Pamoja na udhaifu wake wote ilionao, ni kwanini CCM inaamini itatawala Tanzania milele?

Pamoja na udhaifu wake wote ilionao, ni kwanini CCM inaamini itatawala Tanzania milele?

Kama ina katisha tamaa na hakuna wa kumpindua tufanyeje sasa?
Mfano hai ni hizi siasa zinazoendelea sasa hivi unadhani upinzani watashinda 2025. Mama ameshakubalika anafanya maajabu tunampinga ili iweje? Apewe miaka 10 zaidi
Hivi kwani mtu ukimshukuru kwa kukufungulia mlango wa nyumba yako kwa kuwa umebeba mizigo mkononi, ndiyo anaondoa haki yako ya kumuuliza ni kwa nini huwa anaiba mapapai yako??
 
Sikatishi mtu tamaa, wanaoweza kupambana kuitoa ccm madarakani wafanye hivyo.
Mimi siamini kama wapinzani watakuwa na jipya, siasa hizi kila mtu anaangalia tumbo lake hakutakuwa na jipya lolote. Sichukulii siasa seriously kivile maana nitaishia kuvunjika moyo.
Bibie umeongea ukweli mchungu wanasiasa wapo kwaajili ya kujinufaisha wao wenyewe hao Wapinzani ndio hamna kitu kabisa sasa hivi nao wanalamba asali
 
Hivi kwani mtu ukimshukuru kwa kukufungulia mlango wa nyumba yako kwa kuwa umebeba mizigo mkononi, ndiyo anaondoa haki yako ya kumuuliza ni kwa nini huwa anaiba mapapai yako??
Haki ya kuuliza wanayo. Je umeona wanauliza? Si wamekaa kimya wanaona kila kitu sawa?
 
Hakuna wapinzani......
Watakapotokea CCM watabadilisha msimamo wao.
Upinzani utakaotokana na Watanzania, sio kikundi fulani cha watu wachache, Wenye interest zao na kulazimisha Agenda zao ndio ziwe Agenda za Watanzania.
Siku Watanzania watakapoungana kutetea maslahi yao ndio utakuwa Mwisho wa CCM.
Kwa sasa No, waliopo Nje ni wabaya kuliko waliopo ndani.
Ugumu wa maisha ndio utaikomboa Tz
 
Hicho chama kinahusika kwenye kila madudu yanayotokea kwenye nchi yetu, Hakuna jambo baya kwa watanzania ambalo halijatokana na CCM kuwa madarakani. Lakini CCM wenyewe kwa kujiamini kabisa wanasema kwamba watatawala Tanzania milele?? Haya ni maneno yanayoonesha CCM ina kiburi cha uzima kiasi kwamba inaamini mpaka kyama yenyewe itakuwa inaitawala Tanzania.

Au CCM inawaona watanzania ni mazezeta wasioweza kuwatoa madarakani?
Wakili msomi na kada wa Ccm Pascal Mayalla pitia hapa....
 
Haki ya kuuliza wanayo. Je umeona wanauliza? Si wamekaa kimya wanaona kila kitu sawa?
Labda wameuliza sana kiasi kwamba wameona labda watanzania tumeridhika na hali iliyopo. Hiv wafanyakazi wa Tanzania waliponyimwa kuongezwa mishahara na kupandishwa madaraja kwa miaka mitano mfululizo walifanya nini kuonesha kwamba haki yao inavunjwa??

Hilo pia linataka vyama vya siasa?? Martin Luther King Jr hakuwa mwanasiasa, Malcom X na wengineo wengi tu, lakini nguvu yao ilitokana na kuungwa mkono na wananchi wa kawaida. Sisi hao wapinzani tunaowasema hawafai ni lini tulisimama nyuma yao walipoipinga CCM?
 
Hakuna chama mbadala kinaweza kukitoa CCM madarakani ndio maana Wana kiburi chakusema hivyo we si umeona Wapinzani wana lamba asali now.Vyama vya Upinzani haviaminiki kwa Watanzania kwa sababu kama hizi

1. wanasiasa ambao hawana msimamo
-ukiangalia vyama hivi vya Upinzani ni ndumilakuwili Mara Lowassa fisadi Cha ajabu ndio anakuwa mgombea wa Uraisi kwa namna hii wataanzaje kuaminika kwa jamiii

2. Hawaubili wanachosema
-wanadai demokrasia lakini uwendeshwaji wa vyama vyao sio vya kidemokrasia

3.wanajali mno maslahi yao
-Sijawahi kusikia au kuona Chadema inaamasisha Watanzania kuandamana kwaajili ya kupinga mambo negative yanayowagusa wananchi mfano upandaji wa bei za vitu n.k hata hiyo katiba wanayodai wamejikita kwenye Tume wa uchaguzi kuwa huru lakini sio yale mambo yanagusa Moja kwa Moja wananchi ndio maana wanashindwa kuungwa mkono na wananchi wote wanaongea yale yanayogusa vyama vyao zaidi Je kwa namna hii hata kama CCM ni mbovu je unadhani utawafanya wawachague Wapinzani?
 
Hziyech22 CCM kama chama kwa ujumla hakina msimamo, ni kwa nini watanzania wanahukumu wapinzani wote kwa kutokuwa na msimamo lakini wanaona ni sawa tu kwa CCM kutokuwa na Msimamo kama chama.

Kwa mfano:
CCM walisema watoto wanaopata mimba wakiwa shuleni wasiruhusiwe kurudi shuleni kuendelea na masomo, leo hii CCM hiyo hiyo inasema watoto hao waruhusiwe kurudi shuleni. Unadhani hapa CCM ina msimamo??
 
Inaongoza nchi. Kwa sasa ni imara mbadala wake haujapatikana
Kuongoza nchi pekee ndiyo kigezo cha kupima uimara wa CCM? Hivi hatuwezi kusema kigezo cha kupima uimara wake kiwe ni jinsi gani wanaiongoza nchi!!??
 
Labda wameuliza sana kiasi kwamba wameona labda watanzania tumeridhika na hali iliyopo. Hiv wafanyakazi wa Tanzania waliponyimwa kuongezwa mishahara na kupandishwa madaraja kwa miaka mitano mfululizo walifanya nini kuonesha kwamba haki yao inavunjwa??

Hilo pia linataka vyama vya siasa?? Martin Luther King Jr hakuwa mwanasiasa, Malcom X na wengineo wengi tu, lakini nguvu yao ilitokana na kuungwa mkono na wananchi wa kawaida. Sisi hao wapinzani tunaowasema hawafai ni lini tulisimama nyuma yao walipoipinga CCM?
Chadema hawana madaraka lakini huna uhakika kwamba wakiingia eti watafanya maisha ya watanzania yawe mazuri hawana njia yoyote ya kupata madaraka bila kupitia matatizo ya watu shida yao kuu ni vigeugeu ujui wanasimamia nini na Ndio hawaaminiki na watz Watanzania wanaona Bora ya CCM kuliko Upinzani usiojielewa
 
Hziyech22 CCM kama chama kwa ujumla hakina msimamo, ni kwa nini watanzania wanahukumu wapinzani wote kwa kutokuwa na msimamo lakini wanaona ni sawa tu kwa CCM kutokuwa na Msimamo kama chama.

Kwa mfano:
CCM walisema watoto wanaopata mimba wakiwa shuleni wasiruhusiwe kurudi shuleni kuendelea na masomo, leo hii CCM hiyo hiyo inasema watoto hao waruhusiwe kurudi shuleni. Unadhani hapa CCM ina msimamo??
Watanzania wanataka chama mbadala Bora Mara mbili ya chama tawala je hicho chama kipo? Na Kama kipo nitajie ubora wake uko wapi?
 
Ili wawe wapinzani wanatakiwa wawe na sifa zipi. Maana ni ajabu kama wanaosema hakuna wapinzani ni CCM wenyewe. Jee CCM kwa muktadha huu wanayo sifa ya kusema kuwa hakuna wapinzani dhidi ya CCM?
Wasirambe asali
 
Back
Top Bottom