Pamoja na ufaulu kupanda, shule za kata Dar hali ni mbaya, Division Zero ni nyingi sana, Afisa Elimu aondolewe

Pamoja na ufaulu kupanda, shule za kata Dar hali ni mbaya, Division Zero ni nyingi sana, Afisa Elimu aondolewe

Hao wanaoenda chuo kikuu wakitoka wanakuja kuuza ukwaju wa bakhresa na hao wa kitunda,kusajili laini na hao wa kitunda, kukimbiza boda boda na hao wa kitunda, kuwa wachekeshaji mitandaoni na hao wa kitunda au nakosea ?
Tofauti ni kwamba matokeo tumeyaona na wamelamba miswaki na zero.

Hao wauza ubuyu hatuwaoni hapa na hatujui wamesoma shule gani.
Isiwe kesi, peleka mwanao Kitunda uwe na uhakika wa kumpatia zero ili auze ubuyu wa Azam vizuri.
 
Pia sheria iwekwe ya kuwa mtu akitaka kusomea uwalimu lazima aondoke na 1 au 2 kidato cha nne kwa kuwa watu wengi wanasomea uwalimu wakishapata 3 au 4 na si kwakuwa wanapenda uwalimu.
 
Kwani afisa elimu ndo kafanya mitihani kumbuka wingi wa shule za shule za serikali kuchangia kuleta matokeo mabovu watoto mchelemchele wakiguswa wazazi na walezi midomo juu walimu wafanye nn zaidi ya kukaa kimya mambo yajiendee
 
Yaani watu wanasikitika kuona machangu, wacheza singeli, maafisa ubashiri, wavuta bangi, walevi, n.k n.k wamekata sufuri.
Great Thinkers wa JF ya zama hizi bhana.
Walimu pokeeni matusi wiki hii.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Ndugu yangu LIKUD unaonaje hiyo shule ya Kitunda ni kayumba inayomfaa mwanao maana wewe hutaki EM schools.

Wakati mwanao anaambulia miswaki wewe unamfanyia "uwekezaji" ili usitumie hela bure kulipa ada. Akitoka hapo na zero, aje awashinde wale kina St. Francis kwenye ufaulu wa chuo cha ndotoni, maana kwa matokeo hayo chuo kikuu its likely atakisikia kwenye redio. Labda ianzishwe kozi ya uyaya.
Hao waliopata division one na wale wa zero baada ya miaka michache mbeleni, wote watakutana kwenye kuendesha bodaboda. Trust me..
 
Kwani afisa elimu ndo kafanya mitihani kumbuka wingi wa shule za shule za serikali kuchangia kuleta matokeo mabovu watoto mchelemchele wakiguswa wazazi na walezi midomo juu walimu wafanye nn zaidi ya kukaa kimya mambo yajiendee
Kwani mtoto anafaulu kwa kuadhibiwa?
Walimu wenyewe siku hizi wanaanzisha michango isiyo na mbele wala nyuma halafu unategemea waelewane na wazazi.
 
Shule imerundikiwa watoto 634 na unataka wafaulu wote!, tafuta private school au hata government school iliyofanya vizuri ikiwa na idadi kubwa ya wahitimu kama hao
 
Yaani watu wanasikitika kuona machangu, wacheza singeli, maafisa ubashiri, wavuta bangi, walevi, n.k n.k wamekata sufuri.
Great Thinkers wa JF ya zama hizi bhana.
Walimu pokeeni matusi wiki hii.
Kwani nani anajukumu la kuwaadabisha hao wacheza singeli na wavuta bangi?
Na ukiona mtoto kaingia kwenye hayo makundi ujue ya kuwa shuleni walimu walikuwa wanazembea kwakuwa watoto muda mwingi wanautumia shuleni na wanaanza kuharibika wakiwa shuleni.
 
Unaambiwa kulipa ada ni matumizi mabaya ya fedha. Eti "ufanye uwekezaji" huku mwanao analima miswaki na zero zisizohesabika, wewe unamnunulia vipande vya 20×20 eti chuo atakutana nao hao kina St. Francis.

Mwisho wa siku unakula za uso, anatoka anastahili fani ya uyaya na umamantilie posho alfu tano kwa siku😂
LIKUD yupo sahihi. Kuna graduates hata huo umamantilie wana ulilia bila mafanikio..
 
KAYUMBA schools za Likudi ndiyo chanzo Cha zero Kwa wanafunzi.Hakuna hata EMs Moja ambayo mwanafunzi wake hata mmoja ambaye amepata daraja la sifuri.
Una data?
 
matokeo ya form four kwa mwaka 2024 yametangazwa leo.
Kwa mujibu wa baraza la mitihani, ufaulu umepanda kwa asilimia tatu.

Ila huku kwenye shule za kata hali mbaya. Unakuta nusu ya wanafunzi wamefeli vibaya mno katika shule husika.

Mfano shule kama Kitunda hali ni mbaya, wanafunzi 249 wamepata division zero. Unajiuliza hii shule ina uongozi kweli? Afisa Elimu nae analipwa mshahara kabisa? Nini kifanyike wakuu?View attachment 3211475

View attachment 3211479

View attachment 3211481

View attachment 3211491

View attachment 3211492

Soma: NECTA yatangaza matokeo ya kidato cha nne 2024. Yatazame hapa!
Zero 249 Alafu niendelee kuhangaisha kichwa waangalie na ujuzi wa watu wasikae kuhangaisha vichwa zaidi for nothing
 
Wakati wengine wanalia na zero, St francis wanafunzi wote 92 Wana division one point 7,
 
Back
Top Bottom