TANZIA Pacha waliotenganishwa, mmoja afariki dunia

Mkuu uko sahihi kabisa pia lazima tujue hii operation ilifanikiwa ndio maana huyu mtoto kaishi siku zote hizo.
 
Asante mkuu kwa kunielewesha maana wengine wana nipopoa mawe tu
 
Nilitaka kushangaa tangu lini Tanzania tukawa serious kiasi hiki na kufanya vitu vikafanikiwa.
Sisi tuko bora sana kwenye kimasihara lakini vitu vya maana mhh...
Msinipopoe mawe wakuu
Najaribu kukuelewa.
 
Nilitaka kushangaa tangu lini Tanzania tukawa serious kiasi hiki na kufanya vitu vikafanikiwa.
Sisi tuko bora sana kwenye kimasihara lakini vitu vya maana mhh...
Msinipopoe mawe wakuu
Aaah hapana usiseme hivyo, mmiliki wa uhai na kifo ni Mwenyezimungu pekee, tuwashkuru madaktari kwa jitihada zao,
Kesho na ww utaugua utawategemea wao wakuponye,.Hongereni, Inna lilahi waina ilaihi rajiun
 
Mbona unajihami,wabongo mnachojua ni kuponda na kukashifu. Hawa watoto hawakufanyiwa operation na madaktari wa Tanzania pekee bali jopo la madaktari bingwa zaidi ya 40 toka nchi mbalimbali.

Kwa ufupi hii ilikuwa moja ya operation hatari sana, nadhani walifanya kile kinachowezekana lakini kifo hupangwa na Mungu.
 
Kwa siku ambazo watoto wote wamesurvive inatakiwa tuwape hongera madaktari, hata mbuyu ulianza kama mchicha.

Inauma kupoteza mtoto kwa wazazi, lakini lazima tukubaliane na ukweli mchungu kuna wakati ni lazima wengine waumie ili wengine wanufaike. Sio kwamba nafurahia kifo, ila kwa operation hiyo Moja tayari madaktari wetu wameanza kupata uzoefu halisi na wanajua wapi wazidi kuboresha.

Pole wa wafiwa, Mungu amponye mtoto aliyebaki, na hongera kwa madaktari kwa jitihada zao.
 
Nilitaka kushangaa tangu lini Tanzania tukawa serious kiasi hiki na kufanya vitu vikafanikiwa.
Sisi tuko bora sana kwenye kimasihara lakini vitu vya maana mhh...
Msinipopoe mawe wakuu
Hiyo hatua waliyofikia ni kubwa sana.
Hata wright brothers walijaribu mara nyingi na kufail mara nyingi mpaka wakafanikiwa kutengeneza na kurusha ndege ya kwanza, then muendelezo na maboresho ndio leo kuna bombardiers na boeings. Siku zote hakuna straight way na shortcut au kufanikiwa moja kwa moja kwenye chochote kile especially kwenye maswala ya science ni trials and errors.

Kujaribu na kufail na kushindwa au kuanguka ndio njia pekee ya kujifunza makosa na kutorudia, kurekebisha na kuboresha mpaka kufanikisha lengo. Means hapo watajua wapi walipokosea na kosa halitojirudia tena.
Au kama unaogopa kujaribu na kufail au kushindwa basi hautofanya chochote kitakachofanikiwa maisha yako yote hapa duniani.

Watu wanaofanya Programming wanajua huu mchezo wa Trials, Errors na Debugging it's tedious and stagnating lakini mwisho wa siku lazima Code ikubali same kwenye maisha halisi sema ni way worse kama hivyo.

Failure Is the only Seed of Growth and Success / Development. ONLY WAY.
 
[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Hata mi ningeshangaa,watoboe wote mmm ingekuwa maajabu
Hakuna maajabu kwenye sayansi ni kujaribu na kushindwa mpaka upate kilicho sahihi, ni kama kujaribu pea za viatu.
Au niseme kwa kusisitiza kwamba There's No Miracle In Science Only Trials And Errors Until Success.

Hakuna shortcut wala njia ya moja kwa moja ya mafanikio, hiyo hatua waliyofikia ni kubwa sana kwenye ulimwengu wa science sababu watajua kosa liko wapi na kurekebisha hivyo halitojirudia tena.

Nyie jamaa ndio mnapigagwa Forex mnaota kulala masikini na kuamka tajiri.
 
Watu hawajui misala wanayopitia wataalamu wetu...... Hawa watoto walikuwa complicated sana.... Na kwa nature ya hizi procedure complication kutokea ni kawaida tu... Hata huko ulaya so hawa jamaa wamejitahidi mpaka walipofika inatosha
 
Hata kabla ya hiyo Op nilishangaa "advertise" nyingi mara,"Tutakuwa nchi ya tatu Africa kufanya Op hii".

Nikajiuliza tu,"Vipi isipofanikiwa? Record itaandikwa hivyohivyo."
 
Ungemtibu wewe kama huyo daktari ni wa mchongo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…