Paul Makonda awa kiongozi wa kwanza kuzuiwa kuingia Marekani kwa kuwanyima watanzania HAKI YA KUISHI

Pompeo anayajua zaidi ya hayo
Sent using Jamii Forums mobile app
 
We kwenda zako huko yani mie nife kwa kumtetea bashite?
 
Sasa kumnyima Visa ya kuingia Marekani ndo watazuia juhudi zake na serikali kupiga vita madawa ya kulevya na genge la madawa ya kulevya paomoja na ushoga? Ataendelea tena kwa saana kwasababu amewashika pabaya! Moja ya mikakati ya USA ni kuungana na magenge ya uhalifu wa kimataifa kuzinyongonyeza nchi masikini ili wapore mali na utajiri wa nchi za kiafrica. Moja ya mbinu inayozitumia marekani ni pamoja na kusupport magenge ya madawa ya kulevya kuingizwa katika nchi masikini kuharibu vizazi ili kutengeneza mwanya wa kuzipora rasilimali zao!
 
Juzi kati kondom tu zilikua hadimu watu wakaanza kulialia.
Swali: Hivi una umri gani?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ujue kila mtoto chini ya miaka 5 huwa anaona baba yake bonge la swaziniga. Yaani huwa wanaamini hata lije jambazi la aje baba atalibonda.

Mdogo wangu ukikua kidogo tu utatambua hata huyo baba yetu na swaziniga wetu anawaogopa kishenzi hao jamaa.
 
Mbona USA ilimnyima haki ya kuishi yule jenerali wa IRANI?Tusiwe kasuku
Wairan wanatuhusu nini sisi, sisi wanatuuma Watanzania wenzetu wanaonyimwa haki ya kuishi na Makonda na genge lake. Tunawalilia Watanzania wenzetu Azory Gwanda na Beny Saanane waliopotezwa kwa sababu tu ya uwajibikaji wao. Tuanze kujadili Iran na Iraq tuache kujadili kuuawa kwa Mawazo na kutekwa na kuteswa kwa Mdude? Kwani tumeanza Jana kusema mnaua Watanzania wenzetu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa mabeberu waache kuingilia mambo yetu ya ndani, watuachie uhuru wetu.. Wao nani anawaingilie kwenye mambo yao..

USA hatuendi sio lazima, zipo nchi nyingi za kwenda zenye amani kuliko huko USA wanakouana kila siku..

Ukishapigwa ban na marekani hujue na nchi nyingine itakuwa issue kupata visa.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tutembee kifua mbele sisi ni donor country πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Basi na nyie wawekeeni vikwazo. Lakini pia angalia USA hawakuficha juu ya hilo. Basi Makonda nae aweke wazi nani kamnyima haki ya kuishi.

Na usisahau kwa Makonda ni jambo linalohusu Watanzania wenzetu
Katazo hili kwa kiasi kikubwa tunaweza kusema ni kuhusu kauli zake kwenye mambo ya ushoga. Tangu atoe lile tamko la kukurupuka, nchi za Magharibi hazikufurahishwa kabisa.

Haya mengine wameyaweka tu kwani wanajua wangesema tu ni ushoga basi wananchi wengi wange-react negatively! Tusidanganyane eti wamekasirishwa na manyanyaso yake kwa raia. All in all, wakulaumiwa hapa ni rais mwenyewe.

Huyu Makonda alikwishaonyesha kabisa ni mtu asiye na busara ya uongozi, hafanyi kazi yoyote bali ni msanii na mabovu mengine mengi lakini kwa sababu anazojua aliyemteua hataki kumwondoa. Hata wananchi wengi wa Tanzania hawampendi na Makonda mbaya zaidi anasababisha chuki kati ya serikali na wananchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…