Paul Makonda awa kiongozi wa kwanza kuzuiwa kuingia Marekani kwa kuwanyima watanzania HAKI YA KUISHI

Paul Makonda awa kiongozi wa kwanza kuzuiwa kuingia Marekani kwa kuwanyima watanzania HAKI YA KUISHI

Nimeona taarifa kwamba mkuu wetu wa mkoa ni kinara wa kukiuka haki za binadamu

Je C.I.A wamemchimba vya kutosha na wakawasilisha faili lake kwa Trump ? Kwa nini kama kweli wana ushahidi wasimpeleke ICC? Kama wao ni wanaume,tukutane ICC au watoe hati ya kumkamata

Na kama kuna mtu mnamtafuta ila mmeanzia mbali,mseme
this ban against Bashite is based purely on informed sources/resources.
 
Huu ndio wakati muafaka kwa Watanzania kusimama na rais, maana anatafutwa kwa namna zote, wanataka wamdhoofishe ili waendelee kubeba madini maana yeye ndiye mzalendo wa kwanza kupambana dhidi yao, alifanya kitu ambacho hakijawahi kufanywa na kiongozi yeyote Afrika, leo hii Waafrika wote wanamtegemea kuona kama atashinda kwenye haya mapambano, ili na wao waliamshe.
 
FBI kwa kushirikiana na CIA na watanzania ambao ni wakala wao ambao wapo Nchini wamekusanya data za unyama, unyanyasaji na uonevu wao wote, sasa wanaanza na Bashite kisha wengineo watafuata kabla hawajatuma drone kuja kuwasalimia kimya kimya.
 
Hawa mabeberu waache kuingilia mambo yetu ya ndani, watuachie uhuru wetu.. Wao nani anawaingilie kwenye mambo yao..

USA hatuendi sio lazima, zipo nchi nyingi za kwenda zenye amani kuliko huko USA wanakouana kila siku..

Hapo unaongea kama ww au kama makonda?
 
Back
Top Bottom