Uchaguzi 2020 Paul Makonda achukua fomu ya Ubunge Kigamboni, kupitia CCM

Uchaguzi 2020 Paul Makonda achukua fomu ya Ubunge Kigamboni, kupitia CCM

Hapa ndipo JPM anapochemka. Mbele ya huyu jamaa anafyata mkia. Wakati RC wengine kawazuia wasigombee mfano Chalamila, au waachie madaraka lakini huyu jamaa na madaraka yake anagombea bila aibu kabisa na wasomi wapo ndani ya chama wanaangalia tu.

Sasa naamini hata kumtumbua yule naibu waziri wa afya Bw. ndungulile ambae pia ni mbunge wa kigamboni ilikuwa ni mchongo.
 
Bashite nae ajitosa ulingoni
109528030_333495841377170_2009440987613573230_n.jpeg
 
Wizara ya MNN ndiyo Wizara ambayo kwa mkuu yeyote wa Nchi humteua mtu ambaye kwake ni mtiifu na ndivyo huwa.

Kwa utabiri wangu Magufuli kwa sababu nilizozitaja hapo juu ni wazi bwana Makonda anazo sifa hizo na uwezekano wa yeye Makonda kuwa kiongozi wa Wizara ile ni mkubwa.

Muda utaongea.
 
Hapa ndipo Jpm anapochemka. Mbele ya huyu jamaa anafyata mkia. Wakati RC wengine kawazuia wasigombee mfano Chalamila, au waachie madaraka lakini huyu jamaa na madaraka yake anagombea bila aibu kabisa na wasomi wapo ndani ya chama wanaangalia tu.

Sasa naamini hata kumtumbua yule naibu waziri wa afya Bw. ndungulile ambae pia ni mbunge wa kigamboni ilikuwa ni mchongo.
Mbona mnamsakama sana huyu jamaa? Kwani ndie mkuu wa mkoa pekee aliyekazini kuchukua fomu?
 
Bila kujiuzulu Ukuu wa Mkoa?

Kwa hiyo ni Mkuu wa Mkoa pekee nchi nzima aliechukua fomu akiwa na madaraka yake yote ya Ukuu wa mkoa.

Na atapiga kampeni huku akiwa na Cheo Chake Cha Ukuu wa Mkoa kama Kawaida.

Kuna hatari Makonda akawa Mbunge, Mkuu wa Mkoa na Waziri kwa wati mmoja.
CCM wanaweza kufanya hivyo, imeshawahi kutokea awamu ya tatu ya mzee Ben. Kuna mama aliwahi kuteuliwa ivyo.
 
Hatimaye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa sana Paul Christian Makonda achukua fomu ya kugombea Ubunge Jimbo la Kigamboni.

Ngoja tumuite aje atuambie atapiga vp kampeni huku akiwa mkuu wa mkoa?

Na je huu ndo ule mwanzo wa uwaziri wa mambo ya ndani waliyopanga kwenye vikao vyao vya kihuni?

Vp akiwa mbunge ataendelea na uvamizi wa studio za watu?

Njoo huku mheshimiwa mbingunikwetu utujibu
 
Anapenda makikiii kamaa msaniii, hajachukua fomu.

..............ila kapiga picha na fomu.
 
Mkulu alisema mtumishi yoyote atakaegombea ubunge ni tafsiri kuwa haridhiki na cheo alichonacho na ni mtu mbinafsi na atamtumbua hapo hapo na huko atakapotangaza nia atambwaga na ona sasa leo kisu kimegonga mfupa kwakuwa huyu ndie mwanangu mpendwa ninaependezwa nae kwa kuongoza kikosi cha watu wasiojulikana na kuvamia Clouds kwa zana za kivita na ona sasa Mzee Mkubwa niko njiapanda sijui nimfanyeje mtoto wangu huyu mtukutu na sasa ameninyea mkono je niukate au sasa sijui iweje maana zoezi la vyeti feki liliishia hapo kwake na mengine mengi, huyu mwana kazi yake kuniharibia na kunichonganisha tu na wanyonge wangu na ona sasa amri yangu hii mpya nayo imeishia leo mtoto wangu keshaleta fungulia mbwa kabla ya muda sasa ni sadakalawe amina mwenye kupata apate gombania goli, je huyu kwanini aachiwe wengine waadhibiwe! kweli ngozi nyeusi ni wajinga kichwani tu ila wana matumbo makubwa yaliyonona kwa mafuta yatokanayo na kodi za wanyonge!

Je, inapendeza kuendelea na double standards za kutowaadhibu wasukuma wenzangu wanaoniharibia amri zangu na kuendelea kupoteza heshima yangu kwa wasomi na wazee wa chama ambao deep down in their hearts na wanaponong’ona huniona eti mimi mshamba japo nawanyoosha kweri kweri na wanalima kwa meno na wanaisoma namba nawashangaa wakinisengenya kwenye mazungumzo ya simu zao kuwa mimi ni mshamba naishi mjini ila kijiji hakijanitoka kichwani kama kina Maduhu na Maganga wakati mimi sitembei na redio kaseti kubwa mtaani nikipiga muziki inde monii kwa kelele kubwa? tuheshimiane ndugu zangu na kama ningeweza kuifungia mitandao ningeifunga kweri kweri!!

Watu kukaa kimya haimaniishi hawaoni na hawasikii ujinga unaoendelea nchini ni vile tu FFU wanabonda kweeeeri kweri!

Hongera kwake DAB kwa kutangaza nia, kila shetani na mbuyu wake strike the iron while it is hot!! kata pua uunge wajihi Bashite this is your time for your Godfather Karl Peters favours you!!
 
Back
Top Bottom