama vya aina gani” alisema Nyahoza.

Kuhusu ushirikiano wa vyama vya siasa wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2020 Msajili Msaidizi Nyahoza ameelezea kuwa mpaka sasa ofisi yake haijapokea mkataba wa makubaliano ya ushirikiano kutoka kwa chama chochote cha siasa hivyo kwa mujibu wa sheria vyama ambavyo vina nia ya kushirikiana vimeshachelewa.

Aidha, Msajili Msaidizi Nyahoza amesema hadi sasa vyama vyenye usajili wa kudumu ni 19 na chama kimoja kina usajili wa muda na maombi ya vyama 16 bado yanafanyiwa upembuzi.


Maendeleo hayana vyama!

Hawashirikiani ila wanachofanya ni kuwa

Membe anajitoa, sidhan kama ni kosa kisheria,

Then chadema na ict watatangaza kuwa kwenye kila jimbo wanainchi wachague ict au chadema

Nadhan hapo hakuna shida kisheria
 
Back
Top Bottom