Paul Makonda amtaka mwandishi kumuuliza mama yake baada ya kumhoji tuhuma za kumshambulia Lissu

Hii kesi hakuna hukumu mpaka ijifie yenyewe uchaguzi ukianza.
 
Wanafahamika Wala usione police hawafuatilii ukadhani ni bahati mbaya. Kila kitu kinafahamika maana lilikuwa ni tendo la kishamba sana. Hicho nilichokuleza ndio mchongo mzima ulipo. Anachofanya huyo muhalifu Makonda sasa, ni kutumia platform hii aliyoipata kujisafisha kwa kufanya siasa za maigizo akitarajia watu watasahau.
 
Hahahaaaa ile dhambi itawatafuna wahusika woote hadi dahali
 
Wanapinga huku wakikuonyesha kadi zao? Sasa umejuaje kuwa wanaompinga sio wale wanaccm wenye akili zao timamu?
Maana pamoja na ccm kuwa mbovu lakini wapo wenye akili pia!
 
Huyu mwandishi mjinga sana tena sana. Na tena inatakiwa ashughulikiwe tujue ana cheti halali cha uandishi. Wewe Lisu mwenyewe alishasema Dkt Magufuli alituma watu wakamuue halafu tena wewe mwandishi unaenda kumuuliza mtu mwingine ni akili kweli??!
Maswali ya mihemko kwa kuhitaji sifa.
 
Kwa Kesi za Jinai, mwenye ushahidi anazuiliwa kuupeleka Polisi?

..kwenye post yako iliyopita ulishauri Lissu apeleke ushahidi mahakamani. Sasa naona umebadilika unashauri apeleke ushahidi Polisi.

..Polisi wakifungua uchunguzi wanaweza kuwaita watu wote wenye ushahidi na taarifa zinazoweza kuwanasa waliohusika.

..Lakini kwa mwenendo wa Polisi wetu kuhusu tukio lile nadhani njia nzuri ni Raisi kuunda TUME YA UCHUNGUZI ili iweze kufuatilia kilichotokea.

..Tume ninayopendekeza ni kama ile aliyounda Rais Kikwete iliyoongozwa na Jaji Kipenka kuchunguza tukio la wafanyabiashara wa madini waliouawa wakituhumiwa ni majambazi.
 
Halafu huyu unadhani akihojiwa huku ametumbuliwa macho makavu atakatiza huyu? Mbwembwe tuu za ofisi za umma lakini hakuna ujasiri wowote.
 
Sasa mnakwenda kuhoji nini wakati mna majibu?πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Hata mahakamani kabla ya hukumu lazima mahojiano.

Sasa

Ukisikia kesi inaendeshwa mtaani kwa wananchi badala ya mahakamani, ndio hivyo, ikifika hukumu ni hukumu, taratibu hata miaka 20 ikipita mtaani hakuna formula. Nyie lichukulieni poa , Jambo hali wanawezakuja kuwajibika vitukuu wenu wasio na hatia
 

..wakati wa kampeni za 2020 Mama Samia alisema kwamba risasi 3 za walenga shabaha wa serikali zingetosha kumuua Lissu.

..sasa maadam Lissu hakufa, basi Mama Samia aka'hitimisha kwamba waliohusika sio watu wa serikali.

..Mimi nadhani kuna makosa ktk hoja ya Mama Samia. Ni makosa kuhitimisha kwamba serikali hajahusika kwa kuangalia ushahidi wa idadi ya risasi zilizotumika.

..Na wanaoituhumu serikali wamezingatia mambo mengi mengine ikiwemo kuondolewa kwa walinzi wa serikali eneo la tukio, kuondolewa kwa CCTV camera za eneo la tukio, serikali kukataa wachunguzi toka nje, etc.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…