Paul Makonda amtaka mwandishi kumuuliza mama yake baada ya kumhoji tuhuma za kumshambulia Lissu

Paul Makonda amtaka mwandishi kumuuliza mama yake baada ya kumhoji tuhuma za kumshambulia Lissu

Mahakama zipi, hizi zenye kesi ya kina Mdee zaidi ya miaka minne Sasa na ushahidi wote upo lakini hakuna hukumu? Ingekuwa ni mahakama za kimataifa kule ambako hazipewi maelekezo hapo sawa. Maana kwenye mahakama za kimataifa huko hata serekali huwa haitoboi maana hazipokei amri toka juu. Rejea kauli ya Rostam kuhusu mahakama zetu.
Hii kesi hakuna hukumu mpaka ijifie yenyewe uchaguzi ukianza.
 
Kweli ni rahisi sana, lakini ni kimaongezi zaidi kuliko kimatendo.

Ukweli mwingine ni tukio la kishamba sana na ujinga wa hali ya juu na aliyelipanga ni wazi hakudhamiria kuua na hajui kuua.

Naomba uhai niwepo siku ya kujulikana huyo planner na aliowatuma kumaliza kazi.
Wanafahamika Wala usione police hawafuatilii ukadhani ni bahati mbaya. Kila kitu kinafahamika maana lilikuwa ni tendo la kishamba sana. Hicho nilichokuleza ndio mchongo mzima ulipo. Anachofanya huyo muhalifu Makonda sasa, ni kutumia platform hii aliyoipata kujisafisha kwa kufanya siasa za maigizo akitarajia watu watasahau.
 
Makonda amehojiwa na mwandishi wa habari kwamba Lissu amesema ulihusika na shambulia lake Dodoma

Jibu amepewa kamhoji MAMA YAKO

Bashite ameshindwa hata kukana kwamba hakufanya lile tukio, ni wazi jibu la kwanza ilikuwa ni kukataa kuhusika

Damu ya mtu ni nzito bana.

Hahahaaaa ile dhambi itawatafuna wahusika woote hadi dahali
 
Sasa mbona tunamshambulia Makonda kuliko hao wenye mamlaka ya uteuzi?! Watu wanaotakiwa kuumia zaidi ni wanachama wa CCM, wajitokeze wapinge uteuzi wake.

Kwa kelele hizi kutoka kwa mahasimu wao kisiasa watajivuna uteuzi wao ni sahihi hata kama una madhara.
Wanapinga huku wakikuonyesha kadi zao? Sasa umejuaje kuwa wanaompinga sio wale wanaccm wenye akili zao timamu?
Maana pamoja na ccm kuwa mbovu lakini wapo wenye akili pia!
 
Huyu mwandishi mjinga sana tena sana. Na tena inatakiwa ashughulikiwe tujue ana cheti halali cha uandishi. Wewe Lisu mwenyewe alishasema Dkt Magufuli alituma watu wakamuue halafu tena wewe mwandishi unaenda kumuuliza mtu mwingine ni akili kweli??!
Maswali ya mihemko kwa kuhitaji sifa.
 
Kwa Kesi za Jinai, mwenye ushahidi anazuiliwa kuupeleka Polisi?

..kwenye post yako iliyopita ulishauri Lissu apeleke ushahidi mahakamani. Sasa naona umebadilika unashauri apeleke ushahidi Polisi.

..Polisi wakifungua uchunguzi wanaweza kuwaita watu wote wenye ushahidi na taarifa zinazoweza kuwanasa waliohusika.

..Lakini kwa mwenendo wa Polisi wetu kuhusu tukio lile nadhani njia nzuri ni Raisi kuunda TUME YA UCHUNGUZI ili iweze kufuatilia kilichotokea.

..Tume ninayopendekeza ni kama ile aliyounda Rais Kikwete iliyoongozwa na Jaji Kipenka kuchunguza tukio la wafanyabiashara wa madini waliouawa wakituhumiwa ni majambazi.
 
Kwa shambulio la kishamba vile haiwezi kuchukua zaidi ya siku Moja. Ni rahisi kabisa, wataanza na nani aliagiza askari waliokuwa wanalinda gate kuondoka. Kisha watataka kujua Makonda alikuwa wapi siku ya shambulio la Lisu. Mawasiliano yake na ya RPC wa Dodoma yatafuatiliwa, hapo mchezo utakuwa umeisha.
Halafu huyu unadhani akihojiwa huku ametumbuliwa macho makavu atakatiza huyu? Mbwembwe tuu za ofisi za umma lakini hakuna ujasiri wowote.
IMG_20200326_031355.jpg
 
Sasa mnakwenda kuhoji nini wakati mna majibu?😂😂😂
Hata mahakamani kabla ya hukumu lazima mahojiano.

Sasa

Ukisikia kesi inaendeshwa mtaani kwa wananchi badala ya mahakamani, ndio hivyo, ikifika hukumu ni hukumu, taratibu hata miaka 20 ikipita mtaani hakuna formula. Nyie lichukulieni poa , Jambo hali wanawezakuja kuwajibika vitukuu wenu wasio na hatia
 
Inapofikia hatua kwa mtu/watu walio hai kuweka lawama na visingizio vya kukwama kwao kwa Maiti ambayo mpaka sasa ni hakika imebaki mifupa, ni dhahiri mwisho wa kutenda na fikra umefikiwa.


Kwamba Rais wa JMT aliewatoa gerezani watuhumiwa wa Ugaidi na Uhujumu uchumi anakosa uwezo kimaamuzi wa kufungua upya jarada la uchunguzi wa tukio la jaribio la mauaji? Unayatambua Mamlaka yake na mipaka yake vizuri?

Unaikumbuka kauli ya Rais Samia wakati wa kampeni za 2020 kuhusu shambulio hilo? Kamsikilize tena, uenda ukaelewa.

Hao wapasha Habari wa Lissu walishindwa kabisa kumuokoa kwa kumpasha Habari ya kushambuliwa kwake kabla ya tukio?

..wakati wa kampeni za 2020 Mama Samia alisema kwamba risasi 3 za walenga shabaha wa serikali zingetosha kumuua Lissu.

..sasa maadam Lissu hakufa, basi Mama Samia aka'hitimisha kwamba waliohusika sio watu wa serikali.

..Mimi nadhani kuna makosa ktk hoja ya Mama Samia. Ni makosa kuhitimisha kwamba serikali hajahusika kwa kuangalia ushahidi wa idadi ya risasi zilizotumika.

..Na wanaoituhumu serikali wamezingatia mambo mengi mengine ikiwemo kuondolewa kwa walinzi wa serikali eneo la tukio, kuondolewa kwa CCTV camera za eneo la tukio, serikali kukataa wachunguzi toka nje, etc.
 
Back
Top Bottom