Paul Kagame katoa onyo kwa Kiswahili, walengwa mmepata ujumbe?

Paul Kagame katoa onyo kwa Kiswahili, walengwa mmepata ujumbe?

Naona hauelewi vita za proxy, Kagame hahitaji kwenda Kenya ila obviously Uganda ni koloni la Watutsi so in any war itakua via Uganda.

2. Kingine Kenya Ina vikundi kibao vya uasi sio tu NFD region kwa wasomali na wafugaji ila hata makundi ya msimamo mkali wa kiislamu wa kujitenga huko Pwani. Kagame anaweza fanya kazi na hao watu na ikapigwa vita ya proxy kama tu ilivyokua Ile ya M23..

3. Ukabila ni mkubwa sana Kenya kiasi kwamba wafuasi wa Upinzani yaani Wakamba, waluo, Waluhya, Pwani n.k wakiskia tu jeshi la Kenya limeingia vitani basi watakua wa kwanza kwenda barabarani kupinga nchi kuingia vitani na watakataza wafuasi wao kwenda Frontline. In fact wataona ni short cut ya kumpindua Ruto asubuhi na mapema.

4. Kuhusu uimara wa jeshi yes it's true linatengenezwa ila experience matters. Nchi zilizopo kwenye Kashi Kashi za kivita zinakua hazina margin of error so muda wote majeshi Yako busy. Mfano Rwanda ana majeshi kwenye nchi zaidi ya 13 yote hiyo ni kuwapa exposure na activeness kwenye battlefield. Sasa unadhani akikutana na wanajeshi wavaa ndala wa Westgate Nini kitatokea?? Rwanda fought in the Africa's world war, the audacity to take head-on 13 African countries in a stalemate war for 5 years should be a lesson to Ruto, unless he's dumb enough to disregard history!!
Sasa tukija kwenye proxy wars hapo ndio Rwanda inapigwa mapema kuliko Kenya. Rwanda ina uwezo wa kutoa hata $500 million kufadhili makundi pale Kenya? Kenya inao uwezo wa kuipata hiyo hela bila kukopa wala kuombaomba.

Kwa sasa waasi wenye silaha wanaopingana na Rwanda wapo pale Congo, kuna waasi wenye silaha wanaopambana na Kenya ukiachana na kundi la kigaidi ambalo halina claim na throne ya Kenya? Kenya haihitaji wala kuanzisha kundi jipya, ni kuyapa makundi hasimu ya Rwanda kama FDRL ambayo hata sasa yanatafuta nafasi na ukiyataka yapokee silaha na training leoleo yanakubali.

Kama unaona Rwanda itaitumia Uganda kuipiga Kenya, mbona huoni kama Kenya itaitumia Congo na Burundi kuipiga Rwanda. Burundi na Congo wana uhasama na Rwanda kuliko Kenya ilivyo na Uganda. Na unadhani Uganda ni wapumbavu wapigane na Kenya kisa Rwanda. Hata kama Museveni angekuwa hana akili ila kile sio chama cha vikoba ni nchi, hawezi risk madaraka yake na urithi wa mwanae kwa kutafuta mgogoro na jirani anayepitisha over 80% ya mizigo kwenye bandari yake.

Kenya haihitaji kurusha hata risasi moja kuikomoa Uganda. Funga bandari, barabara na reli zisiingize mizigo Uganda itokee inflation uone kama vijana wa Kampala watamuacha Museveni na walivyomchoka.

Nilikuwa nakuona kwenye uzi LIVE wa uchaguzi mkuu wa Kenya. Unaweza kutuwekea majimbo ya uchaguzi na matokeo yake hapa ukiambatisha na hayo makabila ili tuone upinzani wa Kenya ulivyo wa kikabila.
Kenya ina makabila 56 na hakuna civil war, genocide, assassination of head of state wala mapinduzi yaliwahi tokea. Rwanda ina makabila almost mawili tu yaliyopigana na yashaua marais pinzani, mauaji ya kimbali, uasi hadi sasa, mapinduzi. Nani kati ya hizi nchi mbili ana ukabila kuliko mwingine?

Kama vita ni mazoea basi unasema Switzerland ambayo haijawahi pigana miaka zaidi ya 500 iliyopita ni wapuuzi tu vitani wakati enzi za Cold War walikuwa na maandalizi makali kupindukia, maandaki ya kuficha population nzima ya nchi plus 10% ya ziada, na hakukuwa na nchi yenye uwezo wa kuficha hata 10% ya population. Last time Japan wamepigana vita ni 1945, kwamba kwa sasa wana jeshi yeboyebo?
Mbona Tanzania ya Mwalimu Nyerere iliipiga Uganda ya Iddi Amin mwanajeshi na mipango yake mingi. Mbona Libya ya Ghaddafi ilishindwa kuipiga Chad wakati Libya ilikuwa na harakati nyingi za kijeshi.

Ebu mkuu kaa chini jifikirie utafakari iami yako ya Uganda itaipiga Kenya kwa niaba ya Rwanda, kwa sababu ya Congo.
 
Kama KAWAIDA yangu,HUWA sibezi mawazo ya mtu!


Tujiulize Hawa jamaa wamepenyeza wanajeshi wangapi kwenye jeshi letu!?

Hao tunaowaita wakurya,wasukuma,wazanaki,wanyambo,waangaza na wengine Wana nasaba kiasi gani na Rwanda!!?hao Bahima waliopo huku wamepenyeza maafisa wangapi wakitutsi kwenye idara zetu!?

Wakati sisi KWA miaka sita tukipambana sisi KWA sisi KWA ITIKADI za uchama na sio utaifa wenzetu walikuwa wanajipangaje!!?

Wakati jeshi la polisi likipambana na wapinzani Ili kulipa ahueni ccm wenzetu walikuwa wanapambana na Nini!?

Kuna vitu vingi Sana vya kumuuliza,na juzi Tshesejedi alikuja NCHINI hapa hatujui ni Nini alikuja kufanya japo VYOMBO vyetu vinajua!!

Mwisho niseme kwamba namwamini Sana CDF mpya general mkunda alishaanza maandalizi ya mazoezi sehemu mbali mbali kama ilivoripotiwa na vyombo vya habari majuzi!

Hii inamaanisha yupo pro -active ZAIDI!!!

Mungu atulinde mwaka 2023 ujao!!

Mungu aibariki NCHI yangu Tanzania!!
 
Tatizo mpo divided sana, ikitokea vita trust me Kuna watu wataombea Ruto apinduliwe!!!

Then Kenya Haina jeshi imara, kama mlidunguliwa na amateurs huko samburu au trans mara ndio mtaweza kupambana na Battle-hardened RPF??

Bora Uganda au Tanzania, ila Kenya is weak na mtapata mnachokitafuta.
Ila hiyo msg imekaa kama anatumiwa Tanzania maana tetesi zinadai mwakani JWTZ wataenda congo kuungana na jeshi la eac ukiondoa wa kitambo monusco
 
Wanyarwanda wamejipenyeza karibia kila sekta hapa nchini. Intelligence wako busy tu na issues za Chadema, uchawa na uchaguzi wa 2025. Kale kajamaa kaliwahi mkoromea msoga akaufyata kimya. Wenzetu wanaoperate kwenye viwango vingine kabisa sisi tumelala.
Do not undermine our security organs
 
Usikae hapo utegemee migawanyiko ya ndani, ni jambo la kawaida kwenye kila taifa, hata nyie hapo kunao naona mnashangilia na kushabikia sana ndege kukamatwa, japo sijaelewa ni uzalendo wa aina gani huo, ila likija suala la malumbano ya taifa dhidi ya taifa usithubutu.
Jifunzue na Ukraine ambao wana malumbano yao ya ndani, lakini wamemfanyia Urusi kitu ataishi akikumbuka kizazi baada ya kizazi.
Haahaaa Ukraine yenye jeshi imara ulinganishe na united Kenya yenye jeshi dhaifu 🤣🤣🤣. Let's be serious mkuu.

Mkianza vita na Rwanda (Obviously UG itahusika pia) trust me Wajaluo/Luhya watakua busy Kuandaa serikali inayokuja. NFD watakua busy kupora mifugo, Mombasa itakua busy kujitenga, ilihali Al Shabaab itakua busy kujitanua mandera!!

Tanzania sisi tuna upinzani wa kisiasa ila no udini au ukabila so ni ngumu kutugawanyisha tofauti na nyie ambao mna migawanyiko mingi nje ya siasa!!
 
Na wewe usiwe mjinga,Tanzania haijalala kiasi hicho japo hatujafanya vya kutosha naona Kama unahemka kwa vijimaneno vya mfa maji hapo juu..

Tungekuwa hatufanyi kitu Leo hii tusingekuwa na urali wa biashara kuwazidi wote EAC yaana balance of trade yetu na majirani wote Ni surplus in terms of quantity and value licha ya changamoto zote..
Mkuu, uliamkia nini?
 
Si wazipige tu ? ,tumechoka maneno na mdomo kuongea kimafumbo kama wanawake
 
mkuu napitia kwanza maoni yote ya wadau

Nipo naangalia ya ndani huku kuelelekea election

Ila kwann kagame huwa anapanic sana wakiguswa M23?
Uchaguzi ni lini mkuu? Na Kuna uwezekano wa JK junior kuwa factor kwenye mtanange huo?

ana panic sababu M23 ni ndugu zao walau kikabila na mshirika wao tokea enzi za RCD Goma so ukiua Mnyamulenge wa M23 ni sawa na kuua Mtutsi aliyepo Kigali!!

Upande wa pili labda wanaamini ni kivuli tu ila M23 ni project yake!! So akipanic basi ni mradi unaingia mchanga!!

All in all walitaka Kagame asinune, wafanya operation ya kufuta makundi yote ya waasi huko mashariki sio wabague bague labda ndio inamtia hasira. Yaani wezi tupo wengi ila wananidaka Mimi tu??
 
Watu siwaelewi, eti Kenya itapigwa na Rwanda kisa wana experience ya kupigana vita ya ardhini.
Kwamba Kenya ije na Serbian Nora B-52K1 155mm self propelled howitzer among top in Africa
20221128_230913.jpg

Ije na American M118 105mm artillery
IMG_20221202_122826.jpg


Ije na F-5 fighters na Rwanda haina fighter jets kabisa
20221202_123436.png

Ije na British Vickers MK3 tanks
20221202_124032.jpg


Ije na various helicopters
20221202_123452.png


Na silaha nyingine nyingi tu ambazo ni superior in capabilities and number dhidi ya Rwanda kisha Rwanda iseme ilivyotuma wanajeshi mia tatu mia tatu Mozambique na wapi wapi uko hivyo wataishinda Kenya.

Hakuna anayetoa hoja za msingi kwa nini Kenya inaweza pigwa na Rwanda. Pointi zote nikiona zinanikatalia Rwanda kushinda, hisia tu za ukubwa wa Rwanda ambao haupo. Tofautisha mtu mwenye nguvu na mwenye fujo, Rwanda ina fujo za kudumu ambavyo hata Burundi wakitaka wanaweza anza leo after 20 years wakawa wasumbufu
 
Kusema ukweli kagame ni rais bora zaidi Africa kwa generation hiita mnaokaa hapa kumtukana ni kutokana na upumbavu wenu tu, viongozi wenu wanaiba nchini na kupeleka nije wakati kagame anaiba nje kupeleka rwanda
 
Kusema ukweli kagame ni rais bora zaidi Africa kwa generation hiita mnaokaa hapa kumtukana ni kutokana na upumbavu wenu tu, viongozi wenu wanaiba nchini na kupeleka nije wakati kagame anaiba nje kupeleka rwanda
Mpumbavu mwenyewe kama anakumanua kimpango wako bwege wewe, unamsifia mwizi anaharibu amani ya maziwa makuu wewe unasifia upuuzi wake hapa.
 
Back
Top Bottom